Nyambala
JF-Expert Member
- Oct 10, 2007
- 4,465
- 1,170
Dk. Slaa, Sitta kuvaana ruksa - Makamba
na Irene Mark
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba, amerudia kauli yake inayowazuia wagombea wa nafasi mbalimbali ndani ya chama hicho kushiriki kwenye midahalo aliyodai kushirikisha wenye njaa.
Pamoja na zuio hilo, Makamba ametoa ruhusa kuwepo kwa mdahalo kati ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta (CCM) na mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa.
Alisema hayo mjini Dar es Salaam jana alipokutana na waandishi wa habari ofisini kwake na kuwaeleza msimamo wa chama hicho kutoruhusu wagombea kushiriki midahalo wakati huu wa kampeni.
Alisema wanaotaka mdahalo na wagombea wa CCM wanatakiwa kumwomba kwa niaba na kupanga mada husika, maswali na kujua washiriki wa mdahalo huo ili kuepuka makundi ya wenye njaa.
Kuhusu ombi la Spika Sitta kukutana na Dk. Slaa kwenye mdahalo, Makamba ameruhusu, kwa maelezo kwamba wanasiasa hao wamepakana matope, hivyo ni ruksa kwao kujisafisha.
Alisema si busara kunyamaza unapopakwa tope na mwanasiasa mwenzako, hivyo Sitta ambaye pia ni mgombea ubunge wa Urambo Mashariki, ameruhusiwa kufanya mdahalo ili kujibu mapigo.
Hivi wewe mtu akikupaka tope utanyamaza? Huwezi, lazima ujipanguse halafu ulirudishe tope lile lilikotoka... hiyo ndiyo siasa bwana, si kunyamaza tu unatakiwa kujibu, alisema Makamba huku akinukuu baadhi ya mistari ya kwenye Biblia.
Source: Tanzania Daima
My take:
Makamba is truly a joke!!!!!!!!, Mgombea uraisi afanye mdahalo na mgombea urais period. Hii sasa inadhihirisha ni namna gani JK alivyo mwoga kwa debate.
na Irene Mark
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba, amerudia kauli yake inayowazuia wagombea wa nafasi mbalimbali ndani ya chama hicho kushiriki kwenye midahalo aliyodai kushirikisha wenye njaa.
Pamoja na zuio hilo, Makamba ametoa ruhusa kuwepo kwa mdahalo kati ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta (CCM) na mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa.
Alisema hayo mjini Dar es Salaam jana alipokutana na waandishi wa habari ofisini kwake na kuwaeleza msimamo wa chama hicho kutoruhusu wagombea kushiriki midahalo wakati huu wa kampeni.
Alisema wanaotaka mdahalo na wagombea wa CCM wanatakiwa kumwomba kwa niaba na kupanga mada husika, maswali na kujua washiriki wa mdahalo huo ili kuepuka makundi ya wenye njaa.
Kuhusu ombi la Spika Sitta kukutana na Dk. Slaa kwenye mdahalo, Makamba ameruhusu, kwa maelezo kwamba wanasiasa hao wamepakana matope, hivyo ni ruksa kwao kujisafisha.
Alisema si busara kunyamaza unapopakwa tope na mwanasiasa mwenzako, hivyo Sitta ambaye pia ni mgombea ubunge wa Urambo Mashariki, ameruhusiwa kufanya mdahalo ili kujibu mapigo.
Hivi wewe mtu akikupaka tope utanyamaza? Huwezi, lazima ujipanguse halafu ulirudishe tope lile lilikotoka... hiyo ndiyo siasa bwana, si kunyamaza tu unatakiwa kujibu, alisema Makamba huku akinukuu baadhi ya mistari ya kwenye Biblia.
Source: Tanzania Daima
My take:
Makamba is truly a joke!!!!!!!!, Mgombea uraisi afanye mdahalo na mgombea urais period. Hii sasa inadhihirisha ni namna gani JK alivyo mwoga kwa debate.