Mchungaji Gwajima sikiliza neno la Bwana, ili ujitafakuri imani na kazi yako ya Utumishi wa Mungu.
Mt 5:39 - "haupaswi kulipa baya kwa baya! Badala ya kulipa baya kwa ndugu yako, unapaswa uwe tayari kuteseka au kudhulumiwa".
Njia pekee ya kuvunja ubaya na mzunguko wake ni KUSAMEHE. Kama mtu akilipiza ubaya kwa ubaya zaidi, ubaya hauondoi ule ubaya wa mwanzo bali unaongeza ubaya zaidi. Mzunguko huu wa ubaya, unaweza tu kuondolewa kwa msamaha wa kweli, kutoka ndani mwako.
Mfano, Simoni wa Kirene alilazimishwa kubeba msalaba wa Yesu (Mt 27:31). Huyu ambae alikuwa Zelote, wana mapinduzi wa wakati huo waliwashawishi kugoma na kulipiza kisasi, kupinga kitendo kama hicho. Yesu anawaambia wafuasi wake "sio sheria ya hekima" tabia hiyo haiwezi kuleta matunda mazuri. Anawaambia wafuasi hata bila ya kukunja moyo wafanye kwa uhuru kabisa, bila kupinga, kujiepusha na kitendo chochote ambacho sio cha upendo.
Mchungaji Gwajima, hubiri upendo, ambao msingi wake ni KUSAMEHE. Kama tungehesabu makosa yetu, nani angesimama!
Mh RC Makonda, wewe ni mtumishi wa Kaisari, yaliyosemwa na Mtumishi wa Mungu yanakuhusu wewe kama wewe, msamehe kwa kuepusha kutumia rungu lako la Kikaisari.
MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE