Mdau wa Diaspora ajibu maswali kuhusu daraja litakalojengwa kutoka Dar hadi Zanzibar

Leslie Mbena

JF-Expert Member
Nov 24, 2019
207
677
MDAU WA DIASPORA AJIBU MASWALI KUHUSU DARAJA LITALOJENGWA KUTOKA DAR HADI ZANZIBAR.

Leo 19:15pm,28/12/2019

Kutokana na Mgongangano wa mawazo ili Watanzania tufikie lengo kuu lenye kuleta tija,Mdau wa Diaspora amejibu maswali kiufasaha kuhusu ujenzi wa daraja kutoka Dar hadi Zanzibar ili wadau waelewe nini hasa kimewapelekea kuomba ruhusu kwa Serikali ili waweze kujenga daraja hilo.

Mdau huyo akielezea hayo amesema tayari wana miradi saba kwa jumla ambayo wameazimia kuiwakilisha kuanzia mwaka ujao na yote imepitishwa katika azimio la utekelezaji.

Kiuhalisia daraja kutoka Dar hadi Zanzibar likijengwa litaingia kwenye Guinness book kama daraja refu kabisa linaloelea baharini kwa lugha ya beberu "the longest floating bridge" kwa sasa daraja refu kabisa lina 2km hili la Dar hadi Zanzibar litakuwa na 30km.

Tashwishi ni kubwa na maswali ni mengi kuliko majibu, na muda ni mchache na Watanzania waishio nje wameamua kujenga daraja hilo kuunga mkono juhudi za Rais Mzalendo kabisa,Daktari John Pombe Magufuli.

Swali la msingi kutoka kwa Mwananchi wa Tanzania aliyetaka kujua zaidi kuhusu ujenzi wa daraja hilo,ni kwamba ninyi Watanzania mnaoishi nje ya Nchi mnawezaje kwenda kuomba hela kwa wafadhili kuja kutekeleza suala kubwa kama hili ambalo ni kazi ya serikali na ninavyodhani serikali ingeomba fund za kutekeleza huu mradi nadhani ingekuwa ni rahisi zaidi kuliko nyie kama diaspora,kumbuka huu ni mradi mkubwa sana,ni hilo tu napenda kujibiwa,Ahsante.

Jibu langu la msingi ni hili,Sisi watanzania tunaoishi nje ya Tanzania, Diaspora tumekuja na wazo na kuiomba serikali itupe ruhusa ya kufanya utafiti ili majibu yake yatatupa gharama za ujenzi.Katika ujenzi kuna mbinu mbili ambazo zinaweza kutumika ambayo ni PPP hii anaweza hata Bakhresa kuingiza pesa na ingine ni maataasisi kama worldbank na mengineyo.
Kwa maelezo haya toka mwanzo watu hawataki kuelewa na kuanza kupindisha story.Hakuna mwanadiaspora atakaechangishwa hata buku.
Sasa wakejeli wasikejeli serikali ikiruhusu tu watu wajiandae kupiga Selfie kwenye Daraja.Haya ndio maelezo ya mwisho.

Mdau mwingine akauliza hivi,kuna tofauti ya tunnel na floating bridge.
19km bridge iliyojengwa na Russians na kuzinduliwa mwaka huu imegharimu dola 3.6bn sasa daraja kutoka Dar hadi Zanzibar ni 30km halafu ni floating na pia litapita juu, sasa hapo kuna njia za meli zitazibwa... naomba nipate official tamko kuhusu ujenzi wa daraja la Zanzibar to Dar kama ni la ukweli.

Jibu langu ni hili,katika kila ujenzi unatofautiana na Teknologi,kuna za bei ndogo na kubwa sasa kwa upande wa daraja la znz-dar majibu ya gharama yatapatikana baada ya upembuzi yakinifu.Daraja la Russia wao walitumia Teknologi ya Russia na hili tunatarajia kutumia teknoloji ya Nchi ingine.Katika swala la jinsi gani meli zitapita hili ni jambo jepesi sana kwani uwezekano upo na mfano ni kama huu katika picha hapo chini.

-Umuhimu wa daraja litalotoka Dar - Zanzibar.

Ni daraja ambalo lilitakiwa kujengwa siku nyingi hasa kwa sababu Zanzibar ni kituo kivutio kikubwa cha utalii duniani. Watalii wengi wanaishia Dar kwa sababu ya adha ya usafiri wa kuvuka kwenda Zanzibar.

Usafiri uliopo sasa ni wa boti ambao una mapungufu yafuatayo:

1. Wakati mwingine inabidi uwahi tiketi siku moja kabla.

2. Msongamano wa watu kwenye kupanda boti unafanya muda kamili wa safari kuwa ni zaidi ya masaa matatu.

3. Ratiba ni ya mchana tu. Chukulia uko Dar unataka kwenda Zanzibar saa kumi na mbili jioni unafanyaje? Au unataka kuanza safari saa tano kamili, muda ambao hakuna ratiba ya boti.

4. Usafiri wa vyombo vya abiria haupendelewi sana na watalii.

5. Boti za abiria hazibebi mizigo mingi.

Daraja linaondoa matatizo yote hayo. Mtalii anaweza kulala Double Tree Dar, saa nne na nusu akavuka daraja, saa tano yuko Zanzibar, akapiga picha zake saa tatu usiku akavuka daraja kurudi hotelini kwake Double Tree Dar.

Njia ya baiskeli ni kivutio kikubwa sana cha watalii. Wanaweza hata kufanya mashindano ya kuendesha baiskeli.

Daraja linaweza hata kuitwa daraja la muungano. Kwa sababu ni kiungo kinachounganisha bara na visiwani.

Ieleweke boti zinazovuka sasa hivi ni za binafsi. Siku moja kampuni ikisimamisha huduma kwa sababu yeyote ile usafiri utarudi kuwa ni wa vidau au ile meli kubwa ya zamani ya masaa sita kufika Zanzibar.

Nikiishia hapa,Mimi ni,
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854
 
Diaspora kwa faida wekezeni Chattle...biashara ni pasu pasu kwa muda muafaka

huku kwenye daraja hasara tarajiwa ni kubwa...

ukitilia maanani vile vikundi vya kigaidi,na uwezekano wa kulilipua..

bado muungano wenyewe ni shida shida na minongono ni mingi


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijapata ona wazo la kipuuzi kama hili .wafungue kampuni waitishemifund wajenge green house za kutosha wapangishe vijana welime mbogamboga wawakope pembejeo na wataalamu .kisha wakivuna watumie diaspora wao kuwapa soko la nje wataondoa umaskini mkubwa .sisi hatuna harks ya kwenda zanzibar eboo
 
Zanzibar yenyewe ni ndogo mnataka muweke daraja mtujazie nchi yetu iwe kama manzese..Kwasababu wagogo lazima wajae daraja zima kuombaomba!
 
Sijapata ona wazo la kipuuzi kama hili .wafungue kampuni waitishemifund wajenge green house za kutosha wapangishe vijana welime mbogamboga wawakope pembejeo na wataalamu .kisha wakivuna watumie diaspora wao kuwapa soko la nje wataondoa umaskini mkubwa .sisi hatuna harks ya kwenda zanzibar eboo
Hizo ni siasa ndugu. Hivi unaamini linajengwa kweli?
 
MDAU WA DIASPORA AJIBU MASWALI KUHUSU DARAJA LITALOJENGWA KUTOKA DAR HADI ZANZIBAR.

Leo 19:15pm,28/12/2019

Kutokana na Mgongangano wa mawazo ili Watanzania tufikie lengo kuu lenye kuleta tija,Mdau wa Diaspora amejibu maswali kiufasaha kuhusu ujenzi wa daraja kutoka Dar hadi Zanzibar ili wadau waelewe nini hasa kimewapelekea kuomba ruhusu kwa Serikali ili waweze kujenga daraja hilo.

Mdau huyo akielezea hayo amesema tayari wana miradi saba kwa jumla ambayo wameazimia kuiwakilisha kuanzia mwaka ujao na yote imepitishwa katika azimio la utekelezaji.

Kiuhalisia daraja kutoka Dar hadi Zanzibar likijengwa litaingia kwenye Guinness book kama daraja refu kabisa linaloelea baharini kwa lugha ya beberu "the longest floating bridge" kwa sasa daraja refu kabisa lina 2km hili la Dar hadi Zanzibar litakuwa na 30km.

Tashwishi ni kubwa na maswali ni mengi kuliko majibu, na muda ni mchache na Watanzania waishio nje wameamua kujenga daraja hilo kuunga mkono juhudi za Rais Mzalendo kabisa,Daktari John Pombe Magufuli.

Swali la msingi kutoka kwa Mwananchi wa Tanzania aliyetaka kujua zaidi kuhusu ujenzi wa daraja hilo,ni kwamba ninyi Watanzania mnaoishi nje ya Nchi mnawezaje kwenda kuomba hela kwa wafadhili kuja kutekeleza suala kubwa kama hili ambalo ni kazi ya serikali na ninavyodhani serikali ingeomba fund za kutekeleza huu mradi nadhani ingekuwa ni rahisi zaidi kuliko nyie kama diaspora,kumbuka huu ni mradi mkubwa sana,ni hilo tu napenda kujibiwa,Ahsante.

Jibu langu la msingi ni hili,Sisi watanzania tunaoishi nje ya Tanzania, Diaspora tumekuja na wazo na kuiomba serikali itupe ruhusa ya kufanya utafiti ili majibu yake yatatupa gharama za ujenzi.Katika ujenzi kuna mbinu mbili ambazo zinaweza kutumika ambayo ni PPP hii anaweza hata Bakhresa kuingiza pesa na ingine ni maataasisi kama worldbank na mengineyo.
Kwa maelezo haya toka mwanzo watu hawataki kuelewa na kuanza kupindisha story.Hakuna mwanadiaspora atakaechangishwa hata buku.
Sasa wakejeli wasikejeli serikali ikiruhusu tu watu wajiandae kupiga Selfie kwenye Daraja.Haya ndio maelezo ya mwisho.

Mdau mwingine akauliza hivi,kuna tofauti ya tunnel na floating bridge.
19km bridge iliyojengwa na Russians na kuzinduliwa mwaka huu imegharimu dola 3.6bn sasa daraja kutoka Dar hadi Zanzibar ni 30km halafu ni floating na pia litapita juu, sasa hapo kuna njia za meli zitazibwa... naomba nipate official tamko kuhusu ujenzi wa daraja la Zanzibar to Dar kama ni la ukweli.

Jibu langu ni hili,katika kila ujenzi unatofautiana na Teknologi,kuna za bei ndogo na kubwa sasa kwa upande wa daraja la znz-dar majibu ya gharama yatapatikana baada ya upembuzi yakinifu.Daraja la Russia wao walitumia Teknologi ya Russia na hili tunatarajia kutumia teknoloji ya Nchi ingine.Katika swala la jinsi gani meli zitapita hili ni jambo jepesi sana kwani uwezekano upo na mfano ni kama huu katika picha hapo chini.

-Umuhimu wa daraja litalotoka Dar - Zanzibar.

Ni daraja ambalo lilitakiwa kujengwa siku nyingi hasa kwa sababu Zanzibar ni kituo kivutio kikubwa cha utalii duniani. Watalii wengi wanaishia Dar kwa sababu ya adha ya usafiri wa kuvuka kwenda Zanzibar.

Usafiri uliopo sasa ni wa boti ambao una mapungufu yafuatayo:

1. Wakati mwingine inabidi uwahi tiketi siku moja kabla.

2. Msongamano wa watu kwenye kupanda boti unafanya muda kamili wa safari kuwa ni zaidi ya masaa matatu.

3. Ratiba ni ya mchana tu. Chukulia uko Dar unataka kwenda Zanzibar saa kumi na mbili jioni unafanyaje? Au unataka kuanza safari saa tano kamili, muda ambao hakuna ratiba ya boti.

4. Usafiri wa vyombo vya abiria haupendelewi sana na watalii.

5. Boti za abiria hazibebi mizigo mingi.

Daraja linaondoa matatizo yote hayo. Mtalii anaweza kulala Double Tree Dar, saa nne na nusu akavuka daraja, saa tano yuko Zanzibar, akapiga picha zake saa tatu usiku akavuka daraja kurudi hotelini kwake Double Tree Dar.

Njia ya baiskeli ni kivutio kikubwa sana cha watalii. Wanaweza hata kufanya mashindano ya kuendesha baiskeli.

Daraja linaweza hata kuitwa daraja la muungano. Kwa sababu ni kiungo kinachounganisha bara na visiwani.

Ieleweke boti zinazovuka sasa hivi ni za binafsi. Siku moja kampuni ikisimamisha huduma kwa sababu yeyote ile usafiri utarudi kuwa ni wa vidau au ile meli kubwa ya zamani ya masaa sita kufika Zanzibar.

Nikiishia hapa,Mimi ni,
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854
Daraja aina hii lipo Seattle Washington State US.
Linaitwa Evergreen Point Floating Bridge.
Urefu wake ni 2,350 meters tu! (sehemu inayoelea)
Ujenzi wake ulikamilika 2016
Lina njia (lanes) 6
Lina maboya (yanayoliwezeesha kuelea) ya zege 77 yenye uzito wa Tani 10,000 kila moja urefu mita 110, upana mita 23 na kimo mita 8 na nusu.
Maboya mengine 54 kila moja lina uzito wa tani 2,300 na kadhalika.
Gharama yake US $ 4.5 billions
Karibu sawa na bomba la mafuta toka Uganda mpaka Tanga!
Umbali Dar Zanzibar 90 km
Hiyo ni sawa na madaraja 39 ya Seattle!
Au madaraja 19 kati ya Bagamoyo na Zanzibar 45 km!

Garama sawa na 4.5×39= US $175.5 billions!
Ni kama T. Sh. 403,650,000,000
Hawa wanaojiita diaspora wa TZ achaneni nao ni washamba tu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio wote,huyo diaspora mmoja mpuuzi tu anayewazia kupiga cha juu ikipitishwa🤣🤣🤣
Sijawai kusoma jambo la kijinga km hili.
Mkimuona diaspora mwenyewe sasa mwenye hilo wazo.🙄🍗
 
Watu wajinga kweli "Eti ooh hakuna usafiri wa boti baada ya saa 12 jioni", kwani si wapande ndege. Hawa diaspora ni washamba na wanataka kufanya upigaji. Kazi ya ujenzi wa miundo mbinu ni ya serikali na kama mnataka nyie kujenga basi toeni kiasi cha gharama ielekezeni kwa serikali wajenge. Faqat

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wajinga kweli "Eti ooh hakuna usafiri wa boti baada ya saa 12 jioni", kwani si wapande ndege.

Anasahau kwamba hata ulaya usafiri ni kwa ratiba, anazungumzia mtalii kwenda kupiga picha darajani, naona hii haijakaa vema labda ingekwenda kwenye uwekezaji wenye ajira kwa vijana
 
Back
Top Bottom