Mch. Gwajima amgomea Makonda

Mch. Gwajima amgomea Makonda

Makonda aache unafiki tena unafiki hasa mlokole wa enzi zile mbona ye mwenyewe akiwaga na shida anaendaga kusali kwa Gwajima?
 
Binafsi sidhani kama Mch. Gwajima amekurupuka katika kauli yake. Nadhani kuna jambo na ndo maana amegoma kwenda kwa Kamati inayoongozwa na Makonda. Ikumbukwe kuwa Makonda Mwenyewe hana nidhamu kwani kipindi fulani aliwahi kuporomosha mvua ya matusi kwa viongozi wetu lakin hakuna Jeshi la Police wala Kamati ya ulinzi na usalama iliyomwita kumuhoji.
Sheria za nchii zina macho kama ya Kova.

Mkuu na tashwishwi ya kujua tu hapo kwenye red una maanisha nini( ana macho makali sana au ya kuona mbali sana au?)

Kuna uwezekano mkubwa Makonda aliandika barua mwenyewe na contents zake zikawa sawa na akili za Makonda tunavyozifahamu. Mtumishi wa Mungu akaona kama barua imeandikwa na mapepo wachafu hivyo nampongea kwa kuanza kwa KUKEMEA mapepo yaondoke ndo apange kuonana naye akiwa delivered.
 
Huyu Makonda anapenda awe kwenye hwadlines za magazeti kila siku. Kijana mpuuzi sana huyu.
Anapenda umaarufu wa ghafla ghafla.
 
Makonda aache unafiki tena unafiki hasa mlokole wa enzi zile mbona ye mwenyewe akiwaga na shida anaendaga kusali kwa Gwajima?

Si kila wanaofurika kwa Gwajima huenda kusali na si waumini na viongozi wote kanisa la Gwajima ni misukule ya Gwajima kuna maaskari,mashushu na watu wa kila aina wa serikali ambako wako pale kama kituo chao cha kazi kama ambavyo wengine hupangiwa kituo cha Kazi OSYERBAY POLICE N.K

Kwani hujasoma Biblia si inasema si kila anayesema Bwana,Bwana ni mkristo.Si kila aliye kanisa la ufufuo ni mtu wa kanisa la Ufufuo.Ukilitibua ndio utajua.Unadhani Gwajima alizimia polisi bure usijekuta alikuta mzee wake wa Kanisa ndie mtu anayemhoji!!!!!! na kummwagia siri zake zote.

Amani ya nchi iliyopo kuisimamia iendelee kuwepo si lelemama
 
RAIA MWEMA limeandika kuwa hero wako anadai kufufua wafu,lakini halijawahi kumuona hata mtu mmoja aliyefufuliwa. Pitia web site yake-www.ufufuonauzima.blogspot,halafu uje hapa tena.
Unajua hii ni aibu sana.....
inaonyesha ni jinsi gani watu husukumwa na
1.ushabiki
2.Depression
3.Frustrations
4.insanity
na
5.psychogenic
 
Gwajima kachemka.Mkuu wa wilaya aweza futa au omba NGO fulani ifutwe au isifanye kazi wilayani kwake.hajui role ya mkuu wa wilaya kwenye NGO? ASUBIRI MUZIKI WAKE

We unafkri anajifutia tu kisa kaamua!!!... Lazima awe ana sababu za msingi na afuate utaratibu
 
Sheria haingalii mtu wala watu mwambie akimaliza hapo Osterbay aende kuitika wito kwa mkuu wa wilaya mheshimiwa Makonda ofisini kwake kule magomeni
Naona unapenda ligi Gwajima ameshasema haendi na barua hajibu kama unauwezo kamkumbushe Makonda atumie madaraka yake.

Vile vile mkumbushe kuwa na yeye ana kesi mahakamani ya kumtukana Guninita what goes around comes around.
 
We unafkri anajifutia tu kisa kaamua!!!... Lazima awe ana sababu za msingi na afuate utaratibu

Ndio maana Makonda kwa kuzingatia taratibu kuwa utaratibu wa kwanza ni kumwita mhusika ajieleze kamwita.Akikataa wanaenda utaratibu unavyotaka sehemu ya pili hadi kieleweke.
 
Gwajima anakosea, issue kama hiyo unakaa kimya. Halafu aliyetuma hiyo barua anatafuta majibu mwenyewe ambayo yatatoa taswira halisi ya kile alichokusudia, Na hapo ndiyo kazi inaanza.
 
Naisikikia harufu kwa umbaali ya Gwajima kutulizwa kimya kimya..... mkono wa serikali....haina dini...wala urafiki..






Mchungaji wa makanisa ya kipentekoste mch. Josephat Gwajima amesema hatapoteza muda wake kwenda kumuona Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda.

Amesema barua aliyoipata toka kwa Mkuu wa Wilaya imemfedhehesha na kasema hataijibu itajibiwa na maombi ya mnyororo yanayoendelea.

Chanzo: Kutoka magazetini.
 
Si kila wanaofurika kwa Gwajima huenda kusali na si waumini na viongozi wote kanisa la Gwajima ni misukule ya Gwajima kuna maaskari,mashushu na watu wa kila aina wa serikali ambako wako pale kama kituo chao cha kazi kama ambavyo wengine hupangiwa kituo cha Kazi OSYERBAY POLICE N.K

Kwani hujasoma Biblia si inasema si kila anayesema Bwana,Bwana ni mkristo.Si kila aliye kanisa la ufufuo ni mtu wa kanisa la Ufufuo.Ukilitibua ndio utajua.Unadhani Gwajima alizimia polisi bure usijekuta alikuta mzee wake wa Kanisa ndie mtu anayemhoji!!!!!! na kummwagia siri zake zote.

Amani ya nchi iliyopo kuisimamia iendelee kuwepo si lelemama

Mkuu tukiacha ushabiki.Kulikua kuna haja ya CCM kuleta hii ajenda ya mahakama ya kadhi?

Hauoni ndio chanzo cha haya yote?
 
Mchungaji wa makanisa ya kipentekoste mch. Josephat Gwajima amesema hatapoteza muda wake kwenda kumuona Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda.

Amesema barua aliyoipata toka kwa Mkuu wa Wilaya imemfedhehesha na kasema hataijibu itajibiwa na maombi ya mnyororo yanayoendelea.

Chanzo: Kutoka magazetini.
Dogo anavimbisha kweli. Anaendesha mambo ki Uvi Vi VU!
 
Back
Top Bottom