dailema ipo. kama wewe mwanaume bado umebakiwa na ubinadamu lazima hisia za kusaliti wanawake wawili, na hatma ya mtoto wako zitakuandama, na uamuzi wowote utakaochukua utawaathiri wanawake wote wawili na mtoto wako na wewe mwenyewe. ni jambo zito, linahitaji muda kufanya maamuzi sahihi kwenye jambo bovu.
kama dada ninayejielewa ni lazima nikuonyeshe kuwa mambo si rahisi, mimi pia ni mwanamke na nafaa kuolewa na wewe ndo maana uliweza kuwa na mimi kwa miaka 3 ukiniambia huna mwingine zaidi yangu. kama uliweza kunivumilia miaka 3 hutashindwa kunivumilia milele. tukae tulee watoto, huyo wa ulaya atatafuta mwingine. halafu kwa kuwa ulitaka unisapraiz na pete ya ndoa kidoleni basi nami ndo hivi nakusapraiz. halafu huyo anayependwa nae akijua kasalitiwa na kuna mtoto njiani sidhani kama atabaki yule yule. ndoa inaweza kufilia mbali, wa kukosa mwana na maji ya moto akose.