Mdhamini wa harambee ya CHADEMA usiogope

Mwanajamii

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2008
Posts
7,063
Reaction score
71
Nadhani sote tunataarifa kwamba kuna tangazo linalorushwa na REDIO CLOUDS la kuhamasisha wanachama na wapenzi wa CHADEMA kukichangia chama hicho.


Taarifa RASMI zinasema Mwaandaaji wa sherehe hizo za kukichangia chama chetu ambaye ni moja ya hoteli moja maarufu jijini Arusha amewaomba viongozi wa CHADEMA waseme kuwa chama ndicho kinabeba gharama zote ila ukweli ni kwamba HOTELI ndiyo inabeba gharama zote. Aidha watu maarufu kama Wafanyabiashara ambao wako nyuma ya CHADEMA kukisaidia nao wameombwa kutotajwa hadharani kwa kuhofia biashara zao kupata matatizo.

Maoni yangu: Hakuna sababu yoyote ya Mmiliki wa Hoteli hii wala Wafanyabiashara kuogopa kwa sababu wapo Watu wengi wameonesha nia ya kukisadia CHADEMA na mambo yao yanakwenda poa tu, mfano mzuri ni SABODO.
 

spinning
 

Hamna mamlaka Tanzania inaweza ikaziingilia biashara za Sabodo ndugu yangu. Yeye anacheza na stock exchange market za Marekani, mimi niliye na duka kariakoo nikijifanya kuwa huru kuunga mkono Upinzani utaona jinsi TRA watakavyokuwa wafanisi kwenye biashara zangu na haitashangaza kuona nimegundulika nadaiwa kodi nilizozikwepa miaka ya 90, unachezea CCM wewe!!!!!
 
Habari yako ni nzuri, ila umeharibu hapo kwenye RED!
 
Michango kwa CHADEMA imekuwa mingi, hofu yangu ni kwa vipi viongozi wakuu wa Chama hicho wanatumia fedha hizo. Je ni kwa maslahi ya chama kweli? Mara kadhaa nimekuwa nikiliona gari lao moja aina ya vitara rangi nyeusi likiwa katikati ya jiji na vipaza sauti kuwaomba wananchi kuchangia chama. Hata hivyo leo tutakuwa pamoja katika harambee hiyo.
 

Ni kweli viongozi wakuu wa chama wanatumia fedha hizo kwa ajili ya kampeni
 
Spinning master, tangu lini mbunge wa CCM akawa mwanachama wa Chadema.
 
Wanachadema tujitokeze na kwa wale watakao shindwa kufika pale Naura tafadhali yuma mchango wango kwenye namba zifutazo....
 
hongera kwa hilo,ni hotel gani hiyo?

Mwenye Naura Spring Hotel amefanya kosa kubwa sana ambalo atakuja kulijutia katika maisha yake yote. Na tukumbuke huyu mwenye hii hotel anamiliki pia hotel ya Impala na Ngurdoto. Sijui km biashara zake zitaachwa salama na TRA
 
tutaanzisha kampeni ya kuchangia ccm tuone watanzania wanavyokichukulia chama kilichowalea.
kwa sasa tuma tigo pesa kwenda 0655736379.

nawakilisha.
 

Njia za kuchangia zitajulikana tu, kama mtu akitoa cheque itajulikana, kama ukitoa kwa njia za mtandao itajulika na hata njia ya TISS itajulikana. CCM wana mkono mrefu na wana organs nyingi zakutambua mambo.

 
Njia za kuchangia zitajulikana tu, kama mtu akitoa cheque itajulikana, kama ukitoa kwa njia za mtandao itajulika na hata njia ya TISS itajulikana. CCM wana mkono mrefu na wana organs nyingi zakutambua mambo.

Haogopi mtu hapa hata mkitisha vp
Tutakwenda eneo la tukio, na tutachanga!
Mbona ccm inachangiwa na hakuna anayebomolewa kibanda?
 
mbona chadema mnaogopa tabia ya kuogopa ni ya wahalifu.mwenye busara yeyote hawezi kuchangia vurugu kwa hata yeye hatakuja kuishi kwa amani.
 
tatizo ni wafanyabiasha kufanya kazi bila mipango mizuri, ukiwa na rekodi nzuri za biasha hata waje TRA unawatoa nisha tu
 
Spinning master, tangu lini mbunge wa CCM akawa mwanachama wa Chadema.

huyu jamaa mimi mwenyewe kanistua, memba wa cdm hawezi kuongea vitu hivi hadharani. Wanatafuta uhakika wa nani amefadhili hiyo harambee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…