Mch. Gwajima amgomea Makonda

Mch. Gwajima amgomea Makonda

Makonda mpiga watu aende kufanya nn? pumb.f. zake huyu dogo.

Gwajima ameitwa na Mkuu wa Wilaya, labda tukisema hivyo itasound kidogo. Hata katika biblia tunafundishwa kutii mamlaka za nchi. Gwajima angeenda tu, pengine DC asingekuwa na jipya na kikao kingeisha salama
 
binafsi sidhani kama mch. Gwajima amekurupuka katika kauli yake. Nadhani kuna jambo na ndo maana amegoma kwenda kwa kamati inayoongozwa na makonda. Ikumbukwe kuwa makonda mwenyewe hana nidhamu kwani kipindi fulani aliwahi kuporomosha mvua ya matusi kwa viongozi wetu lakin hakuna jeshi la police wala kamati ya ulinzi na usalama iliyomwita kumuhoji.
Sheria za nchii zina macho kama ya kova.

kwani kova ana macho gani?....

Mbona hajakiona kinachopelekea polisi kupokwa silaha na majambazi tena wakiwa vituoni mwao na silaha wanazo...
 
Tambua kuwa makonda anasaka Sababu ya kumfukuza Gwajima pale Kawe, sasa alitoa Amri ya kuripoti akiamini kuwa Gwajima lazima ataipuuza hivyo wao kupata Sababu ya kwenda kumtoa nduki.
Kumbe hata nyie mnajua Makonda hana sababu ila anatafuta sababu ndio maana tunasema Makonda hana sababu za msingi za kumuita mtumishi wa Mungu.
 
SORRY WAHESHIMIWA...HIVI ILE SHERIA ILIYOPITISHWA JANA YA MITANDAO INAANZA KUTUMIKA LINI???...NIJUWE KABISA ILI SIKU IKIFIKA NIJITOE KWENYE ULIMWENGU WA MITANDAO NA ELECTRONICS NIRUDI ZAMA ZA S.L.P na kulamba vijikaratasi vya posta.

nahisi muda si mrefu kwa sheria zile naweza kujikuta nafungwa miaka kumi au faini milioni 50.
 
What happened to 'Tiini mamlaka zilizopo maana zimewekwa na Mwenyezi Mungu?'
 
Natumaini Makonda alimuita Gwajima kwa ajili ya ushauri kuhusu usalama wake yeye mwenyewe, Gwajima. Na midhali Gwajima anaona hahitaji msaada huo basi, mradi bwana Makonda kaisha timiza majukumu yake na likitokea la kutokea watu msiilaumu serikali!
NB: Mimi ni mfuasi mzuri wa Gwajima japokuwa naona sasa ananizidi 'KISHIMBE' kwa mbali sana. Chonde chonde, wachungaji wetu, HIVI 'VISHIMBE' MTUACHIE SISI KONDOO WENU NA MTUSAIDIE KUVISHINDA!

 
Kumbe hata nyie mnajua Makonda hana sababu ila anatafuta sababu kwa hiyo mnafikiri Makonda anafanya sawa?

Hatafuti sababu ila Gwajima ndiye anatunga sababu.Kama hana tatizo lolote kinachomfanya akatae wito wa mkuu wa wilaya ni nini? Mtu msafi haogopi kwenda polisi,mahakamani au kwa mkuu wa wilaya akiitwa.
 
Gwajima kachemka.Mkuu wa wilaya aweza futa au omba NGO fulani ifutwe au isifanye kazi wilayani kwake.hajui role ya mkuu wa wilaya kwenye NGO? ASUBIRI MUZIKI WAKE

Kawadanganje wajinga wenzako toa kifungu kinachompa mamlaka dc kufuta ngo acha ujinga wewe
 
Mchungaji wa makanisa ya kipentekoste mch. Josephat Gwajima amesema hatapoteza muda wake kwenda kumuona Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda.

Amesema barua aliyoipata toka kwa Mkuu wa Wilaya imemfedhehesha na kasema hataijibu itajibiwa na maombi ya mnyororo yanayoendelea.

Chanzo: Kutoka magazetini.

Hii ni wateule wasio jua mipaka ya kazi zao. Ni matokeo ya utwule wa kishikaji. Kesi iko polisi jamaa anamuita ofisini. Aibu sana.
 
What happened to 'Tiini mamlaka zilizopo maana zimewekwa na Mwenyezi Mungu?'

Huyu hana cha Biblia wala nini si umemsikia kwenye ile video aliyotukana pengo?yeye hajali bunge,serikali wala polisi.Anaishi kwenye dunia yake ya kufikirika ambayo haiko katika dunia hii
 
Kumtukana warioba . na kumshamburia tena jukwaani . Zawadi yake imekuwa ni kupandishwa cheo. Ya Gwajima ndo yamekuwa matusi.
 
Makonda anataka awafurahishe waliompa madaraka mpuuzi tuu eti anamwambia Gwajima kuwa unashugulikiwa kwa sababu ya LOWASSA hahahahaha mpuuzi kweli kweli makondoo
 
Hata ningekuwa Mimi nisingeenda kwa makonda mtomvu WA nidhamu kwakumpiga Jaji sinde warioba
 
Kuwa mkuu wa wilaya sio warranti ya kutenda mambo kilevi yasiyofuata sheria hata yeye yuko chini ya sheria lazima afuate utawala wa sheria rule of law.
Kwani anachomwitia kimeshajulikana mkuu, huo ndo mfumo wetu wa kiutawala DC ndio mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama katika wilaya husika na mara nyingi huwa upande wa wananchi hasa pale migogoro yoyote inapotokea maana si kila sehemu lazima polisi pekee wahusike, kuna mazingira anaingia yeye pia ili aweze kujiridhisha kwa maslahi ya umma. Anachokuambi East African Eagle ni suala la kimfumo tu na ndio maana hata wewe kama polisi wanakuonea kuna mazingira kama kosa sio la jinai au la kubabikizwa au mtu amekudhulumu alafu kuna mtu analitumia jeshi kukukandamiza kikubwa lisiwe limefika mahakamani unatakiwa ukimbilie kwa mkuu wa wilaya kama taratibu za maofisa wa jeshi wameshindwa kutatua kikubwa uwe na vielelezo. Labda tatizo DC ni Makonda
 
Gwajima kaitwa kisheria jopo la kamati ya ulinzi na usalama la wilaya lenye wajumbe kama 20 linamsubiri hajaitwa na makonda kama makonda
Nini lengo hasa la kamati hiyo wakati tayari ameshahojiwa na polisi kwa jambo hilo hilo na leo amekwenda Ostabay polisi kuendelea na mahojiano,

Huoni Makonda anataka kuingilia mamlaka ya vyombo vingine, ndio maana nasema ni lazima Makonda ajifunze kuheshimu mamlaka zingine atambue hata kama ana mamlaka ya ki dc hawezi kufanya kazi peke yake.
 
Back
Top Bottom