Mchepuko wa Kikorea umeng'ang'ana nirudi nao Tz

TUNAZIDI KULIFANYA TAIFA LETU LIZIDI KUWA JUU KWA UONGO....
Binafsi huwa najivunia sana kusema kuwa nimeoa.....na hata wedding ring toka nimeoa sijawahi IVUA....
....KUNA WAZO LA MSINGI UMELETA...Inamaana jamaa muda wote hakuwa akivaa wedding ring.
 
Daa nashindwa kupata picha ya litalotokea pindi mumeo akifanya issue kama yangu. Unaweza ua kabisa.
 
Nimelipenda hili wazo, nitalizingatia. Ila itabidi niache baadhi ya vitu vyangu ili asishitukie mapema.
Hapana sio wazo zuri ulikwisha weka mambo katika uficho ni wakati wa kuweka mambo wazi .Maliza mitihani yako hakikisha dada nae amemaliza mithihani yake ili usimchanganye .Mueleze ukweli ili kweli ukuweke huru ni bora umwambie mapema mkiwa huko iliafanye maamuzi yaliyosahihi mapema ,kumbuka yule dada hana support ya wazazi kwenye mahusiano yenu sasa ukianza kumtelekza utamfanya ajute maisha
Angalau umweke wazi ajue ashike kuti lipi lakini wazo la kumchukua na kuja nae TZ sio sahihi kumbuka wakati huu family yako inakuhitaji sana kwasababu haijawa na wewe muda mrefu utatakiwa utoe muda wako kwaajili yao ,Na pia mkorea ni mgeni atakuwa anahitaji kampani ya kutosha kwasabau hamjui yeyote usiendelee kucheza na moto maliza uliyoyaanzisha kwa kutumia busara na akili
Chuja uashauri unapowa na watu usikurupuke ndugu ,ni hayo tuu
 
....hawezi akakaa siku nzima bila kuonana.
I SEE!..pole sana...hapa utakutana na shauri mbalimbali zenye kujenga ama kubomoa,..walau waweza hata kumuonesha mkeo huu uzi ku''seek'' sympathy...Mwisho wa siku ukweli utajulikana tu.Tatizo ni lini na italeta madhara gani.Imebaki kitendawili.Labda uanze kwa kuwaona wanasaikolojia/washauri wa masuala ya ndoa wakuandae namna ya kudeal na hili tatizo...
 
Mkuu hoja yako imeshajibiwa pitia comment vizuri. Refer comment no #128#
 
Malezi yetu watu weusi, hatuna uaminifu wala uwazi!
 
TUNAZIDI KULIFANYA TAIFA LETU LIZIDI KUWA JUU KWA UONGO....
Binafsi huwa najivunia sana kusema kuwa nimeoa.....na hata wedding ring toka nimeoa sijawahi IVUA....
Heri yako usiyedanganya. Kumbuka uongo ni uongo tu.
 
duuu hatari sana
option zako kiboko nmekubali.
magufuli ana kazi sana kama upo mtandao wa mafisadi
MBONGO NI MBONGO TU HATA AWE UGHAIBUNI hakosi njia
"Mtoto Wabibi" mimi ni mtoto wa mkulima, siko na mafisadi mkuu. Nimejaribu kufikiria tu namna familia yake itakavyopata shida sababu za uzembe wa huyu jamaa. Nikaona bora huyo binti wa kikorea amuache kwa style ile ili akifika bongo basi ataweigh mwenyewe maana kakaa Korea si chini ya miaka 3...atakuwa amemzoea na pengine hapa anatuonjesha tu ila maamuzi ya mwisho keshafanya.

Kama bado hajafanya na hajapigwa limbwata la kikorea, ajitahidi amtoroke kwanza, akifika bongo lazima mapenzi na huyo mkewe kwa sasa yatakuwa yamepungua ila kwa vile wako mbali mbali na kuna watoto nafsi inamsuta. Hivyo, bora hawa watoto waendelee kupata malezi yao wote wawili huku akijiandaa kumpokea mkewe wa majuu!!

Kama ataweza si yeye kidume bwana!! akishasoma upepo ampangishie kwake hapo bongo dar es salaam awe na wake wawili. Hawa wanawake watazoea, na huyo mkorea akishapata mtoto mapenzi yatahamia kwa mtoto hatakuwa king'ang'azi muda wote.
 

Amani sana mkuu laiti ingekuwa imenitokea mimi Ushauri wako umekaa poa sana japo inahitaji mtu mjanjajanja kama wewe.vinginevyo ata fail
 
Duh,hii ni ngumu aiseee......ila pole sana mkuu,haya mambo yanaweza mtokea mwanaume yeyote sioni sababu ya watu kuanza kumlaumu na kutoa maneno makali na hata,matusi
Haya mambo yapo....anyway tumia ushauri wa wadau wa kumtoroka kwanza uje huku na ukifika ndo unampigia kumueleza ukweli maana ukimwambia ukiwa huko anaweza kukuua wewe au kukuharibia maisha!!
 
Ushauri mzuri ila chukulia ww ndie ungekua wife wa jamaa ungepokeaje hiyo taarifa....
 
Ushauri mzuri ila chukulia ww ndie ungekua wife wa jamaa ungepokeaje hiyo taarifa....

Uzuri katika maisha hakuna formula moja kuwa wote tuifuate, ndio maana wengine wanaoa mwanamke mwenye mtoto, wengine wanaoa aliemzidi umri. My take, mpaka hawa wawili wanafunga ndoa walielewana, sasa ni mke wake aamue akishajua ukweli kusuka au kunyoa.
 
Majanga hayo Braza bt kwa ushauri wangu usije ukatelekexa familia hio laana ambayo aitafutika
 
Walioisoma yote naomba wanipe mukhtasari.

Nimeshindwa kusoma, ndefu
 
Ingekuwa hawa madem zetu wa bongo ungeweza kumpaki hotelini afu we ukaenda kusabahi family yako. Lakini hii ngozi nyeupe upendo wao tofauti kabisa mtafuatana mpk chooni, wanalindaga wapenzi wao kwa garama zote, hawataki hata urafiki na mtu mwingine wa kawaida ni wewe na Yeye tu popote. Cha kufanya fanya mtihani ukimaliza mweleze ukweli afu akulaumu na utajibu ulimdanganya coz ulikuwa unampenda so hukutaka uhusiano wenu uvunjike. Ikifika hapo ataamua uje nae ama la. Ukiona bado anataka uondoke nae bas uje nae tu huna namna. Sasa itabaki namna kutomweleza mkeo tarehe kamili ya kuja kwako ili upate mda wa kuandaa makazi ya mkorea kwa mda. Maliza kesi kwa upande moja tu kwanza usiwaeleze kwa wakati moja. Mkeo atakuelewa kwa haraka na atajua usingeweza kuishi mwenyewe mda wote bila mpenzi.
 
Umekuja kumsimanga ili iweje? Toa ufafanuzi au kuna jambo unalifahamu zaidi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…