Mchina aliyepata "A" tisa NECTA

Nawaza tuu, mchina anapata B ya kiswahili anasikitika lakini sisi PhD holder anashindwa kuzungumza kiingereza fasaha alichokitumia kusomea kwa miaka kadhaa mpaka kuhitimu na tunaona kawaida tuu
Hili Dongo limetupwa gizani...
 
Toa jina kamili,mwaka uliohitimu masomo mf form 4,6 or chuo then tukwambie ni nama gan kwako pia hyo bell curve ilikuwa...kumbuka kuna weng wana ndgu,watoto na hata wazaz wamefanya hyo paper so umetukana raia kwa kias flan.....toa ahzo details tuone km kwako bell curve was escaped😀
 
sasa jaman kilasiku mlikuwa mnatusakama wasukuma mmeona sasa TO ni msukuma anaitwa BUTOGWA CHARLES SHIJA wachaga mpooooo
 

Attachments

  • 1455871888682.jpg
    73.8 KB · Views: 50


Ni wapi nilipomtukana mtu?
 
Acheni ubaguz yule ni mtanzania mwenye asil ya china.......mbna obama hamumuit mwafrika
 
Kwa kiasi fulani naungana nawe mtoa hoja hasa kwenye suala la hizo tafiti na mengineyo mengi ila nina mambo mawili nataka kuyaweka sawa:

a) kuna uhuru wa kuwa na mawazo tofauti na hii ni haki kwa kila binadamu ilimradi havunji sheria. hata hayo mataifa makubwa viongozi na raia wake hawakubaliani kwa kila jambo, tofauti ya mawazo na fikra ndio vinatufanya tuwe na maendeleo. Kwa mfano si wamarekani wote waliofurahishwa na uamuzi wa serekali yao kupeleka majeshi vitani Iraq au Afghanistan.

b) Ufaulu wa somo la kiswahili hauwezi kuwa kipimo cha IQ ya mtu haza ukiiegemeza hoja yako kuwa kwa mchina ni lugha ya kigeni. Kiswahili kinachofundishwa shuleni na kutahini wanafunzi si sawa na kiswahili tuzungumzacho. Mtihani unatungwa kwa kuzingatia mitaala husika ambayo inalenga kumfanya mwanafunzi kuwa mahiri wa lugha hiyo hivyo nategemea hata mtanzania akienda kusoma Ulaya Kufaulu somo la Kiingereza kwa alama A au B si kitu cha kustaajabisha.

Mwisho natambua matokeo mazuri ya huyu mtanzania mwenzetu wa asili ya uchina na nampongeza kwa dhati ya moyo wangu ila masuala ya taaluma si mambo ya ushabiki, tuwapongeze basi na hawa vijana wetu waliofanya vizuri zaidi. Kipimo sahihi cha uwezo wetu kitakuwa sawa pale ambapo wanafunzi wote wa tanzania watasoma na kufundishwa katika mazingira yaliyo na uwiano sawa kitaaluma.
 
Wengine hawapendi kutangaza mambo yao yanaishia huko walipo. Lakini wapo naweza thibitisha.


Hili siyo swala la kujitangaza kwani huyu Mchina kajitangaza? Hili likitokea hutangazwa tu ndugu, hivyo kama yupo na unamjua ina maana alishatangazwa huko aliko hivyo unaweza tu kumtaja hapa!
 
Sijaelewa hapo kiini cha thread yako ni ipi! Ni IQ au Sukari au Mchina kuongoza kiswahili!? Au ni tangazo la Magufuli kustopisha sukari kutoka nje!?
Una IQ ndogo ndio maana hujaelewa..... Teh, teh, teh,
 
kaongoza msukumaa bwanaa BUTOGWA CHARLES SHIJA unaweza ukawa na A nyingi zikawa ni za 82 afu mwenzako akawa na A chache za 98 akakukalisha ..katika u T.O vigezo huwa ni wastani na si wingi wa A
 
Mkuu Barbarosa,kumpinga mtu au kupinga kitu au kuwa na mawazo tofauti kumbe ni IQ ndogo?
Pole sana kijana,siasa inakuharibu kijana.
 
Hii kali lakini yote ni mihemko tu ya kisiasa-kuna siku utapigwa picha unafuta viatu vya wakubwa kama DC wa kinondoni shauri yako,mada yako uliyoileta umeonyesha ni jinsi gani huna uwezo wa kufikiri na kuchambua mambo,IQ na sukari!!!!!!!puu!
 
Kwenye semina ya THE AKILI KUBWA atakwepo..Nenda kachukue namba

Hahaha mkuu nimemwambia le akili kubwa akupe mualiko wangu

So ukifika cha kwanza namba za CongCong Wang
 


Ndugu angalia kwanza CV ya huyo mtoto amekuja TZ akiwa na miaka 9 hajui Kiingereza wala Kiswahili, kumbuka hao watoto wa academy wanasoma Kiingeraza tangu cheke chea hivyo ina maana huyu binti ametumia miaka michache tu kuziba hilo pengo na bado ameongoza TZ nzima!

Kama niliyosema sijahitimisha chochote ila nimeuliza maswali kwa maana hili swala linajadiliwa Dunia nzima kwamba watu wa Waasia yaani Wachina, Wajapani, Wakorea, wana IQ kubwa klk binadamu wote hapa Duniani hata Marekani takwimu zinaonyesha kwamba Wamarekani wenye asili ya Asia (Ujapani, Uchina na Korea) ndiyo wanaongoza kwa ufaulu wakifwatiwa na Wazungu na sisi ni wa mwisho, asilimia 60 (60%) ya Wanafunzi walioko graduate schools Marekani kwenye Ivy league kama Princeton, Harvard, Yale, & Co. Uni ni asili ya Asia, wamewashinda Wazungu ambao ndiyo wengi kwa kiasi kikubwa tu!
 
jaman majina kumbe kweli yanamata,namkumbuka mwalimu wangu mkuu bwana Alfred Marya aliwahi kusema wale wenye majina kama Tabu,Chozi,shida,mkiwa,msiba na mengine ya dizaini hiyo wabadili majina yao mana ni sababu ya kupata misukosuko maishani.
 
Kwa hiyo kuwa jumbe ndio ndio kuwa na IQ kubwa?mbona kama umeongea kinyume?kutohoji ndio IQ ndogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…