Mdahalo Star Tv: Nape, Jussa na Marando

Mdahalo Star Tv: Nape, Jussa na Marando

Mkuu, hali kama hiyo hutokana na mfumo uliopo na jinsi anayeuongoza alivyo na mtazamo, japokuwa succession plan inapaswa iwepo ktk mtindo wa scouting!!! Mwl Nyerere hakuwa muunmin wa mfumo kama huu lkn aliweza ku-scout kimtazamo who shall be next ktk line up kiuongozi kv Sokoine, Kawawa, Msuya hata Mkapa je hao walikuwa watoto wake?

Akina Makongoro wametokea jashini.kimsingi naungana nawe Mkuu, kwamba Nape hakutumia hekima kujibu!!!!! Binafsi nilishtuka baada ya kusoma na kutambua kuwa Puttin kumbe babu yake alikuwa mpishi mkuu wa Lenin na Baba yake alikuwa runner wa Lenin hivyo Putin kuwa rais Urusi haikuwa bahati mbaya ni mfumo tu.

TAKE NOTE!!!
 
Nafikiri wakati mwingine ukipewa nafasi ambayo itakupa shida katika kutekeleza majukumu unapaswa kusema nafasi hii si ihitaji kwani Nape kama yeye ni kijana ambaye angeweza kuwa na mafanikio kwenye siasa kabla ya kungia kwe huu mkenge ambao ni mugumu na nafikiri huu utakua mwanzo wa yeye kufanya vibaya kwenye medani ya siasa.
 
NAPE ni jeshi la mtu mmoja, mnaweza kuanzisha thread kwa kila mstari wake jana.
 
Nape hana shida, tatizo yuko kwenye jahazi bovu,magamba mbona yanazidi kuwa magumu?
 
yule dogo ni hopeless sana hana jipya....hata jusa alikuwa hajibu majibu y msingi kama maswali yanvyotaka..........
 
Moja, Hongera mama, seems una kipaji cha mipasho, hapo kwenye red panaweza kukupa ajira leo tena au kile kipindi cha mitaarabu cha tbc.

Pili, Mitazamo inaweza kutofautiana. Nape ni mzungumzaji mzuri. Lakini ili uelewe kama anaongea pumba au point ni lazima na wewe uwe unajua mambo, lazima ufahamu wako uwe sawa na wake katika hilo jambo au ufahamu wako uwe mkubwa zaidi katika hicho anachokizungumza, kama wewe mwenyewe kichwani ni mweupe umeumia, na hiki ndicho kilichomkumba nipe tano na kwa hili nitatoa mifano.

1. Nape anasema CCM inaamini na kutekeleza sera za ujamaa, Tofauti kubwa kati ya sera hizi tatu, yaani ubepari, ulibelari na ujamaa ni namna uchumi wa nchi unavoendeshwa, nani anamiliki uchumi. Sifa mbili kubwa za sera ya Ujamaa ni uchumi kumilikiwa na umma na kujikita katika kupunguza tafouti ya kipato kati ya mtu na mtu, Je hiki ndicho CCM wanachosimamia, Nipe tano unaelewa nachozungumza au nshakupeleka kina kirefu? sema tu mama niko tayari kukuelekeza taratibu, sitaki kumuacha mtu nyuma

NOTE: Hakuna Ujamaa wa kisayansi na ujamaa wa kiafrika, hapa msiojua ndio nape anapowapiga bao, mnashabikia tu.

2.Kwamba serikali yake inajitajidi kuwamilikisha wananchi ardhi, yeye akasema eti huku ndio kumilikisha wananchi uchumi, kuna matatizo mawili hapa, moja hii si kweli hata kidogo kwamba serikali inajitahidi kumilikisha wananchi uchumi, Unajua nini kinatokea katika MKURABITA na kinachotokea katika UBINAFSISHAJI na kuna kile kingine wanaCCM wanakipenda sana UWEKEZAJI? kila kimoja ni page nyingi kama nikiamua kuvieleza. Pili, hata kama hii ingekua kweli (Kwamba seikali inajitahidi kuwamilisha watanzania uchumi wao) bado tusingekua tunatekeleza itikadi za ujamaa kwa sababu tungekua tunauacha uchumi wetu mikononi mwa mtu mmoja mmoja, na katika hali hii nguvu ya soko ndio inaamua mambo (huu ni ubepari na sio ujamaa), unakumbuka mwezi wa pili JK alivochemka na kupanga bei ya sukari, leo (miezi sita tu badae) sukari inauzwa sh ngapi?, Unakumbuka kuhusu mafuta mwanzo mwa august leo wiki tatu tu badae mafuta yanauzwaje? nguvu ya soko inaamua mambo na sio order kutoka state house!

Sijaribu kusema ubepari ni mbaya la hasha ila ninapata mashaka kama nape anajua anachokiongea na kama wanaomshangilia wanajua wanachoshangilia.

Mwandhishi wa comment hii ni mchumi kuanzia 2006, anajua vizuri kuhusu UJAMAA, ULIBELARI na UBEPARI, kama tukidiscuss kila kimoja labda utachoka kusoma, ila kwa kifupi NAPE anachanganya sana mambo, kama anashindwa kunifikia anaweza kupata ushauri kwa JUSA bse yeye alionekana anaelewa vizuri tofauti ya hizo itikadi tatu




Bora umesema Uswe, sasa nataka nimsikie Nipe Tano anasema nn! Hii sio sehemu ya mipasho...!!!!
 
ili kwa uwezo wa Nape asingeliweza kulikwepa labda kujibu kwa ubabaishaji juu juu
 
Hata mimi nilivoangalia niliona Jussa kawabwaga wenzake tena kwa asilimia kubwa,sasa nashangaa unakuja na hoja kama hiyo au tuseme ndo ule msemo si chongo ni kengeza,na ndio maana mara nyengine nakua sipendi kupita hata njia hapa siku hizi maana watu kama nyinyi mnatuharibia ile JF yenyewe hasa,ushabiki mbele halafu ndo ukweli... lol! kazi kweli kweli.
 
Kwa maono yangu naona wote wamejitahid kwa kuwa walikuwa wanawakilisha itikad za chama na wala si zao. Naona tuwapongeze. Wote hawakujibu maswal kwa kiwango cha kuwasifu. Siasa za bongo bado, tunajikongoja.
 
Nilimshuhudia nape akijikanyaga na maswali kwa kushindwa kusema mlengo wa ccm kwa sasa na sikweli ccm haipo katika ujamaa na kujitegemea bali ipo katika ubepari jambo jingine nape kazidi kutudanganya kua ccm inatoka hapo ilipo kwa mafanikio na kutupeleka kuleee!!

Tusipokujua nahisi pekee na chama chake ndio wanakujua.ni vizuri tuliweke wazi kua kwa sasa tumechoka na ccm hatutaki kwenda kule watupelekako kwasababu hapa tulipo ni miaka 50 sasa wameshindwa mfano hata ile misingi mizuri ya mwl wameshindwa kuindeleza e.g reli,ndege,meli,barabara n.k
 
Tumwelewe NAPE vizuri, kulinganisha Marekani na TZ ni ujinga eti George Bush family , sijui Clinton etc. Hawa hawaingii madarakani kwa ajili ya matumbo yao kama wakwetu!

Nape anamaanisha mtoto wa kiongozi wa CCM anakubalika zaidi kuliko sakala mwingine. Hiyo ni special credit ya CCM ni hatari kwa Taifa. Ndio sababu kama sio kwa kelele za Sitta ,Slaa , Mtikila na wanaharakati WENGINE Ridhiwani alianza kwa nguvu kutafuna "QURANI". Tunaona palipofikia kwa Saad Gaddafi na pia Mubarak.

CCM ni hatari sana ina maana kwa watanzania wote 44 milioni wale waliozaliwa hawana nafasi zamkuongoza na wale tu wapo karibu na viongozi ndio wataendelea kuwa viongozi hii ndio chain tunayotakiwa tuikate kwa namna zote. Mifumo yetu ya uwajibikaji haiendani na watoto au ndugu wa vigogo kuwa viongozi. Tuone Mfano wa kiburi cha waziri wetu wa mambo ya ndani Hussein Mwinyi amesema SIJIUZULU ingawa mwanzoni aliahidi angejiuzulu.

HII NI HATARI JAMANI.
 
jamani tuwe wakweli marando kwa upande wetu alichemsha sana ila kama tu mnataka kusafisha safisheni kwa kweli JUSSA wa CUF aliwafunika sana marando na nape.
 
si vibaya mtoto wa kiongozi kuwa kiongozi lakini lazima kusiwepo ushawishi wa baba yake katika kumpatia uongozi mwanae
 
Kurithishana uongozi, kuteuana kindugu, kirafiki, kwa kulipa fadhila n.k kuna madhara makubwa sana kwa taifa hapo baadaye.
Ni muhimu sana ku maintain social mobility ambapo watu wa lower class wanaweza kupanda daraja hadi middle class na middle class kufika upper class and the opposite.

Kujaribu kulinda watu wa tabaka la juu tu kwa kurithishana uongozi ni kuandaa bomu litakalolipuka wakati ujao.
Watu wa tabaka la chini wakiona hakuna kabisa uwezekano wa kupanda kufika tabaka la juu, kama hawana mawazo ya kitumwa, watachukua uamuzi mmoja tu na ambao utakuwa sahihi, kufanya mapinduzi kwa gharama yoyote ile.
 
Kusema ukwel mi cdm
Bt mjadala wa jn jussa alijitahidi sn ingawa alitoka off point baada ya kuanza kuponda cdm n sumhw ccm
Mabere marando did wel ze gud ov em alikuwa anaenda straight 2ze point ya maswal hakwenda kujungua wenzao km wenyewd walivofanya
N abt kute2a mafisadi amerock ile mbaya 1st ile ni kaz ukiachilia usiasa n addtn vle nivijidagaa WAPI MAPAPA?
Nape namsifu anaconfidence yakuongea ht km anajimingo amejitahidi hana asila km magamba wengine wakipigwa maswal
Zey ol tried jaman!Au co?
 
Hatakama munaipenda CDM kiasi hicho ila kuweni wakweli muda mwingine! Sote tumeona jinsi Marando alivyogaragazwa, labda kulikuwa na midahalo miwili!
 
Kusema ukwel mi cdm
Bt mjadala wa jn jussa alijitahidi sn ingawa alitoka off point baada ya kuanza kuponda cdm n sumhw ccm
Mabere marando did wel ze gud ov em alikuwa anaenda straight 2ze point ya maswal hakwenda kujungua wenzao km wenyewd walivofanya
N abt kute2a mafisadi amerock ile mbaya 1st ile ni kaz ukiachilia usiasa n addtn vle nivijidagaa WAPI MAPAPA?
Nape namsifu anaconfidence yakuongea ht km anajimingo amejitahidi hana asila km magamba wengine wakipigwa maswal
Zey ol tried jaman!Au co?

Unaweza kutafsiri kwa kiswahili au kiingereza ili tuweze kuelewa?
 
Hata kiziwi angeulizwa angekujibu ccm 16%, chadema 18%, cuf 66%,
jusa aliwa-outnumber kabisa wenzie, aliweza kueleza mambo mengi ya msingi kwa upana na kwa muda mfupi. Alijibu chochoko zote na propaganda dhidi ya cuf. Pale kwa vyovyote chadema hawakupenda, na kwa zile hoja za cuf hata kama ccm wangemleta nani na chadema wakamleta nani wangetoroka mjadala.
Jusa ni jembe la ukweli, yeye na mtatiro ni vijana wa kutegemea sana ndani ya cuf japo jusa ana uzoefu mkubwa wa mambo ya kimataifa na kitaifa kuliko mtatiro.
Kwa tulioangalia mjadala ule huku mwanza tumepata funzo kubwa sana. Cuf ikiendelea kujipanga namna hii itakuwa tegemeo la watanzania.
 
Back
Top Bottom