MDAHALO: Elimu ya Msingi iwe miaka 5 halafu Middle School then Secondary na High School...

mfumo uliopo bado ni mzuri tatizo lipo kwa wasimamizi wa mfumo huu,wazazi na mwanafunzi mwenyewe.



Kiufupi serikali imeshindwa kudhibiti madhara ya utandawazi.leo hii ukikatiza kwenye vituo vya daladala jaribu kuhesabu matangazo ya '''elimu ya sekondari kwa miaka miwili''' yalivyo mengi na hakuna kiongozi yoyote aliyewahi kuelezea suala hili.

Walimu ni sehemu ya tatizo kwa sababu wanafundisha wasichokipenda na wasichokijua.

Wazazi wa siku hizi hawafuatilii maendeleo ya mtoto shuleni.wazazi hawana muda wa kufundisha watoto wao.wazazi hawashawishi watoto wao wasomee au wapende fani fulani fulani.

Wanafunzi wa sasa wana nyenzo nyingi za kusomea lakini kutwa atakuwa kwenye facebook,video game,kukariri mashairi ya hussen machozi na tamthilia za amerca kusini.hata hivyo vyote hivi sio tatizo iwapo kuna ratiba inayompatia muda wa kujisomea.

Mwisho napenda kupinga hoja ya mwanakijiji kwa sababu bado hatujajua kiukamilifu ni nini hasa chanzo cha kuanguka kwa wanafunzi wetu.
Nashauri ufanyike utafiti katika maeneo yote yanayohusu elimu ili tujue tatizo liko wapi hii ndio njia pekee ambayo ni sahihi na salama ya kubadilisha mfumo wa elimu nchini,hakuna haja ya kudesa kwa wakenya.
Hapo kwenye red ni kudanganyana.Hivi kweli bado hatujui kwa nini wanafunzi wanafeli?
Walimu wana mazingira duni kama mishahara isiyokidhi,taaluma ya ualimu ni ya watu waliofeli form four wanaenda crash course miezi 6 kisha wanakuwa walimu.tena hakuna monitoring performance kwa hao walimu...etc..tujaribu kutatua hayo kwanza
 
Mi naona miaka miwili ya mwanzo watoto wavumbuliwe vipaji pamoja na kujifunza kusoma, kuandika + lugha. Baada ya hapo kila mwenye kipaji chake aendelezwe huko na wale ambao hawana vipaji waandaliwe kuwa taaluma zao tangu awali, kama uhasibu, ujasiriamali, etc.
 
gi tufanye hata miaka mi 3 tu inataosha ...muhimu ni kujua kuandika na kuhesabu hela basi vijana wakajiari wakati bado wadogoooo
sawa sawa, you train them to fish and not the best practices of fishing.
 
sio kaazi kwelikweli, huyu Jamaa anapoint kubwa sana na ndio practically fruitfull kuliko mambo mengine yote yatayotulia muda kwenye hii mada.

mkuu mimi siamini kama kili mtanzania anaweza kuwa msomi!hivyo ni vyema kwa serikali kujikita kwenye jambo moja.......kutengeneza wasomi(hawa ni wachache) ambao ni cream ya taifa.
Pili naona mambo ya ujuzi(vocational training )ingeachwa kama jukumu la sekta binafsi au wawekezaji au wazazi.kipindi tulichonacho ni kigumu sana kwani huwezi kumlazimisha dogo awe daktari wakati anaona msanii wa bongofleva anakula good time na gari zuri la kutembelea.hivyo ni lazima tukubali kuinvest kwenye kundi dogo la wenye uwezo kielimu litakaloongoza kundi kubwa la vilaza wenye ujuzi.
 
Mzee MKJJ unachofikiria samahani kwa kuingia kwenye mawazo yako ni sawa na kocha wa mpira kubadili formation ya 4-4-2 na kuwa 5-4-1 ili timu ishinde, kitu ambacho hakitasaidia kama wachezaji hawana kiwango kinachotakiwa. Tuboreshe kwanza walimu wetu miundombinu ya elimu sio hawa walimu wa voda fasta mwalimu anakuwa trained kwa mwezi mmoja (manufacturing teachers) ataweza nini hata kama utambadilishia structure.
MKJJ, wachangiaji wametoa mwanga mzuri wa wapi pa kuanzia... kifupi 'government intervention' inahitajika kwa kiasi kikubwa kubadiri hali mbaya katika sekta ya elimu. Kwa mtazamo wangu, kuna vitu viwili muhimu ambavyo Serikali na wadau wa elimu tunatakiwa kupigana navyo kwa sasa:
  1. ubora wa walimu
  2. mitaala ya kufundishia.

Tatizo kubwa la ubora wa walimu limetokana na Siasa zilipoingizwa kwenye sekta ya elimu. Wengi wametoa mapendekezo manzuri ambayo kwa ujumla ni Serikali ijirudi na kuhachana na mipango ya kisiasa kwenye masuala yanayoathiri vizazi. Lazima upanuzi wowote katika sekta ya elimu uendane na utafiti na majadiliano ya wazi kabla ya hatua kuchukuliwa.

Suala la mitaala ya kufundishia kwa sasa linatia kinyaa... sasa hivi kuna shule zinafundisha somo la sayansi kwa watoto wa darasa la kwanza, wanaoanza kujifunza kusoma na kuandika! Suluhu ni lazima turudishe vyombo tulivyokuwa navyo zamani, ambapo wakaguzi walipita mashuleni kuhakikisha elimu inatolewa kukidhi mahitaji na malengo ya Taifa. Serikali itambue kuwa si wazazi wote wanaufahamu mzuri wa makuzi ya kielimu kwa watoto; wengi wanapeleka watoto shule kutimiza wajibu. Turudishe chombo kitakachowasaidia wazazi kuhakikisha elimu anayopewa mtoto inaendana na hatua za ukuaji wa mtoto na isisababishe mtoto achukie shule.
 
Hapo kwenye red ni kudanganyana.Hivi kweli bado hatujui kwa nini wanafunzi wanafeli?
Walimu wana mazingira duni kama mishahara isiyokidhi,taaluma ya ualimu ni ya watu waliofeli form four wanaenda crash course miezi 6 kisha wanakuwa walimu.tena hakuna monitoring performance kwa hao walimu...etc..tujaribu kutatua hayo kwanza

sababu unayotoa yaweza kuwa mojawapo lakini tunahitaji kuthibitisha.tatizo linalotukabili ni uvivu wa kuamua mambo bila kuwa na msingi wa maamuzi yetu au kusema mambo bila kuwa na takwimu.ninachojaribu kikisisitiza ni kufuata kanuni za kawaida za kutatua matatizo na sio kuangalia rais,waziri au wazee wa kimila wana maoni gani.ni lazima tutafiti kwanza tatizo la kushuka kwa elimu lipo?limeanza lini?limesababishwa na nini?limemuathiri nani na kwa kiasi gani?ni njia gani zifaazo kutatua tatizo hili na zitatugharimu kiasi gani au muda gani?kuna njia mbadala na kama ipo inaweza kugharimu kiasi gani?kwa nini njia A ni bora kuliko B na C.kimsingi ifanyike situational analysis ya suala la elimu kabla hatujaanza kujadili mfumo gani unatufaa.
 
mkuu mimi siamini kama kili mtanzania anaweza kuwa msomi!hivyo ni vyema kwa serikali kujikita kwenye jambo moja.......kutengeneza wasomi(hawa ni wachache) ambao ni cream ya taifa.
Pili naona mambo ya ujuzi(vocational training )ingeachwa kama jukumu la sekta binafsi au wawekezaji au wazazi.kipindi tulichonacho ni kigumu sana kwani huwezi kumlazimisha dogo awe daktari wakati anaona msanii wa bongofleva anakula good time na gari zuri la kutembelea.hivyo ni lazima tukubali kuinvest kwenye kundi dogo la wenye uwezo kielimu litakaloongoza kundi kubwa la vilaza wenye ujuzi.
Kweli mkuu, elimu yetu bado ni ya holela tunaweza kuwa na mission lakini hatuna vision yeyote lengo letu (la serikali) ni lazima watoto wote waende shule (basic education) yes lakini baada ya shule waende wapi hatujui. Wenzetu ulaya wameshavuka level ya education 4 all sasa wana target kwenye soko husika, walimu wangapi wanahitajika, mainjinia wangapi wanahitajika kwa mwaka gani, ndio maana utakuta wana uwezo wa kuchagua walimu au bank tellers waliofaulu vizuri. Wewe ukitoka huku na cheti chako eti cha BA(ed) UDSM ni vigumu sana kupata kazi ulaya ya kufundisha kwa sababu hukuwa kwenye budget yao.
 
Nadhani watu wanamiss point iliyofichika; suala la quality ya elimu linaenda na structure ya elimu hiyo.... mfumo ambao ninaudokeza unapresume kuwa mambo mengine nayo yatabadilika kuenda sambasamba nayo.. Kwangu mimi issue ya quality sasa hivi inakuwa ngumu vile vile kutokana na structure yenyewe ya elimu...
Mzee MKJJ huu mdahalo ni mzuri, ungekuwa bora zaidi kama ungepanua wigo, wewe umeubana kwenye structure ya elimu ndio maana wengi wanaanzia kwenye ubora wa elimu ndio wanakuja kwenye structure. Huwezi kuzungumzia stucture ya elimu bila kuzungumzia ubora wa elimu lakini unaweza kuzungumzia ubora wa elimu bila kugusia structure. Mimi nafikiri, mdahalo ungezungumzia ubora wa elimu ya msingi kwa ujumla wake hili la structure ungeliweka kama moja ya factors zinazoweza kuathiri au kuchochea huo ubora.
 
mkuu mimi siamini kama kili mtanzania anaweza kuwa msomi!hivyo ni vyema kwa serikali kujikita kwenye jambo moja.......kutengeneza wasomi(hawa ni wachache) ambao ni cream ya taifa.
Pili naona mambo ya ujuzi(vocational training )ingeachwa kama jukumu la sekta binafsi au wawekezaji au wazazi.kipindi tulichonacho ni kigumu sana kwani huwezi kumlazimisha dogo awe daktari wakati anaona msanii wa bongofleva anakula good time na gari zuri la kutembelea.hivyo ni lazima tukubali kuinvest kwenye kundi dogo la wenye uwezo kielimu litakaloongoza kundi kubwa la vilaza wenye ujuzi.

Kiongozi, historia ya nchi yetu imetawaliwa na uwepo wa wasomi wachache, matokeo yake ndio kuwa na watendaji wazembe kupita kawaida, dawa ni kusomesha as many Tanzanians as possible ili ku create displine katika utendaji na kuondoa kabisa dhana ya ungu mtu kwenye maeneo nyeti.

Nakubaliana na wewe kwamba kwa hali yetu ya sasa ya kiuchumi itatuchukua muda mrefu sana kuweza kusomesha vijana wetu kwa wingi kwa wakati mmoja, lakini hata hao wachache wanaosoma sasa basi wapate elimu bora, ndio maana MM Kaja na mtaala wake tuujadili.
 
Kiongozi, historia ya nchi yetu imetawaliwa na uwepo wa wasomi wachache, matokeo yake ndio kuwa na watendaji wazembe kupita kawaida, dawa ni kusomesha as many Tanzanians as possible ili ku create displine katika utendaji na kuondoa kabisa dhana ya ungu mtu kwenye maeneo nyeti.

Nakubaliana na wewe kwamba kwa hali yetu ya sasa ya kiuchumi itatuchukua muda mrefu sana kuweza kusomesha vijana wetu kwa wingi kwa wakati mmoja, lakini hata hao wachache wanaosoma sasa basi wapate elimu bora, ndio maana MM Kaja na mtaala wake tuujadili.
mkuu naomba nijaribu kuweka point yangu vizuri.
Ninaposema 'wasomi' simaanishi mtu aliyemaliza form six au chuo na kuajiriwa pekee.hapa ninamaanisha watu waliosoma vizuri na kupata uwezo wa kufanya tafiti mbalimbali,watu wenye uwezo wa kutengeneza sera na miongozi mbalimbali ya jinsi gani ya kufanya uchumi wetu ukuwe na kuendeleza watu wetu,ni jinsi gani ya kuweka vipau mbele,ni jinsi gani ya kujilinda,ni jinsi gani ya kupambana na changamoto za afya yetu kutokana na mazingira na resources tulizo nazo,sera zetu za mambo ya nje au mahusiano yetu na nchi nyingine ziwe vipi ili tunufaike na sio kuwa washiriki n.k kwa maneno mengine wasomi ni watu watakaokuwa na uwezo wa kutufanya kujulikana kama wa tanzania,ikiwezekana ifike mahali who,world bank au imf watumie sera na mipango yetu kama mfano kwa wengine.hili haliwezi kufanywa na watanzania wote bali kikundi kidogo cha watanzania ambacho kimewezeshwa,kuaminiwa,kuheshimika na kupewa jukumu hilo kubwa.
Sisemi kwamba hawa wengine hawafai but lazima wapate waongozaji.kwa mfano sasahivi tumeona watoto wanavyoizimikia bongofleva mpaka wanashusha mistari kwenye mtihani je kuna mtu aliyeweka mikakati thabiti ya kuhakikisha huyu mtoto anakuwa mburudishaki mahiri wa bongofleva?jibu ni hakuna na sababu ni kwamba hatukinvesti kwenye 'wasomi' wa maswala ya burudani,na isitoshe hatukuinvesti kwa watu ambao wangeweza kutabiri kwamba miaka ya elfumbili kutaibuka mziki wa bongo fleva!

Kuna rafiki yangu aliwahi kuniambia wamarekani wengi ni mbumbumbu lakini wanabebwa na kikundi kidogo cha 'wasomi'
hata sisi hatujachelewa,inatakiwa tuanze sasa na baada ya miaka kadhaa tutaona matunda lakini tukidandia hii treni ya utandawazi kichwakichwa kwa kutumia mikakati ya western au china tutapoteza taifa.

Back to original topic,bado nasisitiza kwa kusema tugundue tatizo kwanza halafu tukabiliane nalo.kama tatizo ni structure ya elimu ya msingi basi hakuna kuchelewa tuibomoe.natumaini nimejaribu kujieleza vizuri
 
mkuu tunakupata sana.kwangu mimi quality ndio ina matter!!hiyo structure unayosema haikidhi imetumika kwa miaka kadhaa mpaka mwishoni mwa miaka ya tisini ambapo watu wakaanza kupoteza muelekeo.

Meningitis.. sasa hivi mtoto wa sekondari akiwa ameanza vizuri shule anamaliza sekondari akiwa na miaka 18 na akienda High School atamaliza akiwa na miaka 21/22. Huu ni muda mwingi sana kwa elimu ya chini. Binafsi ningependa kuona mwanafunzi anamaliza High School by 19. Lakini amalize akiwe competent and proficient enough.

Lakini la pili vile vile ni kuwa tunafundisha kwa kufuata mwaka mzima - mtaala unafuata mwaka huu unajifunza hiki na mwaka ule unajifunza vile. Binafsi naamini inabidi tuanze na kufundisha kwa modules ambapo mto ana move on to the next one baada ya kukamilisha module fulani (hii ni kwa elimu ya msingi. Anapofika Sekondari ndio anaanza kufuata ile semester system.

We have to change the structure of education system to create quality, accountability and global competitiveness.
 
Mzee MKJJ huu mdahalo ni mzuri, ungekuwa bora zaidi kama ungepanua wigo, wewe umeubana kwenye structure ya elimu ndio maana wengi wanaanzia kwenye ubora wa elimu ndio wanakuja kwenye structure. Huwezi kuzungumzia stucture ya elimu bila kuzungumzia ubora wa elimu lakini unaweza kuzungumzia ubora wa elimu bila kugusia structure. Mimi nafikiri, mdahalo ungezungumzia ubora wa elimu ya msingi kwa ujumla wake hili la structure ungeliweka kama moja ya factors zinazoweza kuathiri au kuchochea huo ubora.

Feedback ndio maanaya kuwa mdahalo manake kuwa unaweza ukakosoa hoja yenyewe na hata premise ya hoja; lengo tuweze kuchangia kutoka pande zote na kuexplore majibu yetu. Ukweli kwamba watoto wetu wengi wanafeli siyo suala la kudhania au kukisia. Binafsi naamini ni kwa kukosa msisitizo katika three Rs kwenye elimu ya msingi. Well hoja ni kuvunja elimu ya msingi ilivyo sasa na kuweka msisitizo katika mambo hayo. Watoto wetu hawajui kusoma, kuandika shida na kujieleza ni matatizo hata kwa baadhi ya wale waliofika chuo kikuu. Kuna wakati unasoma alichoandika mtu wa Chuo Kikuu unashangaa - lakini anajua anachotaka kusema lakini ndiyo hivyo.
 
Miaka ile 5 ya kwanza ya elimu ya msingi iwe ni kwa ajili ya:

Kusoma (Kiswahili na Kiingereza)
Kuandika na Uelewa (comprehension)
Kuhesabu (arithmetic)
Michezo na Sanaa

(Mwaka wa kwanza uwe katika kujifunza kusoma na kuandika - exclusively).

Middle School miaka 2 iwe kwa ajili ya:

Kuzama katika hesabu na lugha
Sayansi, Siasa (Civics) na Sanaa
Character development (kupitia michezo na extra curricular activities)

secondary (secondary education) miaka 2
Miaka 2 ya pure liberal arts (introductory courses)

High School - kuzama katika liberal education na semi specialization. (unafuta combination zilivyo sasa). Mwaka wa mwisho mtoto atakiwe kujua anataka kusomea nini Chuo Kikuu au onother tertiary institution.

Au mfumo gani mzuri zaidi wa kujaribu kudeal na hili tatizo la wanafunzi kufeli sana kuanzia shule ya msingi, sekondari na vyuo?

Cambridge system. It is tried and true.
 
MM, nimependa huu mdahalo, nafikiri tukitoa mawazo chanya tutatoka na kitu kizuri, swala la mtoto kupoteza miaka 17 ndio awe amemaliza chuo mimi linanikwaza kweli. Hebu tuangalie mfumo ambao mtoto atakapokua anatimiza umri wa mtu mzima (18yrs) awe ameshaandaliwa kujitegemea na haswa aweze kujiajiri, umri wa kuishi unazidi kupungua, inabidi turekebishe mfumo mzima na ninaamini hata quality ya elimu itabadilika kwani mtoto atapata kile atakachokitumia tuu. na hii itasaidia hata wazazi, wee jitu la miaka 25 bado linamtegemea mzazi, eti bado anasoma, anasoma nini kisichoisha.
 
Umefika wakati katika elimu ya Tanzania ziondolewe legacies za Nyerere. Elimu ya kujitegemea haina mpango.
 
Mwanakijiji,
Ningependa sana kuchangia mada hii kwa undani zaidi lakini nitaishia pale napopatazama mimi kwa udogo japokuwa muhimu sana kuona makosa yako wapi.
1. Lugha ya Kufundishia.
Hili ni tatizo kubwa sana ikiwa sisi hatutaki kuelewa kwamba watoto wanakwenda shule ili wapate kuelimika na sio kitu kingine. Huwezi kumfundisha mtoto kwa kiingereza, lugha ambayo haijui ili aonekane pendeza macho..Kuelimika hakuna lugha isipokuwa lugha ni kwa wawasiliano. Mtoto anayejua mbili jumlisha mbili ni Nne hana tofauti na yule anayejua Two plus two equals Four. Umliona wapi mtu anajifunza elimu kwa lugha ambayo anajifunza pia? hii naiona nchi maskini tu malimbuke na watumwa wa kukoloniwa. Infact Lugha ni kwa mawasiliano sasa inakuwaje mwalimu anawasiliana na mwanafunzi ktk lugha ambayo mwanafunzi haifahamu?.. hamuoni tatizo hapa!. Huu mwanzo tu ni mbaya.

Ni rahisi kumfundisha mtoto wa kiswahili (lugha anayoijua) kuhesabu Moja hadi 100 na akaelewa maana kuliko One to Hundred kwa sababu kiingereza ni lugha ya kigeni na hajui one inasimamia kitu gani hadi aijue lugha hiyo, hivyo ni muhimu sana shule za Primary schools hasa darasa la kwanza hadi nne wafundishwe kwa Kiswahili huku lsomo la lugha ya kiingereza likipewa mkazo (masomo mawili au matatu kwa siku) kama tunataka kuitumia mbeleni ili watoto wajue kuongea kiingereza. Japokuwa mimi sioni umuhimu wa Tanzania kutumia kiingereza kama lugha ya biashara pia - I dont..Hii pia ni kuonyesha utumwa kwa masters wetu..Ila watu kuzungumza kiingereza, Kifaransa, Kichina na hata Kirusi ni kachumbari ya mawasiliano.

Kuilalamikia serikali haitoshi ikiwa bajeti ya mwaka jana 2011 wametumia asilimia 20 ya bajeti na ndio kwanza wanafunzi wameshindwa vibaya sana. Na ukitazama kwa undani utagundua kwamba watoto wengi wameingia Form one wakiwa hawaja master lugha ya kiingereza - hawezi kuongea fluent wala kuandika sentesi ikaeleweka. Kisha wanaendelea kusoma kwa kiingereza tukidhani wanaelimika kumbe wanakariri majibu au sentesi utadhani mtu anayekariri Biblia au Kuran ili kuifadhi sura lakini haina maana anajua maana ya sura hizo (kuelimika).
Nina taarifa nzuri tu toka kwa mwalimu na watoto waliokaa mtihani wanadai kwamba kiingereza kilichotumika kutunga mitihani kilikuwa kigumu. Hii inasikitisha sana maana inaonyesha wazi watoto hawa hatukuwandaa kuelimika bali tuliwa test uwezo wao ktk lugha ya kiingereza..

Where did 20% ya bajeti imetumika ikiwa shule zenyewe zinajengwa kwa michango na Harambee na viongozi? Tumefungua vyuo vingapi nchini kufundisha walimu ama kuongeza vifaa vya kufundishia. Mishahara ya walimu bado midogo hizi fedha zinatumika vipi, kifupi mfumo mzima wa ELIMU nchini ni mbovu kupita kiasi na sintopenda kurudia yale yale kila siku lakini unapoona viongozi wako hawapeleki watoto wao ktk shule hizo ujue kuna tatizo, Unapoona viongozi wako hawatibiwi Hospital zetu ujue kuna tatizo.. Tuna create taifa la Classes na tumefikia mahala pabaya sana.
 
Mbona mitano ni mingi sana? kwa hapa Tanzania nna uhakika mwaka mmoja wa elimu ya msingi na mwaka mmoja wa elinu ya sekondari unatosha kabisa.

Nyerere alikuwa anafyatua ma dokta hata ukitoka form IV unakenda crush course ya udaktari na unapewa na title "dokta". Kina Salamba, kina Dokta Kesi, Kja dokta sigimbi, wote hao madokta wa nyerere. Imewezekana wakati dunia nzima wanasoma udaktari si chini ya miaka 5, kwetu miezi 6 iliwezekana.

Nashanga mwanakijiji anataka elimu ya msingi miaka 5. Mwaka tosha sana tena sana.
 
Elimu ya bongo haitaji tu marekebisho inahitaji matengengenezo mapya. Tazama elimu ya wenzetu wakenya kwa kuthibitisha hilo kumbuka mashindano ya vyuo afrika (zain africa challenge) utapata mwanga fulani. Jo vilevile tazama elimu ya mkoloni na elimu ya sasa. Kiswahili kitiliwe mkazo ili kuhidhi utamaduni wetu lakini kisitumike kufundishia kuanzia darasa la tano hapo tutumie lugha ya kiingengeza kwani ndo maarifa ya dunia yapo katika lugha ya kiingereza. Ni mengi tunayotakiwa kufanya ktk elimu yetu yangu ni hayo. Hata ujerumani wampango ya wajerumani wote kujua lugha hiyo.
 
Miaka ile 5 ya kwanza ya elimu ya msingi iwe ni kwa ajili ya:

Kusoma (Kiswahili na Kiingereza)
Kuandika na Uelewa (comprehension)
Kuhesabu (arithmetic)
Michezo na Sanaa

(Mwaka wa kwanza uwe katika kujifunza kusoma na kuandika - exclusively).

Middle School miaka 2 iwe kwa ajili ya:

Kuzama katika hesabu na lugha
Sayansi, Siasa (Civics) na Sanaa
Character development (kupitia michezo na extra curricular activities)

secondary (secondary education) miaka 2
Miaka 2 ya pure liberal arts (introductory courses)

High School - kuzama katika liberal education na semi specialization. (unafuta combination zilivyo sasa). Mwaka wa mwisho mtoto atakiwe kujua anataka kusomea nini Chuo Kikuu au onother tertiary institution.

Au mfumo gani mzuri zaidi wa kujaribu kudeal na hili tatizo la wanafunzi kufeli sana kuanzia shule ya msingi, sekondari na vyuo?

Mfumo wa sasa. Aliujenga Nyerere. Katika moja ya essays au hotuba zake alitaka elimu iwe na watu wengi waliomaliza elimu ya msingi. Wengi kidogo waliobaliza elimu ya sekondari na vyuo vya kati. Na wachache waliomaliza elimu ya juu.

Waliomaliza elimu ya msingi walitakiwa kuwa kama wapiganaji. Waliomaliza elimu ya kati kama makamanda. Na waliomaliza elimu ya juu kama majemedari(generals).

Kwa mahitaji ya kidunia ya sasa. Mpango huu hauna maana na nakubaliana na hoja yako hapo juu kwa sababu zifuatazo.

Mpango wako unalenga elimu inayoambatana na umri wa watoto. Watoto wa madarasa a mwanzo, wanatakiwa kujifunza skills za kujifunza, kusoma, kuandika na kuhesabu. Na mtoto anayokuwa ndivyo masomo mengine yanaongezeka.

Vilevile kabla ya kwenda vyuoni umeweka liberal arts. Hii inawapa vijana kuwa creative na vilevile kuwa na options nyingi katika maisha yao. Kwa Tanzania kuna shule za mchepuo. Kwa mfano mwanafunzi anasoma bookkeeping akiwa sekondari. Huku ni kuwapotezea muda tu watoto. Kwani mtu ambaye ni comprehensive, anajifunza bookkeeping katika wiki tatu tu.

Watu wanakwenda shule za ufundi kusomea electronics wakati siku hizi kitu kikiharibika unabadilisha tu.

Vilevile mpango wako unaweza kufanya elimu iwe local. Hakuna sababu ya mwanafunzi kusafiri na kutumia gharama nyingi hili ajiunge na shule za kilimo. Kama kuna liberal arts, wanafunzi wanakuwa wanakwenda kwenye local schools na kukaa majumbani mwao.
 
Back
Top Bottom