Mchango uliotolewa na pendekezo la “Ukanda Mmoja, Njia mmoja” kwa Afrika waendana na wakati

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111255073544.jpg


Katika siku za karibuni Kituo cha mambo ya fedha na maendeleo kwenye sekta zisizosababisha uchafuzi (Green Finance & Development Center) katika chuo Kikuu cha Fudan mjini Shanghai, kilitangaza kuwa thamani ya uwekezaji wa China kwenye miradi ya kupitia pendekezo la “Ukanda mmoja, Njia Moja” imefikia dola za kimarekani trilioni 1, na miradi iliyofadhiliwa kupitia utaratibu huo katika nishati katika nusu ya kwanza ya mwaka huu ilikuwa ni ya kijani zaidi kuliko iliyotangulia wakati pendekezo hili linaanza kutekelezwa.

Wakati pendekezo la “Ukanda mmoja, njia moja” linatimiza miaka kumi, na thamani ya uwekezaji wake imefikia dola za kimarekani trilioni moja, kuna mengi ya kutajwa kuwa ni mafanikio makubwa yaliyopatikana kwa nchi mbalimbali katika utekelezaji wa pendekezo hilo, iwe ni kwenye sekta ya ujenzi wa miundombinu au nishati, sekta ambazo kwa muda mrefu zimeonekana kuwa ni changamoto kubwa na kikwazo cha maendeleo hasa kwa nchi za kusini.

Mwezi Oktoba mwaka 2013, Rais Xi Jinping akiwa nchini Kazakhstan alitoa pendekezo hili, ambalo katika siku za mwanzo ni watu wachache sana walimwelewa. Sababu ni kuwa katika historia ya China, ni nchi zilizopitiwa na “njia ya hariri” katikati ya karne ya 15, (kutoka China Asia ya Kati na Ulaya) ndizo zilizonufaika na biashara iliyofanyika kwenye ukanda huo. Mwanzoni nchi hizo zilipokea pendekeza hilo kwa urahisi kutokana na kukumbuka neema iliyoletwa na biashara katika ukanda huo. Mwaka huohuo 2013 Rais Xi alikwenda Indonesia kutangaza pendekezo hilo na kukumbusha njia ya hariri baharini, kuanzia hapo pendekezo hilo lilipokelewa kwa hamasa, na hadi kufikia mwanzoni mwa mwaka 2023, pendekezo hilo lilikuwa na jumla ya nchi wanachama 151 likigusa asilimia 75 ya watu wote duniani.

Utekelezaji wa pendekezo hilo ulipoanza miaka 10 iliyopita, ulionekana kama ni jambo lisilowezekana kwani malengo yake yalihitaji uungaji mkono mkubwa na nia ya kisiasa hasa katika mazingira ambayo baadhi ya nchi za magharibi zilikuwa zikiweka mazingira ya kulikwamisha na kulipinga pendekezo hilo. Lakini ukweli ni kwamba, katika kipindi hicho cha miaka 10, pendekezo hilo ambalo maarufu zaidi kwa jina lake la lugha ya kiingereza yaani Belt and Road Initiative, limekuwa na mvuto mkubwa na kuleta matokeo yanayoonekana kwa nchi nyingi duniani na hasa za dunia ya tatu.

Tukiangalia katika nchi mbalimbali za Afrika, mwanzoni pendekezo hili lilijikita zaidi kwenye kugharamia ujenzi wa miradi ya miundo mbinu hasa ya usafiri. Kuna ushahidi mwingi katika nchi za Afrika Mashariki kama vile Kenya kwenye reli ya SGR, reli ya Ethiopia na Djibouti, na hata reli ya Abuja nchini Nigeria. Licha ya juhudi nyingi tangu miaka michache baada ya uhuru, nchi za Afrika zilishindwa kujenga reli hizi, lakini katika kipindi kifupi cha uhai wa pendekezo la “Ukanda mmoja, Njia moja” ndoto ya muda mrefu kwa nchi za Afrika imetimia. Hali hii pia tunaweza kuiona kwenye barabara au hata viwanja vya ndege.

Kipindi hiki ambapo dunia imekuwa inakabiliana na changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi, pendekezo hili limeonekana kuwa na mchango mkubwa katika juhudi za dunia kubadilisha muundo wa nishati. Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kupitia miradi ya pendekezo hili vituo mbalimbali vya kuzalisha umeme kwa nishati ya jua, upepo na maji vimekuwa vikijengwa katika nchi mbalimbali za Afrika, Asia na hata Amerika kusini. Hali hii inaonesha kuwa pendekezo la Ukanda Mmoja njia moja, sio tu kama linaendelea kuwa na manufaa kwa nchi mbalimbali, bali pia ni pendekezo linaloendana na mahitaji ya sasa ya dunia

.
 
Back
Top Bottom