Mch. Gwajima amgomea Makonda

Mch. Gwajima amgomea Makonda

Mchungaji wa makanisa ya kipentekoste mch. Josephat Gwajima amesema hatapoteza muda wake kwenda kumuona Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda.

Amesema barua aliyoipata toka kwa Mkuu wa Wilaya imemfedhehesha na kasema hataijibu itajibiwa na maombi ya mnyororo yanayoendelea.

Chanzo: Kutoka magazetini.

makonda anauwezo wa kumwambia gwajima kuwa taasisi yako siitaki kwenye wilaya hiyo
 
Nini lengo hasa la kamati hiyo wakati tayari ameshahojiwa na polisi kwa jambo hilo hilo na leo amekwenda Ostabay polisi kuendelea na mahojiano,

Huoni Makonda anataka kuingilia mamlaka ya vyombo vingine, ndio maana nasema ni lazima Makonda ajifunze kuheshimu mamlaka zingine atambue hata kama ana mamlaka ya ki dc hawezi kufanya kazi peke yake.

Haingilii kila mamlaka ina mambo yake na mipaka yake.Ukiwa na duka kuna mamlaka nyingi kuna TBS wanashughulikia viwango,kuna watoa leseni ya duka inatolewa na wengine,kuna mamlaka ya chakula na dawa kama unauza vyakula,kuna Bwana Afya n.k Duka likiwa na matatizo ya kipolisi mfano umeshikwa ukiuza bidhaa za wizi haiwazuii wale wengine kushughulika na wewe kwa bidhaa zingine ambazo polisi hawakugusa TBS watakuja,watu wa leseni watakuja nk.

Wanaotoa leseni ya NGO na kusimamia matumizi yake sio polisi ni mamlaka zingine za serikali akiwemo mkuu wa wilaya.Hilo halihusiani na polisi.
 
Kwanza futa kabisa kauli yako ndug kuwa gwajima ni mchungaji wa makanisa ya kipentecoster. Si kweli kwani mim mwenyewe ni mpentecoste na wala gwajima sio mchungaji wetu wapentecoste. Mchungaji wetu na kiongoz wetu tunamjua. Hatuwez kuongozwa na gwajima anayetukana matusi hovyo kama mhun wa manzes. Hatuwez kuongozwa na gwajima anayeandikwa kwenye magazt kila siku kwa.tuhuma za usinz na uasherat. Yeye tunavyojua ni mchungaji wa kanisa la kufufua misukule na ndivyo weng wanavyojua. Hivyo kauli yako ya kumwita mchungaji wa wapentecost iishie hapohapo.
 
Mbona kamanfda Kova hana muumini wala mfuasi wake hata mmoja mbona alipomwambia Gwajima aende kuripoti kwake mbona Gwajima alienda mbio tena kwa miguu baada ya kuona foleni ya magari inamchelewesha?
Kwenye mambo ya NGO mkuu wa wilaya ana nguvu kuliko Kamanda KOVA.

Gwajima anachezea moto.Hamjui mikuu wa wilaya ni nani anadhani naye ni mmoja wa hao misukule wake.Shauri yake wale mnaomuunga mkono asiende msije kuja kupiga yowe hapa tena kulalamika

Nasema hivi Makonda hana uwezo wa kumfukuza Gwajima kinondoni, narudia tena HAWEZI
 
Kwani anachomwitia kimeshajulikana mkuu
Sababu inajulikana ni Gwajima kutumia maneno makali ya kichungaji kumuonya mchungaji mwenzake na aliyetolewa hayo maneno ameshasamehe sasa Makonda na kamati yake wanataka nini zaidi.

Suala hilo liko polisi ni amani gani anayoitafuta Makonda isiyopatikana polisi kwani polisi wamesema wameshindwa hadi kamati iundwe?
 
Kama Mch Gwajima anaitwa kwa Makonda kwa kosa la kumpinga PENGO,Wewe Makonda kwa kosa la kumkwinda Warioba na kumtusi Mzee Guninita ameitwa na nani?
 
Bora umekataa kukutana naye maana ungebinywa this time nahisi usingeweza hata kufungua macho Gwajima.... hapana chezea hii nchi na viongozi wake!
 
Ila yeye Gwajima aende tu akamsikilize Makonda,asikatae wito aende tu akamuonde huyo Makonda
 
Mchungaji wa makanisa ya kipentekoste mch. Josephat Gwajima amesema hatapoteza muda wake kwenda kumuona Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda.

Amesema barua aliyoipata toka kwa Mkuu wa Wilaya imemfedhehesha na kasema hataijibu itajibiwa na maombi ya mnyororo yanayoendelea.

Chanzo: Kutoka magazetini.

Tunasoma hata Paulo na Sila waliomba milango ya gereza iliyokuwa ina simamiwa na Warumi ikafunguka.Hivyo hata wewe Mch wangu omba sana hata milango ya katiba pandikizwa itaachia.Kuna nguvu katika maombi,maombi yanaweza kabisa yakatupa katiba ya wananchi tuachane na watawala.Hata mimi niko nyuma yako
 
Hatafuti sababu ila Gwajima ndiye anatunga sababu.Kama hana tatizo lolote kinachomfanya akatae wito wa mkuu wa wilaya ni nini? Mtu msafi haogopi kwenda polisi,mahakamani au kwa mkuu wa wilaya akiitwa.
Muda huu yuko polisi Ostabay kama Makonda anataka kumuona aende Ostabay sasa hivi otherwise ana lake jambo,

Watu hawachelei kuhisi labda Makonda anataka kumfanya kama alivyomfanya mzee Warioba maana tabia yake ya utukutu inajulikana.
 
Tunasoma hata Paulo na Sila waliomba milango ya gereza iliyokuwa ina simamiwa na Warumi ikafunguka.Hivyo hata wewe Mch wangu omba sana hata milango ya katiba pandikizwa itaachia.Kuna nguvu katika maombi,maombi yanaweza kabisa yakatupa katiba ya wananchi tuachane na watawala.Hata mimi niko nyuma yako

haaaa angalia hapo kwenye nyekundu ulichoandika.Eti uko nyuma ya gwajima? Huko nyuma ya Gwajima unafanya nini? tobaaaaa!!!
 
Binafsi sidhani kama Mch. Gwajima amekurupuka katika kauli yake. Nadhani kuna jambo na ndo maana amegoma kwenda kwa Kamati inayoongozwa na Makonda. Ikumbukwe kuwa Makonda Mwenyewe hana nidhamu kwani kipindi fulani aliwahi kuporomosha mvua ya matusi kwa viongozi wetu lakin hakuna Jeshi la Police wala Kamati ya ulinzi na usalama iliyomwita kumuhoji.
Sheria za nchii zina macho kama ya Kova.
kwa hii sentensi ya mwisho,umeua!
 
Gwajima is my hero

RAIA MWEMA limeandika kuwa hero wako anadai kufufua wafu,lakini halijawahi kumuona hata mtu mmoja aliyefufuliwa. Pitia web site yake-www.ufufuonauzima.blogspot,halafu uje hapa tena.
 
Sababu inajulikana ni Gwajima kutumia maneno makali ya kichungaji kumuonya mchungaji mwenzake na aliyetolewa hayo maneno ameshasamehe sasa Makonda na kamati yake wanataka nini zaidi.

Suala hilo liko polisi ni amani gani anayoitafuta Makonda isiyopatikana polisi kwani polisi wamesema wameshindwa hadi kamati iundwe?
Kamati ya ulinzi na usalama huwa ipo tu kwa mujibu wa sheria na moja ya mjumbe ni mkuu wa polisi wa wilaya husika. Mie nimeshawishika kuchangia si kwa kuwa Paul Makonda amemwita Gwajima bali nilikuwa naonyesha mamlaka aliyonayo mkuu wa wilaya yoyote kikubwa ashirikishe kamati yake na akiona kama yafaa kufanya hivyo pia endapo mgogoro utahusisha umma
 
Muda huu yuko polisi Ostabay kama Makonda anataka kumuona aende Ostabay sasa hivi otherwise ana lake jambo,

Watu hawachelei kuhisi labda Makonda anataka kumfanya kama alivyomfanya mzee Warioba maana tabia yake ya utukutu inajulikana.

Sheria haingalii mtu wala watu mwambie akimaliza hapo Osterbay aende kuitika wito kwa mkuu wa wilaya mheshimiwa Makonda ofisini kwake kule magomeni
 
Back
Top Bottom