Meli ya MV Skagit yazama

Wat did you expect? kwani waliohusika na uzembe wa kuzama kwa meli mwaka jana walifanywa nini? nchi hii bwana, uzenbe uzembe uzembe tu.....kama imewahi kuripotiwa kuwa meli hiyo ni mbovu je ilikuwa imetengenezwa? ilisimamishwa lini na kufunguliwa lini? nani aliyeidhinisha ianze safari? service ilifanyiwa lini mara ya mwisho?wapi? kwenye gereji bubu? hah what do you expect?
Subiri mtaona mengi katika nchi ambayo kuanzia baba, watoto na watumwa wao wa ndani wote ni wasanii!!!!!
 
Tanzania kama taifa tunachezea makali ya wembe,ukitukata hakuna wa kumlaumu!!!!!!
 
Innalilahi wa Ina ilaihi Rajiun,Hakika kwake tutarejea. Kumbe ndio ile ilizimika Nungwi? Hii balaa jamani!
 
Mh jana niliona taarifa ya habari kuwa ilivutwa sasa kama ilianza tena safari leo, watakuwa wamefanya makusudi kabisa .

Tajiri na wahusika wa meli hii ni wazi watakuwa na kesi ya kujibu ya mauaji ya makusudi.

labda kama sio TZ.......hapa ata Waziri anaeusika alitakiwa kuja kutoa maelezo kwa nini asijiuzulu ikiwa izi ajari zinafuatana..
 

Siyo chama ni uongozi hafifu!! Mimi siyo CCM (actually mimi ni CDM), lakini kwenye issue kama hii unapolaumu chama wakati unajua wazi kuwa ni uongozi, unawapa excuse wahusika. Hakuna hatua ya maana iliyochukuliwa kuadhibu wale waliosababisha vifo vilivyosababishwa na meli ya mwisho iliyozama. Sana sana serikali badala ya kufanya uchunguzi madhubuti na kueleza ukweli walikuwa busy wanajaribu kuficha kiasi cha abiria walipotea kwenye mkasa ule. Hadi sasa hakuna mahali popote nimeshaona namba kamili ya watu waliopotea. Kwani CCM imeanza kuongoza kipindi hiki tu? Mbona kwenye uongozi uliopita mikasa hii ilikuwa haipo kwa frequency hii? Same as corruption! Same as road accidents! Imezidi kwa sababu wahusika hawaogopi kuadhibiwa. Jiulize, kule Loliondo ni watu wangapi walipoteza maisha kwa sababu serikali ili-sanction kile kikombe cha babu? This is **** resulting from crappy leadership NOT the party. Tusikubali kuwaacha viongozi bila lawama wakati tunajua kuwa ubovu uko kwao.
 


Mimi sishangai kwa Tanzania kuendelea kutumia meli mbovu kwani viongozi wetu hawatujali. Magari mangapi yako barabarani yanabeba abiria lakini ni mabovu. Mungu tusaidie ifike 2015 tuondokane na CCM janga la Taifa.
 
Nilisikia ktk TV, kabla ya tukio hili, kuwa Mamlaka ya Hali ya Hewa ilitoa hadhari khs hali ya hewa ya leo, lkn cha ajabu hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kuzuia vyombo vya majini kusafiri au kwenda kufanya shughuli nyingine baharini, km uvuvi.
Milango ya saa sita na nusu mchana wa leo, palitokea a freak storm, upepo usio wa kawaida kabisa ulioambatana na vumbi hapa jijini Dar es salaam.
Ilibidi nikimbilie dirishani katika jengo la ghorofa ya kwanza hapa jijini ili nitazame kulikoni, maana muungurumo ulikuwa mkubwa.

Hii ni pamoja na ukweli kuwa toka asubuhi ya leo pamekuwepo na upepo usio wa kawaida.
Pale bandarini kwa hali hii chombo kisingeruhusiwa kuondoka.

Sasa sijui kama kuonya usafir wa baharini nani anchukua jukumu na kubeba lawama, liondolewe kwenye muungano!
 
Mkuu Mv Seagual ndiyo imezama leo na Mv Karama ilizima juzi usiku mbona imetangazwa na ITV jana.



aisee kumbe kuna nyingine ilipiga mzinga juzi!!!....basi bwana..
 
Image captured from above by a friend aliyekuwa kwenye ndege ndogo
Uki-zoom utaona watu in circles na maboya

sad event
 

Attachments

  • IMG_stun3.jpg
    51.6 KB · Views: 188
mara mv seagul mara mv karama....ni meli ipi hasa imezama?

Ni MV Kalama Mkuu. Ilikuwa na abiria approximately 200. Capacity yake ni 250. Inazo lifeboats za kutosha watu 300 na lifevests pia za kutosha 260. Wengi wameokolewa na habari nilizo nazo ni kuwa process ya kuokoa bado inaendelea.
 
Mkuu kwa nini unasema hii ni breaking news wakati huna taarifa kamili???? Subiri ukishakuwa na taarifa kamili ndo uanzishe uzi.

mbona unamind issue ndogo we unachotaka ni habari au?? kukosoa watu tu kwa issue za msingi acha gubu.
 
Ee Mungu wanusuru viumbe wako,
 
Kwa taarifa tu ni kuwa bado wako baharini, hawajaokolewa.
Meli iliyoenda kuwachukua/kuwaokoa (kilimanjaro) haijarejea..mawasiliano ni hafifu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…