Sakasaka Mao
JF-Expert Member
- Sep 29, 2016
- 14,938
- 20,994
Mimi huwa nasema hivii? Kitu kuwa nacho baba kuliko kutokuwa nacho, na hizo pesa zilizonunulia hayo makitu zisingelinunua zikaishia kwenye midomo ya mumiani, sasa hapo kipi bora?Tulikuwa hatulali kila kukicha kesho angalieni mawinguni, Serikali nzima ilikuwa inakesha airport kusubiri Bombardia, kila hotuba hata iwe kanisani lazima izungumzie ununuzi wa ndege, faida ya ndege, na majigambo kede kede, zile ahadi za kuifanya Dar hub of Afrika zimeishia wapi.
Sisi wachache kina Quinine, barafu, kina Zitto tuliwatahadharisha mapema, tuliwaambia MATAGA biashara ya ndege ni ngumu sana inahitaji back up kubwa ya Serikali hatukueleweka, OK, sasa midege haina route za nje imepaki tu airport mingine ikiishia kuzunguka Kibondo - Ngara kwa hasara, tumebaki kuzindua Rwandair ikibeba mizigo ya samaki Mwanza kupeleka Ulaya.
MATAGA tupeni mrejesho, Msemaji Mkuu wa Serikali lini tena tuangalie mawinguni.
Na tuseme tu kwamba hakuna lolote la maana kwa wingi wake linalofanywa na awamu ya 5 na watu wa aina yako wakaunga mkono, sijawahiona wala kusikia!
Sana sana ni kutoa mabango tu ya kusahihisha kwamba asingenunua hichi akafanya hichi!
Tumewapa kura wakapata madaraka kwa ridhaa yetu, wanayoyafanya wanafuata ilani zao walizojipangia na sisi raia tunafurahi kwa kuona wanachosema wanakitenda na kukitekeleza, nchi imebadilika pakubwa kwa muda mfupi na maendeleo ya kweli yanaonekana.
Kama hayo madege hayaleti faida leo, basi yapaki na kesho yatapata tu cha kuliingizia faida taifa.