Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 4,545
- 7,745
Meli ya MV Serengeti iliyokuwa imefungwa katika gati ya bandari ya Mwanza Kusini imezama upande mmoja wa nyuma majini usiku wa kuamkia leo Desemba 27, 2024.
Taarifa hiyo imetolewa na Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO)na kueleza kuwa MV Serengeti ilisimama kufanya safari zake mwaka 2016 wakati huo ikihudumu kati ya bandari ya Mwanza na Bukoba.
Aidha meli hiyo ni miongoni mwa zile zinazotarajiwa kufanyiwa ukarabati mkubwa katika kipindi cha mwaka wa fedha ujao.
TASHICO imesema inashirikiana na timu mbalimbali za wataalamu kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) na wadau wengine katika juhudi za uokoaji.
Taarifa hiyo imetolewa na Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO)na kueleza kuwa MV Serengeti ilisimama kufanya safari zake mwaka 2016 wakati huo ikihudumu kati ya bandari ya Mwanza na Bukoba.
Aidha meli hiyo ni miongoni mwa zile zinazotarajiwa kufanyiwa ukarabati mkubwa katika kipindi cha mwaka wa fedha ujao.
TASHICO imesema inashirikiana na timu mbalimbali za wataalamu kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) na wadau wengine katika juhudi za uokoaji.