Mchepuko wa Kikorea umeng'ang'ana nirudi nao Tz

Mchepuko wa Kikorea umeng'ang'ana nirudi nao Tz

Pole kaka yangu mnayataka wenyewe, mnatupa nasi pressure tulio na waume zetu ulaya, mie nakushauri kata nyingine tiketi th ya nyuma ya hiyo nyingine cku hiyo mtoroke ukiondoka mtumie email mweleze ukweli huku ukiweka mazingira kwa mkeo, mme anauma. Watz tumezidi uongo.
 
From Korea with love part 1,kama hukujifunza kung fu huko Korea hamna namna mchukue tu.
 
Wakorea awana dini ya uislam wala ukristo. Wao Wana amini Mizimu. Duh? Apo apande nae ndege aje nae bongo. Akifika apo Dar es salaam Tanzania. Afanye ujanja fulani aende nae mpaka hotel nzuri kama New Africa hotel pale amchukulie chumba kama wiki 2. Alafu Afanye mchakato wa nyumba maeneo ya mbezi beach. Apo anatakiwa ajifanye kama kukaa nje ya apo Tanzania kumemuasili lakini ajiibe kwenda kumcheki uko alipo anatakiwa awe bonge la msanii
 
chukua hyo kim nanaa ...,...mtoto wako na mkorea lazma atoe series "gu family book"
 
usipoteze milioni 150 za bure hizo utakuja kujutua mbele ya safari
 
Kiongozi pole natumain haujaja kutafuta public simpathy lakin wew ni mtz i no u can handle that matter we ibuka nae lakin wife mpe kwanza kalenda deal kwanza na alie na mimba then taratibu anza kumpa ukweli
 
Mh hiyo trust ya mkorea ... be very watchful, anaweza akajifanya vibaya ukapata kesi mbaya. Hapo maji yeshamwagika. Malizeni mitihani halafu muambie, akikubali mwambie mkeo wa tz pia. Halafu mchukue mkorea nenda naye TZ, by default ni mkeo kama aliyo mkeo aliyeko tz. Na mtoto atakayezaliwa na mkorea ni mtoto wako kama hao wengine. Kuhusu ukristo, utatubu dhambi, na Mungu ni mwema, atakusamehe.
 
Nina rafiki yangu amekwama Philippines kwa mambo haya haya ya kuendekeza upumbavu, yehe hataki kurudi na familia yake inataka kumfata alipo watoto wamekuwa, alitoka na demu chuo australia wakaishia huko kwa familia ya mwanamke walimchukia ila sasa anaishi nao vizuri
 
Hapo akishaujua ukweli,sita ya ulaghai tunapewa watanzania wote ila hakuna namna mlete tu shemeji
 
Ila inauma eeh!!! Wengi mmemshauri amwambie mkewe ukweli kua anaoa mke mwingine yaani huyu Korea hamjawaza kua hata mke nae ataumia amelea familia toka 2014 akijua mmewe yuko masomoni
Leo fadhila yake kuletewa mke mwingine? Kweli? Wewe kaka bora hiyo ndege utakayopanda ipoteze mawasiliano huko angani familia italia weeee eeee baada ya
muda watazoea kuliko kuwaletea mke mwenza atayeleta ufa ktk hii familia.

Kwa maneno yako ni kwamba jamaa hatakiwi kusamehewa...,? je ww ushawahi fanya kosa lolote ?
Kama ushawahi sijui kama maneno haya yana maana yoyote....
 
maliza kwanza mitihani ndo umueleze ukweli ukiwa na ushahidi wa picha
 
Nipe Mimi Demu wa buree na mimba ya buree.To a stress nipe Mimi nitalea hiyo mimba
 
Mimi nachangia kwasababu umeomba ushauri au ulitaka nikwambie kile kinachokufurahisha?!

Mnafki sana na nawish mkeo ajue aina ya nyoka anayeishi naye ndani ya nyumba..

Kama ulitaka ushauri ndio huo nimekupa cheza na mtoto wa watu unyongwe ....

Umechagua kuishi kisanii endelea kuishi kisanii usikimbie kivuli chako..

Kwanza mimi sijaja kukushauri nimekuja kukusimanga tu.

Sasa masimango ya nini na mtu kaomba ushauri???ni kweli ulikuwa huna la kumshauri kwanini usipige kimya tu badala ya kuleta Frustration kwa mtu aliye frustrate????mshauri kwanza kulingana na ombi lake then masimango baadaye
 
sina ushauri, ila lolote laweza kuwa, Korea sio Bongo, wanawake wa Kiasia nawaelewa vema. Husijaribu kusema ukiwa kwenye ardhi yao. Ukimtoroka na anayo address atakuja tu maana anayo mimba yako. Umeficha hukusema ukweli hawa watu kuwa na mahusiano na ngozi nyeusi ni shida, wewe ana mimba yako. hawezi kukaa kwao lazima akufuate. Chalii wa Arusha wanasema imekula kwako.

Ondoka naye mlete Bongo, Mweke mahali, then mueleze ukweli na mwambie aamue na unampenda. mwambie utaishi nao wote. ninavyowaelewa hao mwanzoni ataoverlook ila kuna muda atachomoa na kurudi kwao, ila atakuwa ameshakuwa na maamuzi ya kukuacha kwani atakuwa amejua kama alivyoambiwa wanaume wa kiafrica ni matapeli. ni matepeli kweli. huo utakuwa mwisho wake wa kufuata watu wasiokuwa na P.o Box
 
Back
Top Bottom