Mchepuko wa Kikorea umeng'ang'ana nirudi nao Tz

Mchepuko wa Kikorea umeng'ang'ana nirudi nao Tz

Kuna African movie moja intaitw Billo from Dakkar it's very interesting. Billo alisoma Madras Mali, baadae alifundishwa charahani, alitafutiwa mchumba. Kabla ya kuoa alikwenda Italy kwa boat, katika kuhustle na maisha akakutana na msichana mzuri sana wa kiitaliano, yule msichana alimsaidia Billo kupata tender ya kushona jeez za mpira. Ndugu zake yule msichana walikuwa against Billo lakini wote walipendana.

Siku Billo anakwenda Mali mwitaliano alitaka kwenda lakini Billo alikataa. Amefika Mali Billo alimuoa mchumba aliyekuwa anamsubiri mchumba akitegemea anakwenda Ulaya baada ya ndoa alikuwa disappointed Billo alimwambia utakuwa mke wa Afrika. Aliporudi Rome alimwambia siri binamu yake kuwa nimeoa home, binamu kiherehere mpaka familia ya msichana, akawaambia, msichana alikuja juu, Billo alimwmbia sikiliza mimi Mwislam ninaweza kuwa na wake wawili.

Italy alifunga ndoa ya bomani, basi aliishia kuwa na wake wawili na wote walielewa position zao. Unaweza kuipata hiyo movie you tube.
 
Wewe ni mkiristu na kwa hiyo nitakayosema hapa utayaelewa:
1.Maisha ya Kristu kama Mungu na binadamu yawe rejea katika suala hili.Kwamba kunapotokea tatizo shurti suluhisho hata kama ni la kufedhehesha kiasi gani lichukuliwe.Kukimbia matatizo sio njia aliyowahi Yesu kutuasa hata siku moja.Yeye aling'ang'ania msalaba hadi dakika ya mwisho
2. Time heals.Mkeo mtanzania na Mkorea ni watu wamekulia tamaduni tofauti kabisa.Unahitaji kumfundisha taratibu na kwa upole kwamba hilo lilotokea ni mambo ambayo Afrika yanatendeka.Njoo naye kuwa naye karibu.Usijaribu kumuumiza akiwa mjamzito.Ni kipindi anahitaji utulivu sio vurugu.Mkeo mtanzania ukifika mueleze.Hataelewa lakini wewe umeshakosa kama ambavyo yeye pengine amekosa kwa mambo mengine japo kuwa wewe hujui.
3.Tukio la wewe kuanguka dhambini usiliangalie kwa sura moja tu ya ubaya.Mungu ndiye anajua yote.Yapo mambo huja kwa sura ya ubaya lakini nyuma yake ni neema na yapo yajayo kwa sura nzuri lakini nyuma yake ni ubaya mkubwa.Usifikirie utafika Mbinguni kwa sababu umeweza ku-maintain ndoa ya mke mmoja mume mmoja na wala usifirie hutafika mbinguni kwa sababu ya kuongeza Mkorea
4.Huyo Mkorea kwa huo mtaji alionao nao unaweza kumuanzishia biashara nyumbani na ikawa msaada baadaye hata kwa mke mwenzie
Mafundisho ya dini hayana maana kama mwisho hayalengi kumsaidia mwanadamu.Mwanadamu hayupo kwa sheria na torati bali torati kwa ajili ya mwanadamu.Unakumbuka majibu ya Yesu juu ya wanafunzi wake kuparamia masuke ya ngano siku ya Sabato?
4.Hakikisha hatua yoyote utakayochukua hai-spoil passport yako.Dunia ya leo ni kijiji.
 
Wadau,

Nahitaji mchango wa mawazo yenu kama kichwa cha habari kinavyojieleza. Kisa chenyewe ni hivi mimi ni diaspora ambaye nipo Korea kimasomo tangu November 2014. Mwezi Juni 2016 nahitimu masomo. Nimeoa na tumebarikiwa kuwa na watoto wawili.

Nikiwa huku Korea ya Kusini nilianza mahusiano na mdada wa kikorea, ni mrembo ila si wa kutisha sana si unajua watu wa ukanda huu kinachowapendezesha ni rangi tu waliyonayo vinginevyo kama wangelipakwa rangi nyeusi hakuna atakaye watamani.

Mdada huyu anajiheshimu sana tulianza kuzoeana kama classmate tu. Alikuwa karibu sana na mimi mpaka tukaanza kuvuka mipaka na kuwa wapenzi. Kosa nililofanya ni kwamba sikuwahi kumweleza ukweli kuhusu hali yangu ya ndoa, yaani nilimdanganya kwamba mimi sijaoa.

Tulianza mahusiano kwa siri kwasababu ya kuhofia jamaa zake wasijue kuwa anamahusiano na ngozi nyeusi. Ilifika wakati usiri ukawa unashindikana maana tulikuwa tunaenda club pamoja na kurudi na kulala aidha sehemu ninayoishi au anayoishi yeye. Kuna wakati mama yake aliwahi kuja juu sana akasema kwamba niachane na bintiye vinginevyo ataliwasilisha swala hilo polisi na ninaweza kufutiwa visa ya kuishi Korea.

Tulishauriana na binti kuwa tuachane ili nisije nikaharibu future yule binti akadai yeye akadai hawezi kuachana na mimi kwasababu hajawahi mjua mwanamume mwingine zaidi yangu tangu azaliwe. Na swala la yeye na mama yake anasema hawezi fanya chochote kwasababu yeye ni mtu mzima anapaswa kufanya maamuzi yake bila kuingiliwa na mtu. Nilimsihi tuendelee kwa siri ili nisije nikaharibikiwa kimasomo.

Mwezi uliopita mdada kanimaliza kabisa kaniambia anaujazito wangu, nimechoka mpaka sasa anasisitiza kuwa tunarudi wote Tanzania. Mwanzo nilijua ni utani lakini mpaka nimejua kuwa hatanii. Kwasababu ya urahisi jana Jumatatu nilimtuma yeye aende kunikatia ticket ya ndege amerudi na ticketi mbili yangu na ya kwake tunayosafiri pamoja.

Nimeshikwa na mfadhaiko, nimejaribu kumwambia tu kwa busara kwamba yeye angebaki kwanza ili nikafanye maandalizi ya kumpokea maana mimi nilipotoka nilikabidhi nyumba niliyokuwa naishi hivyo kwenda mahali na mgeni sina mahali pa kufikia itakuwa si vizuri.

Yeye amesisitiza kuna shida gani nikatapo lala naye atalala hata kama kibarazani. Pia akasema hawezi kuendelea kuwepo Korea maana ndugu zake wanaweza hata kumwambia atoe ujauzito wangu na pia wanaweza kumtenga ni heri akaondoka akaenda kuishi na mtu anayempenda hata kama ni sehemu ya tabu.

Kuhusu pesa yeye anasema sio shida anakiasi cha fedha ambazo ukizibadili zinaweza kufikia hadi 150 m ambazo zilikuwa ni mirathi ya marehemu baba yake. Kiukweli mdada huyu amenisaidia sana kifedha. Sikuwahi kuwa na shida ya kifedha muda wote nikiwa Korea.

Hofu yangu ni nyumbani ambako mke na watoto wangu wananingojea kwa hamu, nimeshindwa hata kuwanunulia zawadi maana huyu mdada anajua kila kitu ninachofanya. Ndani kwangu ni kama kwake. Jana nilipanga nimwambie ukweli lakini nilipokuwa namtazama nikajua anaweza nivuruga mpaka nikashindhwa kufanya mitihani yangu ya mwisho. Pia nilimwonea huruma sana kwamba naye anaweza asifanye vizuri hiyo mitihani yake. Ananipenda sana mpaka namuonea huruma sijui nikimwangalia.

Nilikuwa nafikiri nimwache wakati narudi nikifika Doha wakati wa kubadili ndege nimchenge potelea mbali hata kama nitakula hasara ya ticket. Lakini nimejikuta naona hiyo itakuwa ni kazi bure maana mdada huyu anajua mpaka ninapofanya kazi anwani yangu ya Tz anazo hata akaunti namba ya benki yangu anayo mana kuna wakati nikiwa likizo Tz alishawahi kunitumia pesa kwenye akaunti zangu.

Mke wangu na wanangu wananisubiria kwa hamu sana, na wanadai niwapelekee zawadi japo natoa kisingizio kwamba nimebakiwa na fedha ya nauli tu. Cha ajabu wife akasema basi atanitumia kwa Western Union mana kuna vitu nilishawahi kuwapelekea ni vizuri sana na vilikuwa vinauzwa bei ya chini sana. Huku mrembo wa kikorea naye anahesabu siku zilizobakia ili aweze kuruka nami kuja Tz.

Msaada wa kutatua tatizo hilo wadau. Niko njia panda nampenda mke wangu nawapenda wanangu. Namhurumia Mkorea alivyojitoa kwangu.

Nawasilisha kwa ajili ya ushauri.
Mkuu nianze tu kwa kukupa pole..hilo jambo ni lakwaida kabisa hasa hasa kwa waafrika wengi waishio nchi za wazungu.. Waafrika waliowengi wanakosaga kabisa control wakikutana na wazungu kimapenzi..wanajiona wa maana sana..na mara nyingi hutegemea kufaidi kifedha kutoka kwa wazungu...Naongelea wote wanaume na wanawake.
Sasa kwa swala lako hili..kwanza ukubali umekosea sana na hakuna reverse yakurekebisha kosa hilo...mimi nakushauri kwanza maliza mtihani wako, kisha baada ya mthihani mwite huyo mkorea wako pahali then mwambie ukweli wote kua una familia achague chakufanya...ataumia sana ila atakubali tu coz ndo ukweli huo...
Ukubaliane na kitakachotokea. Huyo mkorea akijua ukweli..badae atafanya abortion akusahau kabisa.

Ila mkuu iwe fundisho kwako...usijesema uongo tena.
Wacha dhambi na usijikoshe eti unampenda mkeo wakati umemsaliti.
 
Mkuu nianze tu kwa kukupa pole..hilo jambo ni lakwaida kabisa hasa hasa kwa waafrika wengi waishio nchi za wazungu.. Waafrika waliowengi wanakosaga kabisa control wakikutana na wazungu kimapenzi..wanajiona wa maana sana..na mara nyingi hutegemea kufaidi kifedha kutoka kwa wazungu...Naongelea wote wanaume na wanawake.
Sasa kwa swala lako hili..kwanza ukubali umekosea sana na hakuna reverse yakurekebisha kosa hilo...mimi nakushauri kwanza maliza mtihani wako, kisha baada ya mthihani mwite huyo mkorea wako pahali then mwambie ukweli wote kua una familia achague chakufanya...ataumia sana ila atakubali tu coz ndo ukweli huo...
Ukubaliane na kitakachotokea. Huyo mkorea akijua ukweli..badae atafanya abortion akusahau kabisa.

Ila mkuu iwe fundisho kwako...usijesema uongo tena.
Wacha dhambi na usijikoshe eti unampenda mkeo wakati umemsaliti.
ushauri mzuri sana huuu
 
MwanaDiaspora, pole kwa unayopitia. You have crossed the line, you are just facing the consequences.
Swali kwamba ufanyaje sio sahihi kwa sasa, kwa waliowahi kukosea kwa namna hii wanajua kuwa ni swala la muda tu Kabla dunia haijakujua vizuri.
Mkeo atajua vile ulivyo, hata watoto wako pia.
Haya ni aina ya makosa ambayo ukijaribu kuzuia matokeo yake basi inazidisha damage.
Unaweza kufanya yafuatayo.
1. Mweleze binti wa Kikorea kuwa una mke na watoto ( haitamshangaza maana Waafrika hatuaminiki Sana)
2. Kwa mkeo subiri kidogo, huna haja ya kukwambia chochote kwa sasa mpaka utakapopata response ya Mkorea ambaye she will likely opt for abortion.
3. Don't feel guilty..haisaidii you are guilt already
4. Sio wakati wa kutangazia ulimwengu kuwa unampenda sana mkeo kilichofanyika ni kinyume kabisa na maneno hayo labda Kama una maana nyingine ya Upendo.

Acha tusubiri.
Point namba nne nimeielewa hasa
 
Uongo Ni mbaya, and it will cost u, mwambie ukweli akikufuata awe ameufaham


Wadau,

Nahitaji mchango wa mawazo yenu kama kichwa cha habari kinavyojieleza. Kisa chenyewe ni hivi mimi ni diaspora ambaye nipo Korea kimasomo tangu November 2014. Mwezi Juni 2016 nahitimu masomo. Nimeoa na tumebarikiwa kuwa na watoto wawili.

Nikiwa huku Korea ya Kusini nilianza mahusiano na mdada wa kikorea, ni mrembo ila si wa kutisha sana si unajua watu wa ukanda huu kinachowapendezesha ni rangi tu waliyonayo vinginevyo kama wangelipakwa rangi nyeusi hakuna atakaye watamani.

Mdada huyu anajiheshimu sana tulianza kuzoeana kama classmate tu. Alikuwa karibu sana na mimi mpaka tukaanza kuvuka mipaka na kuwa wapenzi. Kosa nililofanya ni kwamba sikuwahi kumweleza ukweli kuhusu hali yangu ya ndoa, yaani nilimdanganya kwamba mimi sijaoa.

Tulianza mahusiano kwa siri kwasababu ya kuhofia jamaa zake wasijue kuwa anamahusiano na ngozi nyeusi. Ilifika wakati usiri ukawa unashindikana maana tulikuwa tunaenda club pamoja na kurudi na kulala aidha sehemu ninayoishi au anayoishi yeye. Kuna wakati mama yake aliwahi kuja juu sana akasema kwamba niachane na bintiye vinginevyo ataliwasilisha swala hilo polisi na ninaweza kufutiwa visa ya kuishi Korea.

Tulishauriana na binti kuwa tuachane ili nisije nikaharibu future yule binti akadai yeye akadai hawezi kuachana na mimi kwasababu hajawahi mjua mwanamume mwingine zaidi yangu tangu azaliwe. Na swala la yeye na mama yake anasema hawezi fanya chochote kwasababu yeye ni mtu mzima anapaswa kufanya maamuzi yake bila kuingiliwa na mtu. Nilimsihi tuendelee kwa siri ili nisije nikaharibikiwa kimasomo.

Mwezi uliopita mdada kanimaliza kabisa kaniambia anaujazito wangu, nimechoka mpaka sasa anasisitiza kuwa tunarudi wote Tanzania. Mwanzo nilijua ni utani lakini mpaka nimejua kuwa hatanii. Kwasababu ya urahisi jana Jumatatu nilimtuma yeye aende kunikatia ticket ya ndege amerudi na ticketi mbili yangu na ya kwake tunayosafiri pamoja.

Nimeshikwa na mfadhaiko, nimejaribu kumwambia tu kwa busara kwamba yeye angebaki kwanza ili nikafanye maandalizi ya kumpokea maana mimi nilipotoka nilikabidhi nyumba niliyokuwa naishi hivyo kwenda mahali na mgeni sina mahali pa kufikia itakuwa si vizuri.

Yeye amesisitiza kuna shida gani nikatapo lala naye atalala hata kama kibarazani. Pia akasema hawezi kuendelea kuwepo Korea maana ndugu zake wanaweza hata kumwambia atoe ujauzito wangu na pia wanaweza kumtenga ni heri akaondoka akaenda kuishi na mtu anayempenda hata kama ni sehemu ya tabu.

Kuhusu pesa yeye anasema sio shida anakiasi cha fedha ambazo ukizibadili zinaweza kufikia hadi 150 m ambazo zilikuwa ni mirathi ya marehemu baba yake. Kiukweli mdada huyu amenisaidia sana kifedha. Sikuwahi kuwa na shida ya kifedha muda wote nikiwa Korea.

Hofu yangu ni nyumbani ambako mke na watoto wangu wananingojea kwa hamu, nimeshindwa hata kuwanunulia zawadi maana huyu mdada anajua kila kitu ninachofanya. Ndani kwangu ni kama kwake. Jana nilipanga nimwambie ukweli lakini nilipokuwa namtazama nikajua anaweza nivuruga mpaka nikashindhwa kufanya mitihani yangu ya mwisho. Pia nilimwonea huruma sana kwamba naye anaweza asifanye vizuri hiyo mitihani yake. Ananipenda sana mpaka namuonea huruma sijui nikimwangalia.

Nilikuwa nafikiri nimwache wakati narudi nikifika Doha wakati wa kubadili ndege nimchenge potelea mbali hata kama nitakula hasara ya ticket. Lakini nimejikuta naona hiyo itakuwa ni kazi bure maana mdada huyu anajua mpaka ninapofanya kazi anwani yangu ya Tz anazo hata akaunti namba ya benki yangu anayo mana kuna wakati nikiwa likizo Tz alishawahi kunitumia pesa kwenye akaunti zangu.

Mke wangu na wanangu wananisubiria kwa hamu sana, na wanadai niwapelekee zawadi japo natoa kisingizio kwamba nimebakiwa na fedha ya nauli tu. Cha ajabu wife akasema basi atanitumia kwa Western Union mana kuna vitu nilishawahi kuwapelekea ni vizuri sana na vilikuwa vinauzwa bei ya chini sana. Huku mrembo wa kikorea naye anahesabu siku zilizobakia ili aweze kuruka nami kuja Tz.

Msaada wa kutatua tatizo hilo wadau. Niko njia panda nampenda mke wangu nawapenda wanangu. Namhurumia Mkorea alivyojitoa kwangu.

Nawasilisha kwa ajili ya ushauri.
 
Kwanza pole na ukome vilevile.Truth heals,na usitegemee kufunika kosa kwa kosa tena.
Mwisho story yako very interesting bongo muvi wachukue hii script ya bure
Nami naiona kama story maana amesema mkorea yupo smart na ameishampekua jamaa anajua mambo mengi kumhusu eti ashindwe kujua kama ameoa na familia? Ngumu kumeza, kwa vile tumeambiwa ana wivu anapekua kila kitu itawezekana vipi awe hajaona hata picha za familia, calls za wife, hata documents za usajili wa vyuo vingi nje huwa unajaza marital status!!! Kama amemudu kumficha haya yote kwa muda wote basi anaweza kuficha zawadi atakazonunulia familia na Kumficha mkorea buguruni kwenye chumba atakachompangia wakifika bongo.
 
Nami naiona kama story maana amesema mkorea yupo smart na ameishampekua jamaa anajua mambo mengi kumhusu eti ashindwe kujua kama ameoa na familia? Ngumu kumeza, kwa vile tumeambiwa ana wivu anapekua kila kitu itawezekana vipi awe hajaona hata picha za familia, calls za wife, hata documents za usajili wa vyuo vingi nje huwa unajaza marital status!!! Kama amemudu kumficha haya yote kwa muda wote basi anaweza kuficha zawadi atakazonunulia familia na Kumficha mkorea buguruni kwenye chumba atakachompangia wakifika bongo.
Hapo umenena mkuu
 
Nami naiona kama story maana amesema mkorea yupo smart na ameishampekua jamaa anajua mambo mengi kumhusu eti ashindwe kujua kama ameoa na familia? Ngumu kumeza, kwa vile tumeambiwa ana wivu anapekua kila kitu itawezekana vipi awe hajaona hata picha za familia, calls za wife, hata documents za usajili wa vyuo vingi nje huwa unajaza marital status!!! Kama amemudu kumficha haya yote kwa muda wote basi anaweza kuficha zawadi atakazonunulia familia na Kumficha mkorea buguruni kwenye chumba atakachompangia wakifika bongo.
Aiseee kumbe anaweza mficha mkorea buguruni??
 
Dili nipe namba ya mkeo unifumanie naye and then mtimue Maisha yataenda... Watoto utamuambia umesingiziwa ni wangu ila unawapenda moyoni... na unataka kuishi nao kama baba yao wa kufukia... ila ndio mkeo nitampangia sehemu niwe namla kimapozi tu hutoumia am sure.. Bonge la Ushauri... Habari ya Kifacebook inajibiwa kifacebook pia Alamsiki.
 
Nimefananisha story yako na movie za ki_Korea yaani chief umelenga kweli doo!!
 
Usimuache huyo binti. Kwanza subiri mtihani uishe mpange safari.

Mwambie huyo mkeo wa bongo ulimzalisha long time so huna jinsi.

Kiukweli hapo ukizingua tu umemuua huyo binti.
 
Hahahaha hii kitu inanikumbusha mshua alimtania mama siku moja nitakuletea Mke wa Kikorea hapa ndani ,tuone utafanyaje ,kiswahili hajui wala kingereza ukimzingua ni huuu haaa za kutosha

Dah sina hata cha kukushauri ila nikutakie kila la kheri kwenye maamuzi yoyote utakayo chukua hata kama ni kujitundika
 
Back
Top Bottom