Kuna wakati fulani Yesu alimponya mtu mmoja mwenye ukoma; akamwambia "nenda kwa makuhani ukajioneshe". Lengo lilikuwa ni kuthibitisha kuwa ameponga kweli na haikuwa hoax.
Wakati mwingine alimponya mtu mmoja aliyezaliwa kipofu. Wakuu wa Makuhani waliposikia habari hiyo hawakuamini na wakawaita wazazi wa huyo jamaa na kuuliza habari zake. Wale wazazi wakasema "yeye ni mtu mzima muulizeni mwenyewe". Yule bwana alipoitwa akawaambia kuwa "mimi sijui kama huyo aliyeniponya ni mtakatifu au la, ninachojua ni kuwa nilikuwa kipofu na sasa naona".
Katika mifano hiyo miwili utaona kuwa kwenye mambo ya miujiza kufanya uchunguzi siyo kukana miujiza bali kuondoa uwezekano wa uongo. Ninaamini miujiza lakini miujiza yote inafanywa kwa kutumia vitu vya asili. So, kuhoji suala la misukule si kukana uwezo wa Mungu kutenda miujiza bali kuthibitisha nguvu hizo na kuzikiri lakini wakati huo huo kuondoa uwezekano wa roho ya mwanadamu kujikweza na kujiinua na kujisamamisha mahali pa Mungu!
Ninachofahamu na kuamini ni kwamba hakuna jambo gumu la kushinda Mwenyezi Mungu. Kwake kila kitu kinawezekana na hujibu maombi kwa saa na majira yake. Kinachotakiwa ni imani yako.
Kwa sayansi ilivyokuwa kwa sasa kumezuka vikundi vya dini au makanisa yenye itikadi mbalimbali za kidini. Katika yote hayo kuna wasanii wale Yesu mwenyewe alisema tujihadhari nao "Manabii wa Uongo". Pia kuna wale kweli walioitwa kwa kazi na makusudi ya Mungu. Inakuwa vigumu sana kuyatenganisha makundi hayo mawili "wakweli na waongo".
Kwa mantiki hiyo si mimi wala wewe unaweza kumsemea Mch. Lwakatare kuwa huenda yupo kundi lipi katika haya mawili. Kinachotakiwa hata wewe hapo ulipo kwa imani yako uliyo nayo unaweza kumwomba Mungu aweze kumdhihirisha huyu mama kama kweli ni tapeli au la. Na mwisho wa siku uovu huwa unajitokeza tu kwani kila kitu kiovu kina mwisho wake kama vilivyo vitu vingine.
Wito, tumweke kwenye maombi na Mungu atajibu. Naona pia media imemwandama sana siku hizi katika itikadi zake na mali zake ikiwa ni pamoja na shule zake.
Pia tuwe makini sana katika kuhukumu tusikute kuna kundi au mtu yuko behind all these. Maadui aweza kuwa nao ukianzia mtalaka wake (sijua kama wamesha divorce rasmi) na wanasiasa pia. Unajua tena ujiko wa Siasa.
Mengi ya huyu mama yameanza kushamiri sana kuandikwa magazetini baada ya kwenda Bungeni. Sisemi kuwa huko awali hajaandikwa but kwa sasa kasi ni kubwa ya kuandikwa.
Hata mimi huwa napata tabu sana kuamini hizi dini na makanisa ya siku hizi maana yamekuwa "profitable business". Tuwe tu makini, fahamu utashi wako na kuwa kiimani unahitaji nini katika masuala ya kumtumikia Mungu. Kuna baadhi ya waumini wamefilisika kwa imani hizihizi za dini na makanisa uchwara na wako kijiweni na wachungaji wanapeta. Ikumbukwe kuwa ukishatoa sadaka au kitu kwa kanisa ni ngumu kukirudisha na pia wachungaji hawa ukiishiwa wanakukimbia. Ukipata tu bahati ya kuonana nae baada ya kufilisika atakupa tuu mistari ya biblia na kukutia moyo kwa mdomo. Hawezi hata kukusaidia lolote physically.
Kwa ukweli wengine, ni vile tu hatuna taarifa za account zao bank, yaani wana pesa nyingi sana na ambazo hazina hata Bodi za kanisa zinazochunguza wala kufahamu idadi ya fedha hizo na matumizi yake.
Nyingi ya makanisa hayo yanaendeshwa kifamilia, Mara Baba Mtume au Nabii, Mama Mchungaji Mkuu au Kiongozi, watoto ushers, waweka hazina etc. So please, be carefully na nyumba yako ya ibada uliochagua. All the best.