Mdalasini na mtu mwenye sukari je inadhuru naomba msaada wajuzi.

Safari111

Member
Jan 29, 2012
6
1
Ndugu zangu , assalam aleikhum.

Napenda kuchukua nafasi kuulizia mtu mwenye sukari anaweza kutumia asali au kuna asali ya aina
nyingine ambayo siijui, naomba msaada wenu .
 
Safari, hizi issue nadhani ni vizuri kuongea na dr wako. Kuna matibabu ya aina mbali mbali kwa level tofauti za sukari, utaingia chaka hapa upate matatizo. Pole na kila la kheri. Be encouraged, ukifuata ushauri wa dr. Auntie yangu aliishi na sukari for 40 years na kilichomuua ni uzee!
 
Dawa ya ugonjwa wa kisukari


Upate aina za dawa zifuatazo, kila moja kiasi cha gram 100, saga
>>>>pamoja na dawa zifuatazo:
>>>>1. Shubiri
>>>>
>>>>2. Ubani
>>>>
>>>>3. Mvuje
>>>>
>>>>4. Ukwaju
>>>>
>>>>5. Habasoda
>>>>
>>>>(kiasi cha dawa hizi hazijatwangwa, hivyo jaribu kukadiria
>>>>mwenyewe) baada ya kusaga vizuri, gawanya katika mafungo matatu
>>>>yaliyosawa. Changanya fungu moja na maji kiasi cha chupa mbili na
>>>>uchemshe kwa dakika kumi. Ipua na iwache ipoe, chuja na hifadhi
>>>>katika chupa nadhifu.
>>>>
>>>> MATUMIZI YA DAYA YENYEWE
>>>>
>>>>Tumia kila siku kikombe kimoja cha kahawa kabla ya kula chochote
>>>>asubuhi kwa muda wa siku 13. Ikiisha dawa hii basi chukua fungu
>>>>la pili na uchemshe kama ulivofanya kwa fungu la mwanzo. Tumia
>>>>daya hii tena kwa muda ule ule wa siku 13.
>>>>
>>>>Itakapokwisha dawa hii basi chukua fungu la tatu na uitayarishe
>>>>kamaUlivyofanya mafungu mawili ya mwanzo. Tumia dawa hii kama
>>>>dawa hizo mbili za mwanzo ila tu kwa muda wa siku 14 , hii
>>>>itafanya jumla ya siku za kunywa daya kuwa siku 40.
>>>>
>>>>Baada ya siku hizo 40 utajisikia kuwa ugonjwa wa kisukari
>>>>umekwisha na unaweza kuanza kula vitu vyote ulivyokuwa
>>>>umekatazwa. Inshallah kwa kudra zake mwenyezi mungu utakuwa
>>>>umepona maradhi hayo.

Kuhusu Mdalasini haina madhara na mtu mwenye ugonjwa wa Kisukari au hata asali ukipata Asali safi haina madhara na mtu mwenye ugonjwa wa kisukari hiyo Asali safi mbichi. Tumia hizo dawa zangu hapo juu
kisha unipe Feedback.
 
Mwenye sukari???au mimi sijakuelewa au ni uandishi mchundo??kufuatana na swali lako namimi najibu hivyo hivyo,mwenye sukari anaruhusiwa kuwa na vitu hivi mdarasini,maji,jiko lakupikia na kijiko cha kukologea!nini baada ya hapo??ni chai nzito inayo nukia vizzzuuurrriiiii!!
 
Mwenye sukari???au mimi sijakuelewa au ni uandishi mchundo??kufuatana na swali lako namimi najibu hivyo hivyo,mwenye sukari anaruhusiwa kuwa na vitu hivi mdarasini,maji,jiko lakupikia na kijiko cha kukologea!nini baada ya hapo??ni chai nzito inayo nukia vizzzuuurrriiiii!!
Mkuu Kakakiza Mhusika wa hi thread hakukusudia sukari ya kutia kwenye chai la hasha kakusudia ugonjwa wa kisukari kwa kiingereza unaitwa diebetic

Diabetes mellitus is a condition in which the pancreas no longer produces enough insulin or cells stop responding to the insulin that is produced, so that glucose in the blood cannot be absorbed into the cells of the body. Symptoms include frequent urination, lethargy, excessive thirst, and hunger. The treatment includes changes in diet, oral medications, and in some cases, daily injections of insulin.
 
Asante sana ndugu kwa ukarimu wako , inshaalah nitajaribu na kwa uwezo wake mola inshaalah atanijaalia.
dawa ya ugonjwa wa kisukari


upate aina za dawa zifuatazo, kila moja kiasi cha gram 100, saga
>>>>pamoja na dawa zifuatazo:
>>>>1. Shubiri
>>>>
>>>>2. Ubani
>>>>
>>>>3. Mvuje
>>>>
>>>>4. Ukwaju
>>>>
>>>>5. Habasoda
>>>>
>>>>(kiasi cha dawa hizi hazijatwangwa, hivyo jaribu kukadiria
>>>>mwenyewe) baada ya kusaga vizuri, gawanya katika mafungo matatu
>>>>yaliyosawa. Changanya fungu moja na maji kiasi cha chupa mbili na
>>>>uchemshe kwa dakika kumi. Ipua na iwache ipoe, chuja na hifadhi
>>>>katika chupa nadhifu.
>>>>
>>>> matumizi ya daya yenyewe
>>>>
>>>>tumia kila siku kikombe kimoja cha kahawa kabla ya kula chochote
>>>>asubuhi kwa muda wa siku 13. Ikiisha dawa hii basi chukua fungu
>>>>la pili na uchemshe kama ulivofanya kwa fungu la mwanzo. Tumia
>>>>daya hii tena kwa muda ule ule wa siku 13.
>>>>
>>>>itakapokwisha dawa hii basi chukua fungu la tatu na uitayarishe
>>>>kamaulivyofanya mafungu mawili ya mwanzo. Tumia dawa hii kama
>>>>dawa hizo mbili za mwanzo ila tu kwa muda wa siku 14 , hii
>>>>itafanya jumla ya siku za kunywa daya kuwa siku 40.
>>>>
>>>>baada ya siku hizo 40 utajisikia kuwa ugonjwa wa kisukari
>>>>umekwisha na unaweza kuanza kula vitu vyote ulivyokuwa
>>>>umekatazwa. Inshallah kwa kudra zake mwenyezi mungu utakuwa
>>>>umepona maradhi hayo.

Kuhusu mdalasini haina madhara na mtu mwenye ugonjwa wa kisukari au hata asali ukipata asali safi haina madhara na mtu mwenye ugonjwa wa kisukari hiyo asali safi mbichi. Tumia hizo dawa zangu hapo juu
kisha unipe feedback.
 
Assalam aleikhum.

Nakusudia, mtu anaugonjwa wa sukari anaweza kutumia asali? Au kuna asali za aina nyingi.
 
Assalam aleikhum.

Nakusudia, mtu anaugonjwa wa sukari anaweza kutumia asali? Au kuna asali za aina nyingi.
Anaweza kutumia asali lakini asali yenyewe ina Masharti. kwanza hiyo asali ahakikishe ni Asali ya kweli yaani asali iwe Asali safi mbichi ambayo haijapikwa, na iwe asali ya ukweli sio iliyochanganywa na sukari kama zilivyo siku hizi hizi asali feki mimi huwa ninaziita. Asali Safi mbichi ya nyuki ni dawa kila maradhi Kwa research iliyofanyika tumeona katika asali kuna :
22 amino acids, 28 minerals, 11 enzymes, 14 fatty acids na 11 carbohydrates, kiwango cha vitu hivyo hupungua au huodoka kabisa ikiwa utavichoma kwa moto wa 150F.
Moisture 20.0% - calcium 5 mg
Protein 0.3% - Phosphorus 16 mg
Minerals 0.2% - Iron 0.9 mg
Carbohydrates 75.5% - Vitamins C 4 mg (samall amount of Vitamin B complex)
 
Faida ya Kutumia ASALI

Asali ni moja katika vitu tulivotunukiwa na Mola wetu ambayo ndani yake hutibu magonjwa yote ila mauti.

Inshallah tutaanza historia ya Asali kwa ufupi, Asali imetumika miaka elfu na zaidi huko nyuma katika mji wa Egypt watu wa Egypt walikuwa wakitumia asali katika kila jambo lao kwani walikuwa wakiamini kuwa sali inazidisha afya, pia walikuwa wakiweka katika makaburi ya wakubwa wao.. kwani asali hakiozeshi kitu chochote kile.

Kiwango na vitu vilivyokuwemo katika Asali (madini)
Sukari iliyomo katika asali ni glucose,fructose,na sucrose.
Glucose ni sukari ya kawaida ambayo imo katika katika miili au damu zetu na pia hupatikana katika matunda na mbogamboga.

Fructose pia inajulikana km ni grape sugar mvunjiko wake uko mwepesi zaidi ya glucose pia hujenga tissue katika mwili
Sucrose ni mchanganyiko wa glucose na fructose kiwango chake ni kidogo sana katika asali lakini inafanya asali ifanye kazi ya kusanga kwa muda mdogo.

Kwa research iliyofanyika tumeona katika asali kuna :
22 amino acids, 28 minerals, 11 enzymes, 14 fatty acids na 11 carbohydrates, kiwango cha vitu hivyo hupungua au huodoka kabisa ikiwa utavichoma kwa moto wa 150F.
Moisture 20.0% - calcium 5 mg
Protein 0.3% - Phosphorus 16 mg
Minerals 0.2% - Iron 0.9 mg
Carbohydrates 75.5% - Vitamins C 4 mg (samall amount of Vitamin B complex)


Umuhimu na faida za Asali
Asali ni moja katika nyanja ya ujoto na nguvu (energy) ni muungano wavyakula vya carbohydrates na asali ni moja katika inayosaga vyakula vya carbohydrates kwa wepesi mno.Huingia moja kwa moja katika mishipa ya damukwasababu ya viwango vyake.Viungo vyote vya mwili hufanya kazi bora asali inapoingia katika miili yatu yaani tukinywa au kujipaka.

Kijiko kimoja cha asali ukichanganya na nusu ya maji ya ndimu katika glasi ya maji ya safi ya uvuguvugu (yaani sio ya moto sana) ukinywa asubuhi hurudisha hamu ya kula na huondoa maradhi ya acidty.
Mchanganyiko wa asali na alcohol (hii sheikh nitapenda kuuliza je inafaa kwa waislaam??) inaaminika kuwa huzidisha kuota kwa nywele, inasemakana kuwa Japan hutumia sana kwa kufanya nywele zao kuwa silky yaani nyepesi na zenye rutba, huchanganyaka vijiko kadha vya aali (hutegemea na nywele zenyewe) hutia na alcohol kidogo na kuchanganya pamoja, hupaka katika nywele hadi kufikisha katika ubongo huwachia wka muda wa masaa 2 na baadae kukosha

Asali pia ni nuzri sana kwa wenye matatizo ya moyo, kwani asali inafanya msagiko wa mara moja katika mwili wala haileti madhara.Kwa wenye matatizo ya moyo ni vizuri sana ikiwa watakunywa asali mara tano kwa wiki chukua mfano kama wa sala ikifika time ya swala ukishaswali chukua kijiko kimoja unywe., pia kwa wenywe watatizo ya moyo hii huwa sababu ya

mafuta mengi mwilini au mzunguko wa damu kupungua kwa kasi flani au kuzidi kwa kasi fulani kwahivo wenywe matatizo wa moyo hawaruhusiki kabisa kufanya kazi nzito wala kutokula usiku ni lazima mtu ale usiku japo kdg na aende japo hatua mia ili chakula kizidi kusagika. Pia tunawashauri wenywe matatizo ya moyo wanywe glass moja ya maji liyochanganywa asali anda maji ya ndimu na pia kama utaamka usiku unywe tena,Asali husaidia katika maumivu ya mishipa ya moyo.


Kwa wenywe maradhi ya Anaemia (upungufu wa damu mwilini). Asali husaidia katika kujenga Haemoglobin katika mwili hii husababishwa kwa uwingi wa iron,copper na manganese, ni faida kubwa ikiwa asali itatumia katika matibabu ya anaemia inasaidia kuweka usawa wa haemoglobin katika red blood corpsles

Skin Disease asali pia husaidia katika wale wenye maradhi ya ngozi, pia husaidia kwa wale walioungua, Asali ukipaka katika mwili hurutubisha ngozi yako wala ngozi hiyo haizeeki mara moja pia ikiwa umeungua ni vizuri kupaka asali hapo hapo ndonda hupona mara moja na kovu huondoka

Oral Disease, asali husaidia kwa kuweka kinywa safi na cha afya. Paka asali siku zote katika meno na mafizi, inasafisha and kung'arisha meno, inasaidia katika kutoa udasi wa meno na pia husaidia uharibikaji wa meno na kutoka kwa meno pia hupigana na vijidudu vinavyoharibu meno. Kwa upande wa watu wenywe ulcer wachanganye asali na mdalasini kijiko kikubwa kimoja na anywe kila siku.

Matatizo ya macho Asali ni bingwa kwa ajili ya macho, Paka asali katika macho huzidisha nuru ya macho, pia husaidia katika matibabu ya trachoma, conjuctivits na maradhi mengine ya macho, kila siku paka asali kaika nje ya jicho na ndani ya jicho (kwa ndani ya jicho unaweza kutumia unyoya au wa kuku au ndege yoyote yule)kufanya hivo asali hupigana na kujilinda na maradhi ya glaucoma.

Asali
pia husaidia kwa matatizo ya cataract, chukua 2 grams ya maji ya vitunguumaji na asali uchange pamoja upake hii kwa wale wenywe immature cataract.

Matatizo ya matumboAsali ni muhimu kwa kuweka matumbo katika hali ya uafya, inasaidia kufanya digestion na kuepusha maradhi ya matumbo pia hupunguza hydrochloric acid ambayo husababisha kichefuchefu au kutapika pia husababisha kuumwa kwa moyo na pia hulainisha choo.

Old age asali husaidia kuleta ujoto na nguvu katika mwili wakati wa uzee. Kijiko kimoja cha asali au 2 katika kikombe cha maji ya yaliochemshwa (uvuguvugu) inasaidia na kutoa nguvu mwili.

Sexual Debility, Asali huzidisha hamu na huzidisha mbegu za kiume yaani sperm, asali inaaminika ni kmama magical yaani dawa ya maajabu huzidisha uzazi kwa mwanammke na huzidisha hamu kwa mwanamme (kwa wenye wake inawafaa hii) Hurudisha nguvu za kiume.

Source. P.h.D. Mzizimkavu https://www.jamiiforums.com/jf-doctor/184017-faida-ya-kutumia-asali-2.html#post3071961
 
Back
Top Bottom