Idugunde
JF-Expert Member
- May 21, 2020
- 6,273
- 6,637
Kauli kuwa maiti ziliokotwa kwenye viroba wakati wa utawala wa hayati JPM ni kauli nzito, sio kauli za kubeza hata kidogo.
Inaonekana Membe ana ushahidi wa kutosha na ana siri nzito juu ya hizi tuhuma.
Mpaka sasa baadhi ya Watanzania hawajulikani walipo. Inahisiwa waliuawa na kutupwa kwenye viroba. Membe ametoa msaada na mwanga mkubwa. Sasa huu ndio mwanzo na yeye awe msaada.
Huu ndio wakati wa kupata ukweli juu ya madhira mabaya ambayo Membe anadai Serikali ya CCM iliyafanya.
Inaonekana Membe ana ushahidi wa kutosha na ana siri nzito juu ya hizi tuhuma.
Mpaka sasa baadhi ya Watanzania hawajulikani walipo. Inahisiwa waliuawa na kutupwa kwenye viroba. Membe ametoa msaada na mwanga mkubwa. Sasa huu ndio mwanzo na yeye awe msaada.
Huu ndio wakati wa kupata ukweli juu ya madhira mabaya ambayo Membe anadai Serikali ya CCM iliyafanya.