Tofauti na ilivyotarajiwa na wengi kuwa Mch. Gwajima angejibu kashfa iliyosambaa kwa kasi magazetini kumuhusisha yeye na kesi ya Mbasha ameibuka na kudai yeye sio kama wale.
Katika ibada ya jumapili hii iliyoudhuriwa na maelfu ya watu alisikika akisema, "mimi sio kama wale, sijibu hoja kama zile, mfano ukiwa unaoga alafu chizi akachukua nguo zako na ukamkimbiza nani ataonekana chizi?" akaendelea kusema nanukuu " tatizo la watanzania ni kuwa wakisikia kitu kipya kinaanza kwao badala ya kukithamini wanakididimiza ili kisiendelee, lakini mimi sio kama wao" aliendelea kusisitiza.
Mch. Gwajima alisema, "mimi kila mwaka naenda Japan na ninawalecture wajapan, ambao pia huja hapa kanisani zaidi ya 40 kila mwaka na mwaka huu watakuja Septemba, lakini watanzania hawashtuki na kuja kujifunza wao juu Ufufuo wa wafu wengi wao wanakalia kuandika stori kwenye magazeti lakini mimi sio kama wale"
Ingawa Mch. Gwajima hakueleza moja kwa moja kuhusu tukio la mbasha na maelezo yoyote lakini maneno haya yanaonyesha kujibu hoja zinazomuhusisha yeye na tukio hilo; aliendelea kusema kuwa, "Mimi nimehubiri nchi zaidi ya 53 duniani, na nyingi za ulaya na marekani alafu mtu amekaa magomeni miaka yote anatengeneza story ya gazeti unatarajia niijibu, mimi sio kama wale nimetumwa na nina kazi natakiwa kuifanya duniani na siwezi kufa mpaka niimalize." aliendelea kusema "inawezekana mlishawaangamiza wengi kabla ya mimi, kwa kuwatungia story hizo za uongo lakini mimi sio kama wale; na mwezi huu wa nane ninaendelea na mkutano Iringa; waache waandike lakini mimi ni chombo kingine na sio kama wale"
ibada hiyo ilikatishwa na kelele za waumini wake kila muda mfupi alipokuwa akiongea. Mimi sio kama Wale.
baadhi ya Clip za ibada hii unaweza kuzipata pia youtube!!!
Picha ya Mkutano wa Mch. Josephat Gwajima mkoani Tanga...
View attachment 165507
Picha ya Mkutano wa Mch. Josephat Gwajima mkoani Tanga...