Mchungaji Anthony Lusokelo apinga ndoa za mke mmoja

Mchungaji Anthony Lusokelo apinga ndoa za mke mmoja

Hizo aya zote ulizoweka hazijabatilisha ndoa ya wake wengi.

Daudi alikuwa na wake wangapi?

Napenda uelewe kuwa ndoa za wake wengi ni "solution" ya tatizo kubwa sana lililopo duniani sasa hivi, sikiliza:


Kuwa na mke zaidi ya mmoja ni uzinzi kama ulivyo uzinzi. Watu wengi wa kipindi cha Agano la Kale kina Daudi, Suleimani, n.k walioa wake wengi hatukatai lakini hakuna sehemu yeyote inayoonesha kuwa Mungu aliwaruhusu kufanya hivyo. Hizo ni nyakati ambazo Mungu alijifanya haoni, na aliziita nyakati hizo kuwa ni nyakati za ujinga. (Mdo 17:30) -"Basi zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kuwa hazioni; bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu." Saivi hatuishi kipindi cha ujinga. Tuko kipindi cha Agano Jipya yaani DAMU YA YESU.
 
Ulicho sema lusekelo ni kweli kabisa, ukisoma bibilia manabii na mitume karibia wote walikuwa na wake zaidi ya mmoja! Wakristo tukubali figisu nyingi tuu zilipenyezwa kwenye imani yetu
 
biblia inasema ukimuacha mke na kuoa unafanya uzinzi. sasa kuoa akate anaye si ndiyo balaa zaidi.
 
Ameongea kuwa kuna mtu mmoja ndiye aliyeweka amri ya mke mmoja sijaona kwny amri za Mungu amri ya namna hii kuna haja ya kufanya utafiti juu ya hili vitabu vinaelezea watu kuwa na wake hadi mia 3 na vimada ....
 
Hiyo hapo.
Mchungaji kasema hayo kwenye ibada ya leo. Huyo ndo mzee wa upako.
View attachment 433450
Sina maslahi na huyu mchungaji ila na wewe mleta mada usiwe unakurupuka. Ulimsikiliza hadi mwisho? Kuna maelezo aliyatoa ambayo yana logic sana na ambayo yanaharamisha ndoa za wake wengi. Tafuta hiyo clip na uje utuwejee tena hapa usikie alichokisema akihitimisha hiyo mada
 
kwani sehemu gani ya Bible imekataza kuoa wake wengi? kama kila neno la Mungu Lafaa kwa mafundisho kwa nini tusijifunze kwa suleiman au Daudi? kwa nini tujifunze kwa Paulo tu? mbona Bible inasema mwanamke asipewe nafasi ya kuongea lakini tumepuuza?
 
Yeye si mchungaji? Basi akasome biblia vizuri atajua nani aliyeweka hivyo.
 
Ni vizuri. Sioni maana ya kupinga na ndoa za wake wakati huohuo watu wanasapoti ushoga tena makanisani, kama hatuwezi kuona ushoga ni dhambi ni kwanini kuoa wake wengi iwe dhambi?

Na kuacha kuoa wake wengi badala yake mnaanza kuwanyemelea kwa siri maanake nini, ni kwanini Mungu aliumba wana ke wengi kuliko wana me? Mungu alikuwa mjinga? na mnapooa mmoja mmoja mnataka hawa wanaobaki bila kuolewa waende wapi kumaliza haja zao? si ndo hao hao wanaokuja kuanza kujiuza na kuvuruga ndoa za wenzao, kwa hili mnamlaumu nani?

Hawa wanawake wote Mungu kawaumba, wangependa kila mmoja aolewe bila vikwazo. Iweje leo mnawaambia eti aolewe mmoja mmoja ama kisa wanaume mko wengi na ndo mnafanya maamuzi? Waacheni wanawake na wanaume waoane ilimradi wameelewana kuhusu masrahi ya ndoa yao, na Mungu alivyosema mkaijaze dunia alijua dunia haiwezi kujaa kwa mke na mme mmoja, so let's do our best on that.
 
Tatizo wakristo tunaendeshwa na sheria za madhehebu sio sharia za Mungu kiukweli Mungu hajawahi kukataza kitu ki mficho .Je kwenye bibilia kuna katazo hili
Hivi mtumishi wa Mungu Sulemani alioa wanawake wangapi vipi Mungu aliwahi kumuonya
Tuwe wakweli mungu anatuona wakristo tuishi na neno la Mungu sio maneno ya makasisi
 
Mbona yeye ana Mke mmoja tu?

Imagine huyo mke wake anajisikiaje...
Nisaidieni wadau nimejitahidi kumfuatilia sana jamaa lakini sijabahatika kumjua mkewe. Hata kwenye mahubiri yake sijawahi kusikia akizungumzia kuhusu mkewe. Kuna kipindi mwaka 2013 alikuwa anahojiwa kwenye kipindi cha mikasi katika kueleza habari za familia yake alijikanyaga kutaja majina ya watoto wake wanne. Kweli mtu unaweza kuchanganya majina ya wanao tena wanne tu???
 
Yuko sawa hao wa mke mmoja wengi wao wanachepuka full tamaa
 
Back
Top Bottom