Mchungaji Gwajima ni Mtumishi wa Mungu wa kweli au? Asema Uongo. Adai yeye ni zaidi ya Rais

Tangu nianze kumuona mhubiri huyu katika media amekuwa more in politics ndiyo maana hata katika uchaguzi mkuu 2015 alizunguka nchi nzima akimnadi Fisadi Papa ili awe rais wetu.

Swali langu ni kwamba, sheria inasemaje kwa mhubiri anayechanganya dini na siasa?

Kwa nini serikali inakuwa na kigugumizi kumkanya ama kumchukulia hatua?

Au hayo anayoyafanya yana mkono wa serikali ndani yake?

Aulizaye anataka kufahamu
Kwanza tudhibitishie alizunguka mkoa upi na upi kumnadi huyo unayemuita fisadi ambaye mnaogopa ata kivuli chake achia mbali kumfunga.
Tangu nianze kumuona mhubiri huyu katika media amekuwa more in politics ndiyo maana hata katika uchaguzi mkuu 2015 alizunguka nchi nzima akimnadi Fisadi Papa ili awe rais wetu.

Swali langu ni kwamba, sheria inasemaje kwa mhubiri anayechanganya dini na siasa?

Kwa nini serikali inakuwa na kigugumizi kumkanya ama kumchukulia hatua?

Au hayo anayoyafanya yana mkono wa serikali ndani yake?

Aulizaye anataka kufahamu
 
Hajasema ana matokeo, amesema ana vyeti mezani kwake, hivi kweli kuna cheti cha divisheni 0 ya miaka hiyo?.

Paskali
pascal mayala unaboa sana. halafu acha kuchafua wenzako, nahisi kuchafuliwa kunauma sana, na wewe unaweza kuwa unajua iyo experience kama alivyosema jamaa hapo nyuma kwamba wewe pia ulihangaika kweli kujisafisha hapa baada ya kusemekana una practice ukameron. kama ni kweli sawa, lakini kama sio kweli nahisi itakuwa ilikuuma sana, na ikizingatia mkeo ameachana na wewe watu ndio watapigia mstari kabisa kwamba mama alikimbia mdada mwenzie. the same way uache kuhangaika kwenye mitandao kuchafua na kutoa conclusion kwenye maisha ya wenzio, tafuta maisha yako ili uheshimike. la sivyo hata wewe kuna mengi yapo gizani yakiwekwa nuruni utatamani ardhi hii ipasuke uingie.
 
Naheshimu sana michango yako senior Pascal Mayalla,lakini kwa baadhi ya maeneo nikitafakari kwa utulivu napata shida sana kukuelewa,UNAPOSEMA GWAJIMA AMESEMA UWONGO,unamaanisha nini,na huo uongo ni upi,na kama alichosema Gwajima ni uongo,ukweli ni upi basi,ni vema ukathibitisha uwongo wa Gwajima kwa kuweka ukweli halisi bayana.

Pascal,wewe ni mwanasheria,unadhani unachosema ni sawa katika misingi ya kisheria?
GWAJIMA atabaki kuwa mkweli kwa swala zima la vyeti vya MAKONDA,mpaka MAKONDA aje na vyeti vyake Hadharani,kuthibitisha Uwongo wa GWAJIMA.

Ni ukweli usiopingika kwamba hata wenye vyeti vyenye UTATA katika zoezi zima la uhakiki kwa watumishi wa umma,ili kumaliza utata wao WAMEAMBIWA WAENDE BARAZA LA MITIHANI NA VYETI VYAO HALISI.wala hakuna sababu ya kukesha kumtetea BASHITE,GWAJIMA WAS AND STILL IS,RIGHT UNTILL MAKONDA PROVE IT OTHERWISE!!
 
Naheshimu sana michango yako senior Pascal Mayalla,lakini kwa baadhi ya maeneo nikitafakari kwa utulivu napata shida sana kukuelewa,UNAPOSEMA GWAJIMA AMESEMA UWONGO,unamaanisha nini,na huo uongo ni upi,na kama alichosema Gwajima ni uongo,ukweli ni upi basi,ni vema ukathibitisha uwongo wa Gwajima kwa kuweka ukweli halisi bayana.

Pascal,wewe ni mwanasheria,unadhani unachosema ni sawa katika misingi ya kisheria?
GWAJIMA atabaki kuwa mkweli kwa swala zima la vyeti vya MAKONDA,mpaka MAKONDA aje na vyeti vyake Hadharani,kuthibitisha Uwongo wa GWAJIMA.

Ni ukweli usiopingika kwamba hata wenye vyeti vyenye UTATA katika zoezi zima la uhakiki kwa watumishi wa umma,ili kumaliza utata wao WAMEAMBIWA WAENDE BARAZA LA MITIHANI NA VYETI VYAO HALISI.wala hakuna sababu ya kukesha kumtetea BASHITE,GWAJIMA WAS AND STILL IS,RIGHT UNTILL MAKONDA PROVE IT OTHERWISE!!
Nahisi kama vile unapoteza muda na nguvu nyingi kujaribu kumuelimisha mtu ambaye kajitoa ufahamu kwa makusudi vile....!!
 
Nadhani sasa ni wakati muafaka kabisa kwa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania afikirie kumpa ama usajili wa muda wa kudumu kabisa Askofu Josephat Gwajima ili tujue moja huu ' upuuzi ' wake tunaoanza kuuchoka sasa.

Najua humu JF kuna Watu wake wengi mnaomuamini na niliweke tu wazi kuwa hata Mimi kuna mahala fulani huwa nakubali michango yake hasa ile yenye uelekeo wa kuijenga Jamii yetu ambayo kimsingi hata yeye anaitegemea kwa ' Sadaka ' zao.

Katika huu ' uzi ' wangu nawaombeni tumwangalie Askofu Gwajima katika dhana nzima ya ' Society Development ' ili tuweze kujua kuwa tunapomkabili hivi Kihoja tunakosea au tupo sahihi na tukisema tukae kimya eti kwa Kigezo cha ni ' Kipenzi ' chetu au chako nadhani tutakuwa hatumsaidii.

Natambua matatizo makubwa yaliyopo sasa nchini Tanzania na pia naitambua kabisa Kazi yake kama Kiongozi wa Kiroho ambaye ana haki ya Kukemea na Kulisemea pale inapobidi ina nadhani sasa Askofu Gwajima ame exaggerate hii kitu na nimeanza sasa kuhisi kuwa pengine kuna ' kamchezo ' fulani ambako anakafanya kupitia Watu maarufu wengine ili kumpaisha na kusudi kila Jumapili Kanisani Kwake kufurike ili azidi kula Pesa za ' wasiojielewa ' wala ' kumshtukia '.

Hivi logically tu Askofu unaweza ukaanza kuhubiri kuanzia Saa 4 hadi Saa 8 na katika hayo mahubiri yako neno la Kimungua au la Kiroho tunalisikia kwa 5% tu lakini maneno ya Kimajungu, Majigambo na Vitisho tunayasikia kwa 95%.

Mimi sijasomea mambo ya ' Theology ' ila nina uhakika kabisa humu humu JF wapo ' wanazuoni ' wazuri wa hiyo Elimu ya Kidini hivyo wajitokeze kutusaidia kuwa je huu ' utoto ' wa Kiimani anaoufanya Askofu Gwajima kila Jumapili ndivyo walivyofundishwa huko Vyuoni Kwao?

Sasa kituko zaidi ni pale jana ambapo Askofu Gwajima kasema kuwa Msanii wa Miziki ya Bongo Fleva Nassib Abdul a.k.a Diamond au Dangote kuwa ni mmoja wa Wafuasi wa lile Kundi linalohisiwa kuwa ni la Kichawi la Freemason na kwamba ana uhakika wote juu ya hilo.

Nadhani Watanzania ama tumejisahau au tumejisahaulisha tu kwa makusudi kuwa huko nyuma kwa miaka kadhaa huyu huyu Askofu Gwajima amekuwa akihusishwa na hilo hilo Kundi la Freemason sasa labda pengine ili tumuamini atuambie je yeye ndiyo alimkaribisha Diamond huko au alipishana nae labda yeye alipoondoka humo?

Sipo hapa wala humu JF kumtetea sijui Diamond au kumachafua Askofu Gwajima ILA vita ambayo siku zote GENTAMYCINE huwa napigana nayo ni ya kutopenda ' Unafiki ' na kuwa ' Mwoga ' kusema ukweli wako na laiti Watanzania wote tungeuchukia huu ugonjwa wa unafiki nina hakika leo nchi yetu ingekuwa mbali mno Kimaendeleo.

Askofu Gwajima nitoe tu RAI Kwako kuwa Wewe ni mmoja kati ya Viongozi wa Dini wenye kuheshimika na jamii kubwa ya Tanzania ( japo nahisi ni ya sisi tu wana Dar es Salaam ) hivyo jaribu sana kutenganisha kati ya Utumishi wa Kiroho na Harakati za Kisiasa kwani nisikufiche siku hizi ' Bifu ' zako zikija kupatiwa ' Ufumbuzi ' wa muda mrefu nadhani hapo Kanisani Kwako utabaki Wewe, Mkeo na hao Walinzi wako na wenye akili wote ' watakukimbia '.

Askofu Gwajima mbona hizi ' harakati ' zako hatuzioni kwa wenzako kama akina Mwingira, Lusekelo, Mwakasege, Kakobe na wengineo ambao nina uhakika kuwa wao wameanza hili ' game ' kabla yako? Kwanini Wewe? Je huyo Mungu wako Wewe kakutuma uwe unaitumia tu Jumapili kwa ' kuwananga ' Watu?

Nimalizie tu kwa kukukumbusha Mkuu japo Wewe unaonekana kuwa ' kimbelembele ' Waganda wanasema ' Lugezigezi ' kwa kutoa ' SIRI ' za ndani kabisa za Wenzako ILA je Askofu Gwajima na Wewe unalikumbuka lile tukio lako la miaka minne ( 4 ) iliyopita ambalo ulilifanya katika Nyumba ya Mtu pande za Mbezi Beach maeneo ya kwa Marehemu Mzee Sykes ambapo ' lilikugharimu ' hadi ikakubidi uruke ' ukuta ' wa ile nyumba baada ya kushtushwa na waliokuonea huruma kisha baada ya hapo ukatumia gharama nyingi mno kulimaliza kupitia kwa ' Msukuma ' mwenzio Erick Shigongo na ' Magazeti ' yake?

Kwa leo naomba niishie tu hapa ila ukiona hayo niliyoyaandika hapa yana tija yachukue na ukiona hayana niachie tu mwenyewe tafadhali ila naamini wenye akili za kutukuka na wanaojitambua watakuwa wamenielewa. Tanzania ya sasa hatuhitaji majungu, fitina, bifu na chuki bali tunahitaji msaada wa kutoka hapa tulipo Kimaendeleo ili tuweze kukimbizana na waliotupita siki nyingi.

Nawasilisha na niwatakieni tu mwanzo mwema wa wiki hii na Pasaka njema nyote.
Mkuu Genta, kwanza pole kwa uzi wako huu kuunganishwa kwangu!, nimelisoma bandiko lako na maudhui yake, ni tofauti kabisa na uzi wangu.

Mode: Uzi wangu ulizungumzia unabii wa mchungaji Gwajima kama ni nabii wa kweli au wa uongo, uzi huu unamzungumzia Mchungaji Gwajima kuchanganya dini na siasa. ni vitu viwili tofauti.

Paskali
 
Tangu nianze kumuona mhubiri huyu katika media amekuwa more in politics ndiyo maana hata katika uchaguzi mkuu 2015 alizunguka nchi nzima akimnadi Fisadi Papa ili awe rais wetu.

Swali langu ni kwamba, sheria inasemaje kwa mhubiri anayechanganya dini na siasa?

Kwa nini serikali inakuwa na kigugumizi kumkanya ama kumchukulia hatua?

Au hayo anayoyafanya yana mkono wa serikali ndani yake?

Aulizaye anataka kufahamu
You're wrong these two are inseparable. Unamjua mtu anayeitwa Musa? Huyo alikuwa mtumishi wa Mungu na alifanya siasa alipokwenda kuwakomboa wana wa Israeli kutoka utumwani misri. Lakini pia huyo mnaye mwita fisadi papa mbona hamumpeleki kwenye mahakama ya mafisadi ambayo tunaambiwa imekosa wateja? Au huo ujenzi wa hiyo mahakama
 
Kwa sa
Sasa mbona Lowassa na Maalim Seif wanaulilia sana urais? Kwa nini wasiwe wachungaji?
Mkuu kwa sababu uchungaji ni kazi ya kiroho zaidi kuliko uraisi. Ni wale walio rohoni tu ndiyo watakuwa wachungaji. Kiroho Gwajima is right, uchungaji ni zaidi ya uraisi. Ukiwa mchungaji mwema faida yake ni eternal wakati uraisi hata ukichakachua ni miaka kumi tu. halafu unakaa nasi benchi.
 
Hajasema ana matokeo, amesema ana vyeti mezani kwake, hivi kweli kuna cheti cha divisheni 0 ya miaka hiyo?.

Paskali
Mayala naona nawe sasa umeazimwa kama ilivyo kwa akina Lemutuz! Mayala elewa kuwa mtu anapotaka kukutumia ili kumsafisha au kumsemea anakuwa tyr amejua akili yako ni nyepesi sana! Kuwa makini mkuu utapoteza credibility yako mkuu.
Ila kuhusu Gwajima ni 'mpiga deal' kama walivyo wengine wanaotumia jina la Yesu na nchini wako wengi tu.
 
Bottomline ni kuwa wanadamu wote ni unpredictable na waongo. Huyu anayesema yeye ni rais wa wanyonge ni kweli? msemakweli ni mpenzi wa Mungu, ni kweli anasema kweli? etc, etc, etc,
Hivyo ya Gwajima ni kama ya wengine, hata wewe Paskali! Kuna wanaokuona hivyo kumpenda Katili! Hata mimi kuna wanaoniona katili, mwongo etc! La muhimu tusiende kwenye extremes kuwapoteza wenzetu! Tumpinge Gwajima, tusimuue, tusimtoe roho!
 
Tangu nianze kumuona mhubiri huyu katika media amekuwa more in politics ndiyo maana hata katika uchaguzi mkuu 2015 alizunguka nchi nzima akimnadi Fisadi Papa ili awe rais wetu.

Swali langu ni kwamba, sheria inasemaje kwa mhubiri anayechanganya dini na siasa?

Kwa nini serikali inakuwa na kigugumizi kumkanya ama kumchukulia hatua?

Au hayo anayoyafanya yana mkono wa serikali ndani yake?

Aulizaye anataka kufahamu
Kweli alizunguka nchi nzima?
 
Mayala naona nawe sasa umeazimwa kama ilivyo kwa akina Lemutuz! Mayala elewa kuwa mtu anapotaka kukutumia ili kumsafisha au kumsemea anakuwa tyr amejua akili yako ni nyepesi sana! Kuwa makini mkuu utapoteza credibility yako mkuu.
Ila kuhusu Gwajima ni 'mpiga deal' kama walivyo wengine wanaotumia jina la Yesu na nchini wako wengi tu.
Mayalla uhome boy umemmaliza, hatuna mwandishi tena
 
Pascal Mayalla,
Kuna aina mbili za injili
1.Kuna injili ya kikoloni
2.Na kunainjili ya kweli

Injili ya kikoloni imemeza wengi ndio maana watu hawataki.

Uwe unatoa maelezo vizuri hasa na ushaidi mzuri, siku io alio ongea hayo nilikwenda kwakua kulikua kuna habari ya makonda.

Alisema hivi "hawezi gombea ubunge ama uraisi kwakue yeye alie mpa kazi hiyo ni Mungu mwenyewe rais kaajiliwa na wananchi na swaiba wake kaajiliwa na raisi hivyo yeye ni zaidi kwakua amepewa kazi hiyo na Mungu "
 
Sasa mbona Lowassa na Maalim Seif wanaulilia sana urais? Kwa nini wasiwe wachungaji?
Kila mtu ana wito wa aina yake, huwezi wapangia watu wafanye kazi ambayo si wito wao. Wewe huwezi panga hatma ya wanadamu wenzako maana wewe si Mungu. Wao wito wao ni uanasiasa na Gwajima wito wake ni uchungaji. Kaa uelewe kwaamba haitakaa ije kutokea binadamu wote wakawa na wito wa aina moja. Ikiwa hivyo basi hata dunia itapoteza ladha yake.
 
Ni rahisi sana muumini wa kawaida kuingia mbinguni kuliko mchungaji kuingia mbinguni. Trust me
Haya ni maoni yako binafsi. Kwa Mungu hakuna lisilowezekana. Kama jinsi ilivyo kwa waumini kwamba kuna watakaoingia na watakaoshindwa, kadhalika ndivyo ilivyo na kwa wachungaji. Mungu ni Mungu wa haki na ndani yake hakuna udhalimu wowote.
 
Back
Top Bottom