Mchina aliyepata "A" tisa NECTA

Sizitaki mbichi hizi! Wivu tu, tambua hizi shule zinafundisha sio mchezo na kitu kingine ni kwamba watoto wanasoma kwenye shule hizi ni wale waliochunjwa sana, yaani ni wale VIPANGA kwa lugha ya wasomi kwa hapa bongo!
 
Tuhuma za fedha kutumika kuhonga wasimamizi na walinzi wakati wa mitihani, hasa kwenye shule binafsi, awamu hii ya utumbuaji majipu izifanyie kazi.
kiswahili cha kwenye mtihani si cha kuongea,ingekuwa hivyo wale waliozaliwa uswahilini ndo wangeongoza mtihani wa kiswahili
 
Hata watoto wa kijaluo baadhi tuliosoma nao wakiongea kiswahili anakuwa the comedy kwenu lakini kuandika tulikuwa hatufui dafu
 

Hata kama sikubaliani na wewe kwa baadhi ya issues, lakini nimependa namna ulivyojenga hoja yako. CONGRATULATIONS.
 
Hilo swali waulize watu wote waliosoma combination za sayansi kama PCB,pcm hawa Kiukweli kwa kushuka tu ni hatare lakin mwambie aongee english ni mitihani,fanya utafiti utajua


Mkuu ni ukweli ambao hauna shaka yani ukitaka kucheka waambie watu hao waongee kingereza aisee utacheka
 
huyu amesoma tanzania tangu 2006 atashindwaje kufaulu
 
Wakati tunaingia chuoni..kuna mzungu alifeli screening test ya English wakati sisi wengine tulipeta..sasa sioni haja ya kushangaa...
mlimwuliza ni mzungu wa wapi? maana isijekua jamaa alikua mreno mkategemea angekua vizuri kwenye ngeli. ukweli ni kwamba si kila mzungu anajua vema kimombo.
 
Unaweza kujua lugha ukashindwa kutamka maneno bali ukajua kuyaandika.
Ndiyo hayo maneno yako kweli kbs !! Mie nilikuwa msemaji kweli shule mtaani mjini..ila ktk mitihani yote ya kiswahili sikuwahi kupata hata D!! ilikuwa zero tupu!!
 
Mi nilidhani utauliza alipataje B ya kiswahili na sio ya kiingereza,kwasabab hata kiingereza sio lugha yake!.
 
Sizitaki mbichi hizi! Wivu tu, tambua hizi shule zinafundisha sio mchezo na kitu kingine ni kwamba watoto wanasoma kwenye shule hizi ni wale waliochunjwa sana, yaani ni wale VIPANGA kwa lugha ya wasomi kwa hapa bongo!
Bahati nzuri ni kuwa nina uzoefu na hizo shule. Nilishawahi kuona cases nyingi za wanafunzi kupewa hints za mtihani. Japo nakubali kabisa bila shaka yoyote kuwa hizi shule zinafundisha vizuri sana na wanafunzi wake wana uwezo mzuri. Lakini kwenye mtihani huwa wanapewa hints nyingi sana. Jambo jingine ni kuwa japo wanaonyeshwa lakini ni kwa disaini fulani hivi kiasi kwamba kama mwanafunzi hana uwezo hataweza kupasi.
 
tanzania kweli ni tanzania,........ hongera mchina.... embu tumpate na yule binti aliyekuwa wa kwanza kiingereza kapata ngapi?
Well said, sawa anastahili hongera kwan amejitahidi sana kwa kweli lakini mbona hatuoni the same publicity to the first runner up. Mimi naona si sawa kwa kumfanya huyu mchina kuwa ndio central theme ya ufaulu wa mitihani ya kidato cha nne. Embu tumpe credit na mdogo wetu aliyeshika nafasi ya kwanza.
 
Duuuuu wa Tz tupo nyuma jamani na inabidi tuamke sasa mana hata watu wa nje wanakuja nchini na wanatupita kirahisi tu....
 
Alitisha sana
 
Jamii za asia
Wachina
Singapore
Taiwan
Korea
Japan
Ndio binadamu wenye iq kubwa duniani sababu kubwa ni diet yao ambayo ni protein rich
 
Kuna mahali nilisoma kwamba huyo ni mtanzania, yaani ni raia wa Tanzania. Kama hivyo ndivyo kumuita mchina ni vibaya. Yeye ni mtoto kama watoto wengine. Hongera zake kwa kufanya vizuri
Ni mchina bwana acha ubishi
Mtanzania ana jina la kichina?!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…