Mchele wa plastic waingia UDOM

Mchele wa plastic waingia UDOM

Halafu matumizi ya mifuko hiyo kama kifungashio cha chakula cha moto,ilisemekana no hatari kwa afya,ila naona mama lishe wote wanaitumia kufunikia wali,wapishi wa viazi pia wanafunikia kuzuia mvuke,bila kusahau wauza chipsi wa mjini!
Ifike mahali tfda waache kutisha watu kama wameshindwa kudhibiti hili.

Nilienda stand ya Mwanza karibu na ofisi za tfda,nikapewa ugali uko kwenye mfuko wa plastic,nilipowauliza ni kwanini wanaweka humo wakati imepigwa marufuku,wakasema tfda wenyewe ndio wametuambia tuweke humu kuepuka kipindu pindu!Sasa ninyi tfda,hamkusoma shule moja?
 
Acha sayansi uchwara hapa!wewe unajua sayansi wewe?Ukinywa dawa inakuwa digested na enzymes gani?Ama ukameza big g inakuwa digested na enzymes gani?Ficha ujinga wako,hao wanaotengeneza hiyo mi compound wanakuzidi maarifa na akili!
Cha msingi tungeomba wataalam wetu waache siasa na kazi za mazoea washughulikie jambo hili haraka.
Sawa bwana msomi ni wewe.... Sisi soote darasa la saba.... Endelea.
 
Ndo hata sielewi wamefanyaje mpaka plastic inayotakiwa kuyeyuka ikawa mchele upikwe na uumuke?
Kama waliweza mtengenezea ray dawa akanywa akawa mweupe vile?
Kama waliweza mtengenezea wema dawa ya makalio yakawa makubwa vile?
Wanashindwa nini kututengenezea wali unaoyeyuka?
 
Kwa mini msiwaite hao TFDA waje waushuhudie live ili wathibitishe,,manake walidai in rumaz tu...Kama upo basi fanyeni jitihada ijulikane upo coz kinachotakiwa in ushahidi tu. Tunza hicho kitenesi asee usikile mi sijui nimeshakula vingapi masikini wa Mungu sijawahi hata kuwaza kudundisha tonge la wali Mimi!!!!
Mimi ninao room hapa kwa mfuko waje tuwaonyeshe
 
Achana na wali piga dona na wudagala na maharagwe kwa mbaaali bila kusahau kachumbari,achana na vitenesi
 
Mimi naomba waje wataalamu wa kemia(organic chemistry) watueleze unavyoweza kuvunja bond ya plastic kwa kuichemsha kwenye maji.
Watu wapuuzi Achana nao.... Wanavamia fani za watu wakiambiwa wanamwaga povu.
 
Moja ya habari zilizoshtua zaidi na kufanya vijana waamke usiku huu ni video zinazosambazwa katika whatsapp groups zikionesha chakula cha wali kikigeuzwa vitenesi na kudunda kabisa..

Ikiwa ni mojawapo ya ushahidi kuwa ni mchele wa plastic.....
Mwanzo ilikuwa ni fununu lakiin kwa sasa imekuwa confirmed mchele huu upo ndani ya taifa hili..…

TBS, TFDA mko wapi jamani..........
Vijana huku tutaisha kama kuku.....
Tumechanganyikiwa jamani
Usituletee story za kijinga hapa kama kama ndio umeingia form 1. Hivi unaijua plastic wewe?
 
Kwanza plastic ni Ghali kuliko mchele.... Sasa hata kama mwanadamu angeweza kudigest hio plastic... Mchina angepata faida gani? Au unafikiri watu wana pesa za kuchezea.
 
Ujinga ni mzigo kwa taifa na ni adui namba Tatu kwenye list ya mwalimu julius
 
Ndo hata sielewi wamefanyaje mpaka plastic inayotakiwa kuyeyuka ikawa mchele upikwe na uumuke?
Kuna mchele ulikuwa unatoka china ulikuwa wa mahindi, unapika robo unatoka sufuria kubwa mbili wakaja wakaupiga marufuku..
 
Ndo hata sielewi wamefanyaje mpaka plastic inayotakiwa kuyeyuka ikawa mchele upikwe na uumuke?
Kuna mchele ulikuwa unatoka china ulikuwa wa mahindi, unapika robo unatoka sufuria kubwa mbili wakaja wakaupiga marufuku..
 
Wajinga mmeanza kusambaza ujinga wenu tena baada ya mwanzo huo ujinga kupotea.....
 
Back
Top Bottom