Meneja wa kampeni UKAWA/CHADEMA hafai, aondolewe mara moja

Meneja wa kampeni UKAWA/CHADEMA hafai, aondolewe mara moja

dala dala

Senior Member
Joined
Nov 16, 2011
Posts
106
Reaction score
105
Zinaitwa Kampeni, na katika Kampeni za Kisiasa kuna njia kuu nne za kuwafikia wapiga kura ambazo ni;

1. Kukutana na wapiga kura moja kwa moja yaani Direct Voters Contact (DVC) kupitia Mikutano ya hadhara (Impact ni Ndogo kwa maana ya kuwafikia wapiga kura wachache)

2. Vipeperushi na machapisho (Still Billboards, Electronic Billboards, Posters na Leaflets); impact yake ni ya kati maana idadi ya watu wanaofikiwa ni wengi kiasi tena karibu kila siku;

3. Mass Media (Redio na TV). Njia hii ina impact kubwa kwani inawafikia watu wengi kwa mpigo, Katika hili CHADEMA na UKAWA wamefanya chini ya Wastani. Kwa mfano Mkutano wa leo Arusha watu wengi walijipanga kuufuatilia kupitia Vyombo vya Habari cha kushangaza hakuna linaloendelea. Jamani kushinda uchaguzi sio kazi nyepesi.

Kwa nini UKAWA haitumiii vyombo vya habari kuwafikia wananchi wengi? Njia nzuri na rahisi ni Redio kwani angalau kila kaya hapa nchini ina Redio maana hata simu (Feature Phone) zina Redio. UKAWA hamtumii hii njia hivi tatizo nini? Yaani leo mmeboa sana. Huyu Kampeni meneja wa UKAWA/CDM hafai kabisa. Kushinda uchaguzi kwa Mazingira haya si rahisi. Tusijidanganye!!. CCM wanatumia TV na Redio tena zile ambazo zinawafikia watu wengi. Amkeni jamani wananchi wanahamu ya kuwasikia na kusikia Sera zenu.

4. Mtu kwa Mtu, Hii hutumika katika scale ndogo ambapo wagombea hutembelea katika Kaya au maeneo ya mikusanyiko mfano Vituo vya Mabasi, Vijiwe nk. Njia hii ina impact ndogo sana.

USHAURI:
Kama tatizo sio fedha, basi huyo meneja wa Kampeni hafai kabisa anawashauri vibaya. Tanzania ina vijiji zaidi ya 20,000 (ishirini elfu), je mtavifikiaje vyote? Njia rahisi ni vyombo vya habari.

Ninashauri Mgombea wa Urais na Timu ya Kampeni Kitaifa afanye Press Conference kabla ya siku ya Kupiga KURA ili wananchi kwa upana waweze kumsikia. Tena hiyo Press conference irudiwe mara kwa mara. Vinginenvyo tutasema kura zetu zimeibiwa kumbe hatukujipanga vizuri. Huu ni ushauri wangu mpenda mabadiliko.

Kazi kwenu.
 
Hakuna siku waliyoonyesha dharau kwa wapenzi wao kama leo. Huyu tumaini Makene wamweke pembeni ama akajiunge na Dr Mihogo
 
Mkuu umenena yote. Binafsi nimekuwa nikijiuliza kama ni Lowassa kama Lowassa mwenyewe ndio anajisimamia na kujiendeshea kampeni hii kama atakavyo mwenyewe? au ni CHADEMA kama Chama? Kwani naona kama kuna walakini mkubwa hizi siku za karibuni kampeni yake imekuwa ikienda ndivyo sivyo kwani hata mashambulizi yanakuwa hafifu na limited ukilinganisha na CCM wanavyojitutumua sasa hivi.

Binafsi nilitaraji huu mwezi wa mwisho wangaliongeza kasi iwe kufa kupona na hata kuimarisha ile team ya mgombe mwenza lakini naona kama vile hasikiki tena kabisa kwa wananchi. Kwa kweli kuna hitaji marekebisho ya haraka sana kati kuendeshaji wa team ya kampeni.
 
Naunga mkono hoja 100% hakuna unafiki hapo umesema fact tupu! Hatutaki mchezo katika hili. What's wrong? Money? How much?
 
kuna hujuma imefanyika ..si bureee tatizo kingunge kaharibu kitendo cha kutangazwa atakuwepo kimesababisha vyombo vya habari viingiliwe kazi zao .........kingunge angefanywa kama suprise leoooooo...tatizo wamemtangaza sana hadi ccm wakaogopa leooo

Wamuogope kingunge kama nani?
Kwa lipi alilonalo LA kutisha!
ila niwasaidie ndugu zangu wenye akili wanawashangaa kumuona slaa na zito na lipumba kama takataka na kuinua shangwe na vigelegele kwa kingunge
Ni aibu,watu wanawacheka tu,
 
Mgombea anahujumiwa! Tumaini makene ni timu mihogo
 
Hakuna siku waliyoonyesha dharau kwa wapenzi wao kama leo. Huyu tumaini Makene wamweke pembeni ama akajiunge na Dr Mihogo

cheki sasa meneja campeni wakwao ila cheki anavyoporomoshewa matu.... UKAWA tumeshawazoea natusubr tu washindwe oct25. utaona yatakavyo mporomokea mny/k na mgombea wao siye yetu macho
 
nikweli mkuu inabidi ukawa wasome nyakati,mkutano mkubwa wa leo arusha,ktokuonyesha nitatizo kubwa,kama tatizo nihela wadau 2ngechangia,tatizo lingine nilamabango picha za mheshimiwa lowasa zimefifia,namabango mengine makubwa hayana picha ya lowassa kuna hujuma kubwa ktka media waratibu wa matangazo namedia wabadirishwe ushauri,wangu
 
Mkuu umenena yote. Binafsi nimekuwa nikijiuliza kama ni Lowassa kama Lowassa mwenyewe ndio anajisimamia na kujiendeshea kampeni hii kama atakavyo mwenyewe? au ni CHADEMA kama Chama? Kwani naona kama kuna walakini mkubwa hizi siku za karibuni kampeni yake imekuwa ikienda ndivyo sivyo kwani hata mashambulizi yanakuwa hafifu na limited ukilinganisha na CCM wanavyojitutumua sasa hivi.

Binafsi nilitaraji huu mwezi wa mwisho wangaliongeza kasi iwe kufa kupona na hata kuimarisha ile team ya mgombe mwenza lakini naona kama vile hasikiki tena kabisa kwa wananchi. Kwa kweli kuna hitaji marekebisho ya haraka sana kati kuendeshaji wa team ya kampeni.

Mkuu hakuna MTU wa hivyo kama mgombea mwenza hana msaada alikuwa kwetu mtwara ,na vikauri vyake vya chaliiiii kifo cha mende watu wakamuona wa hivyo,hana msaada,
 
Pale ukawa hasa chadema kwasasa imeshikwa na watu wajinga wenye upeo mdogo wa kufikiri mtu kama sumaye,mgeja,masha na Lowasa mwenyewe mnategemea nini? Lowasa yeye anajua kuhonga wapiga kura ndiyo mwisho wa yote.
 
kuna hujuma imefanyika ..si bureee tatizo kingunge kaharibu kitendo cha kutangazwa atakuwepo kimesababisha vyombo vya habari viingiliwe kazi zao .........kingunge angefanywa kama suprise leoooooo...tatizo wamemtangaza sana hadi ccm wakaogopa leooo

Mkuu kila nikikuona(comment yako) ni kuhujumiwa tuu.........
 
Kushinda uchaguzi kwa mwenendo huu WA kampeni ni NDOTO....
 
Tumaini Makene hana "kasi na viwango" vya 120 km/hr. Ni tatizo
 
nikweli mkuu inabidi ukawa wasome nyakati,mkutano mkubwa wa leo arusha,ktokuonyesha nitatizo kubwa,kama tatizo nihela wadau 2ngechangia,tatizo lingine nilamabango picha za mheshimiwa lowasa zimefifia,namabango mengine makubwa hayana picha ya lowassa kuna hujuma kubwa ktka media waratibu wa matangazo namedia wabadirishwe ushauri,wangu
Nyie acheni utani Lowasa anaumwa kama ataoneshwa mara kwa mara watu watamuona anavyotetemeka ndiyo maana wanacheza na akili zenu karaga baho na ubwenzi wako.
 
Wamuogope kingunge kama nani?
Kwa lipi alilonalo LA kutisha!
ila niwasaidie ndugu zangu wenye akili wanawashangaa kumuona slaa na zito na lipumba kama takataka na kuinua shangwe na vigelegele kwa kingunge
Ni aibu,watu wanawacheka tu,

Mlimdharau Sumaye ona anavyo wagarim, na sasa Mnamdharau Mzee kingunge Nakuambia atawagharm zaid, na si dhan kama Magufuli atapata hata 20%
 
Ni kwel kabisa. Lowasa anakuwa kama yeye ni mgombea binafsi bana. Wametuuz sana. Hii lkurugez ya habari inatuuz sana tena inahujumu ukawa.
 
Back
Top Bottom