Meneja wa TRA Kigoma asimamishwa kazi

Bikirajohola

JF-Expert Member
Jun 11, 2022
356
632
Meneja wa TRA mkoa wa Kigoma bwana Gabriel Mwangosi amesimamishwa kazi na kamishina mkuu wa TRA bwana Alphayo Kidata baada ya kupandisha ushuru wa forodha mkoani humo kutoka millioni 15 kwa mwezi hadi millioni 300 kwa mwezi!

Alichokifanya bwana Mwangosi alipofika Kigoma ni kuziba mianya yote ya upigaji na kuwaelekeza wafanyabiashara wote kulipa mapato halali TRA na kupata risit halali matokeo yake mapato yakapanda maradufu kitendo ambacho kiliwakera wakubwa ikiwemo wafanyabiashara wakubwa na kuamua kumzushia zengwe na hatimaye amesimamishwa kazi na mapato ya forodha mkoani humo yameshuka tena na kuwa vilevile millioni 15 kwa mwezi!.

Ni kama tu Sabaya alivyoikuta wilaya ya Hai ikiwa ya 144 kwenye mapato na kuipandisha mpaka ikawa ya nne kitaifa lakini akaishia kuzushiwa zengwe na kupelekwa mahakamani. Jambo hilo la wazalendo kutafutwa kwa tochi na kuzushiwa mazengwe limemkera mbunge Tabasamu na kukataa kuomba radhi kwenye mwongozo wa waziri Simbachawene.

 
Meneja wa TRA mkoa wa Kigoma bwana Gabriel Mwangosi amesimamishwa kazi na kamishina mkuu wa TRA bwana Alphayo Kidata baada ya kupandisha ushuru wa forodha mkoani humo kutoka millioni 15 kwa mwezi hadi millioni 300 kwa mwezi...
Huyo meneja ni bonge la tapeli hakuna lolote huyo kamishna amefanya vyema sana na ilitakiwa muda huu awe Kisongo kule alipopelekwa Sabaya ili ukawafananishe vizuri
 
Meneja wa TRA mkoa wa Kigoma bwana Gabriel Mwangosi amesimamishwa kazi na kamishina mkuu wa TRA bwana Alphayo Kidata baada ya kupandisha ushuru wa forodha mkoani humo kutoka millioni 15 kwa mwezi hadi millioni 300 kwa mwezi...
Uzalendo wa kuumiza watu siyo uzalendo na ikumbukwe kuwa Sabaya hawahi kuwa ofisa wa TRA hata siku moja.
 
Kupindisha mapato sio sababu pekee ya kubakia kwenye cheo, je hayo mapato ni kiasi gan yanalandana na utaratibu sahihi wa TRA?

Unapandisha mapato kwa milioni 300 kwa kushinikiza penalty na hapohapo unagundulika unaiba mamilioni.
Maguu style....unaje ga barabara ndio ila una 30% kwa mradi
 
Hata kama kafanya unyang'anyi kwamba serikali iendelee kumuacha tu kisa kaongeza pato kwa njia za wizi na unyanganyi!

Unapomkaribia mfanyabiashara kodi zaidi ya anayotakiwa kulipa kisa upate sifa haujengi ila unabomoa!

Mwisho wa siku biashara zinakufa kabisa, kodi hazitakuwepo, ajira hazitakuwepo serikali haitapata chochote!! Ukiwa unaona kwenye pua tu utafurahia kukamua miaka miwili mitatu baada ya hapo kila kitu kitakuwa kimekwisha!

Wafanye kazi zao kwa halali, wawatendee watu haki, watoze watu kodi za haki si kukomoa kwa sifa!!

Watu wakiopo serikalini siyo wapumbavu wana akili pia, wanajua hicho unachofanya ni sawa au sawa!
 
Kupindisha mapato sio sababu pekee ya kubakia kwenye cheo, je hayo mapato ni kiasi gan yanalandana na utaratibu sahihi wa TRA?....

Huwezi kupandisha mapato kwa njia za unyanganyi ukafikiri kwamba unatenda sawa!! Karma lazima ikurudie maana kuna watu wengi utakuwa unawaumiza kwa namna isiyo halali!!

Watendaji wa TRA wafanye haki
 
Sabaya ameshinda kesi zote mahakamani
Sabaya hakushinda kesi bali kulikuwa na mapungufu ya kiufundi ya kisheria ambayo kitaalamu yanafanya mwenendo wote wa kesi uwe siyo sahihi.

Yani ukiambiwa mfano hati ya mashtaka ina mapungufu haina maana kwamba Sabaya hakutenda makosa bali utaratibu wa kuwasilisha mashtaka umekiuka utaratibu wa kiufundi wa kisheria.

Binafsi nilishangaa kwanza aliachiwa huru kivipi kwa makosa ya kiufundi ya kisheria wakati ilipaswa mahakama itoe utaratibu wa kufanya marekebisho ili kesi iwake vyema.

Good, rufaa imekatwa tena na kesi inaendelea kuwaka moto vyema.
 
Kupandisha mapato kuendane na kuzingatia sheria na haki za mlipa kodi. Kukusanya kodi isiwe chanzo cha kuvuruga utaratibu wa kisheria

Unaweza ukaenjoy kukusanya mapato kwa miezi michache halafu baadaye hali ikawa tete.
 
Sabaya hakujua majukumu ya mkuu wa wilaya ndo maana mwisho wake ni mbaya, Kama ma-DC wote wangefanya kama ya Sabaya basi nchi isingekuwa na uongozi.

Ili mumsaidie Sabaya simamieni hoja zenye mantiki na sio kusema kaonewa
Changamoto kupewa maagizo! Kwani kuna tofauti gani sasa Mkuu wa Mkoa wa Arusha kufanya yale yanayoendelea kule Loliondo?
 
Huyo meneja ni bonge la tapeli hakuna lolote huyo kamishna amefanya vyema sana na ilitakiwa muda huu awe Kisongo kule alipopelekwa Sabaya ili ukawafananishe vizuri
sema utapeli wake hapa!kafanya nini??otherwise ni story tuu
 
Meneja wa TRA mkoa wa Kigoma bwana Gabriel Mwangosi amesimamishwa kazi na kamishina mkuu wa TRA bwana Alphayo Kidata baada ya kupandisha ushuru wa forodha mkoani humo kutoka millioni 15 kwa mwezi hadi millioni 300 kwa mwezi...
Huyo hajasimamishwa Kuna Mambo yanawekwa sawa tu, anapangiwa sehemu nyingine ya kukamatia ugali.
 
Mliobakwa na kuvamiwa na Sabaya kama wewe hamjitokezi mahakamani kutoa ushahidi ndiyo maana anaachiwa huru kila siku na mahakama
Eti anaachiwa huru kila siku,nakukumbusha tu leo hii ameamkia kwenye kuta ndefu za Gereza la Karanga pale Moshi,sijui huko kuachiwa huru kila siku unakokuandika JF ni kupi?juzi kalia Mahakamani kwamba Jela si Picknic ni sehemu ya mateso halafu wewe unaandika utumbo JF!!nilishasema hata ukibadili ID kila siku lakini akili zako zipo mkunduni
 
Eti anaachiwa huru kila siku,nakukumbusha tu leo hii ameamkia kwenye kuta ndefu za Gereza la Karanga pale Moshi,sijui huko kuachiwa huru kila siku unakokuandika JF ni kupi?juzi kalia Mahakamani kwamba Jela si Picknic ni sehemu ya mateso halafu wewe unaandika utumbo JF!!nilishasema hata ukibadili ID kila siku lakini akili zako zipo mkunduni
Kama mliobakwa hamjitokezi ataachiwa tu tarehe 14
 
Kama mliobakwa hamjitokezi ataachiwa tu tarehe 14
Hata akiachiwa leo lakini cha moto amekipata,ule ubabe wake wote wa Moshi na Arusha HAUTAKUWEPO,kule kula Bata kwake kote kwa Moshi na Arusha akiwa na misafara yake tena akitumia namba za UN kwenye magari binafsi HAKUTAKUWEPO tena,nina uhakika hata akiona Kuku atakuwa anapiga magoti na kutoa SHIKAMOO,habari ndio hiyo
 
Duru zinatabanaisha meneja TRA Mkoa wa Kigoma aliyefukuzwa na Kidata walikuwa hawaivi tokea kipindi cha JPM.

Inasemekana taarifa za siri zilizopenyezwa Magogoni kumhusu bwana Kidata na zilizopelekea kufutwa ubalozi na kuvuliwa hadhi ya ubalozi mmoja wa wanyetishaji alikuwa huyo muhanga aliyefukuzwa kule Kigoma.

Ni wazi bwana Kidata kwa sababu za chuki binafsi na kutaka kumkomoa ilikuwa lazima amfute kazi!
 
Back
Top Bottom