Chapa Nalo Jr
JF-Expert Member
- Dec 8, 2010
- 7,515
- 6,489
Nilikuwa maeneo ya mahakama kuu leo mchana. Kwa kweli Le profesa ana mbwembe za kiulinzi na kiushabiki usipime. Yaani fuso limejaa wamama, halafu kuna gari ndogo kama nne zikiwa na makomandoo wa usalama kama anapita Obama vile, wanaruka kwenye gari kabla haijasimama vizuri kuchukua nafasi zao kumlinda prof.
Kwa haraka haraka ile ni gharama kubwa kuwaleta washabiki na walinzi wa aina ile. Ana hela sana Le profeseri! Hii dunia hii ni shida kwa kweli lakini tutakomaa nayo hivyo hivyo.
Sikuweza kipiga picha maana wale jamaa yawezekana wapo juu ya sheria, nimeona gari la magereza likiwapisha wapite kwanza.
Kwa haraka haraka ile ni gharama kubwa kuwaleta washabiki na walinzi wa aina ile. Ana hela sana Le profeseri! Hii dunia hii ni shida kwa kweli lakini tutakomaa nayo hivyo hivyo.
Sikuweza kipiga picha maana wale jamaa yawezekana wapo juu ya sheria, nimeona gari la magereza likiwapisha wapite kwanza.