GE2025 Mchinjita: Raia kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali iseme ni Wasiojulikana, hiyo ni Serikali au Takataka?

GE2025 Mchinjita: Raia kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali iseme ni Wasiojulikana, hiyo ni Serikali au Takataka?

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,499
Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Bara, Isihaka Mchinjita amesema, "Unapofika mahala una Serikali ambayo raia wake wanaweza kwenda kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali inasema walioua ni watu wasiojulikana — hiyo ni Serikali au takataka?"

"Haijawahi kutokea duniani kote, kukawa na takataka iliyopata hadhi kuitwa Serikali kisha takataka hiyo ikatengeneza sheria safi za kuleta Serikali isiyotakataka."

 
Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Bara, Isihaka Mchinjita amesema, "Unapofika mahala una Serikali ambayo raia wake wanaweza kwenda kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali inasema walioua ni watu wasiojulikana — hiyo ni Serikali au takataka?"

"Haijawahi kutokea duniani kote, kukawa na takataka iliyopata hadhi kuitwa Serikali kisha takataka hiyo ikatengeneza sheria safi za kuleta Serikali isiyotakataka."

Ukweli mtupu, takataka
 
"Haijawahi kutokea duniani kote, kukawa na takataka iliyopata hadhi kuitwa Serikali kisha takataka hiyo ikatengeneza sheria safi za kuleta Serikali isiyotakataka."
Bado watu wa Mama Samia hawajamuita kumuhoji? kisha tusubiri upelelezi ukamilike miezi 17.

Hizi Lugha wanatumia hadharani, ni dalili ya watu KUCHOKA na kuwa tayari kwa Lolote.

Samia amekuwa predictable sana, watu sasa wameshajua kuwa nikifanya hivi nitakamatwa, na wapo TAYARI.

Hii ni ishara ya Hatari kubwa sana hapo mbeleni endapo hali ikiendelea hivi.

Ewe sikio la kufa, tafadhali zibuka na usikie hii dawa.
 
Bado watu wa Mama Samia hawajamuita kumuhoji, kisha tusubiri upelelezi ukamilike.

Hizi Lugha wanatumia hadharani, ni dalili ya watu KUCHOKA na kuwa tayari kwa Lolote.

Samia amekuwa predictable sana, watu sasa wameshajua kuwa nikifanya hivi nitakamatwa, na wapo TAYARI.

Hii ni ishara ya Hatari kubwa sana hapo mbeleni endapo hali ikiendelea hivi.

Ewe sikio la kufa, tafadhali zibuka na usikie hii dawa.
Hapana sio kua wamechoka watu kama huu bali ni kutafuta kiki za kisiasa na kujikatia tamaa
 
Bado watu wa Mama Samia hawajamuita kumuhoji? kisha tusubiri upelelezi ukamilike miezi 17.

Hizi Lugha wanatumia hadharani, ni dalili ya watu KUCHOKA na kuwa tayari kwa Lolote.

Samia amekuwa predictable sana, watu sasa wameshajua kuwa nikifanya hivi nitakamatwa, na wapo TAYARI.

Hii ni ishara ya Hatari kubwa sana hapo mbeleni endapo hali ikiendelea hivi.

Ewe sikio la kufa, tafadhali zibuka na usikie hii dawa.

..watawala walitakiwa wajiulize kwanini vyama vya upinzani vinatumia lugha ngumu.

..kwa maoni yangu hizo lugha zinaelezea mateso na dhuluma wanayopitia wapinzani.

..Mjumbe[ally kibao] wa Kamati Kuu ya chama kuuwawa na maiti yake kutobolewa macho haliwezi kuwa jambo dogo kwa chama cha siasa.

..dhuluma hiyo, au zozote zinazofanana na hiyo, haiwezi kuzungumziwa kwa lugha lainilaini, au za bashasha.

..Watawala wajifunze, na wajisahihishe, badala ya kuwapingia waliodhulumiwa namna ya kulia na kulalamika.
 
Back
Top Bottom