Niliwaona na kuwasikiliza wazazi wake wakihojiwa na "mawingu TV",hivi wanajisikiaje kushiriki udanganyifu wa kiwango hiki?Kwa nini wasijitokeze na kuusema Ukweli juu ya majina yao halisi na ya mtoto wao?
Kughushi vyeti kunaweza kuwa mwanzo wa mwisho wa kijana mlopokaji,mjivuni na mlaghai anayemtumia Mungu katika kuhalalisha hadaa zake.Tunaoamini katika Kristo Yesu tunapomkiri Yesu huwa tunaongozwa sala ya toba ambayo miongoni mwa maneno yatumikayo katika toba hiyo ni kumuomba Mungu ayafute majina yetu kwenye kitabu cha hukumu na kuyaandika majina yetu kwenye kitabu cha uzima,sijuwi muheshimiwa mungu wa Dar anatumia majina gani kwenye vitabu hivyo.
Baba yake alisema kupitia mawingu Tv.kuwa yeye ni kiongozi wa kanisa,mwanaye anapohusishwa na udanganyifu wa kiwango cha lami huku yeye akikaa kimya huku akitumbua mapato ya udanganyifu wa mwanaye anajisikiaje?Hii ni fedheha sana.