Mbwembwe za ndege zimeishia wapi?

Mbwembwe za ndege zimeishia wapi?

Naoana post yangu imefutwa, narudia tena hivi unaweza ukafurahi baba yako kufeli, utakua mzima kweli, hizi ndege ni kwa faida ya nani? Ni yetu sote watanzania lilifanyika jambo hili kwa manufaa yetu lakini watu mnakejeli sana uwekezaji huu.

Sasa baba yako akishauriwa na watoto kuwa akodishe kwanza idadi chache za hizo mashine za angani kisha akishaona kuwa biashara inalipa basi anaweza kuamua kununua mashine hizo kidogo kidogo kadiri itavyoonekana inafaa, na akikataa ushauri na kuamua kununua hayo mavitu kwa mkupuo watoto mnafanyaje?
Baba atajitetea kuwa hakujua kuwa kuweka mayai ya kuku ktk kikapu kimoja kuna hasara & faida?
 
Hizo ndege tumeingizwa chaka, bora hayo matrillioni yangepelekwa kwenye miradi ya maji vijijini tungeweza kuokoa raia na adha kubwa za maji wanazopata..
 
Naoana post yangu imefutwa, narudia tena hivi unaweza ukafurahi baba yako kufeli, utakua mzima kweli, hizi ndege ni kwa faida ya nani? Ni yetu sote watanzania lilifanyika jambo hili kwa manufaa yetu lakini watu mnakejeli sana uwekezaji huu.
Baba akiwa anaua watoto badala ya kuwashsuri akifel ni raha sana!!! Pia hizi ndege zimenunuliwa kwa kodi za watz wote ila wapumbavu wanasema niza ccm wakaenda mbali zaidi wakaandika "hapa kazi tuu"
 
4 Julai 2020
Mbeya, Tanzania

Toka mwaka 2017 Kina Mama Inawalazimu Kusafiri Kilometa 70 kupata Huduma za Afya

wananchi walilia Maendeleo ya Watu toka mwaka 2017 wamejiongeza kwa kufanya harambee 89 lakini serikali haioni juhudi zao za kutaka huduma ya afya kwa Maendeleo ya Watu .

VIFO vya MAMA na MTOTO Wananchi Wamlilia RAIS MAGUFULI, -"Tusaidie Tumechanga Mill 102"



WANANCHI wa Kijiji cha Ifupa Wilaya ya Mbeya wamemwomba Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila kufikisha maombi yao kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli ili kuwasaidia ujenzi wa kituo cha Afya.

Source : Global TV Online
 
1 Jul 2020
Busekelo, Mbeya
Tanzania

"HUU NI UPUUZI, HATUWEZI KUVUMILIA, NAVUNJA MKATABA, HATUWEZI KUBEMBELEZANA" - RC MBEYA



MKUU wa mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila, amevunja mkataba wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Busokelo lenye kugharimu Bilion 5.2 baada ya kampuni ya Mzinga Holding Company kushindwa kukamilisha ujenzi huo kwa wakati.

Source : Global TV online
 
Kweli kabisa ndege zimeanza kuingiza hasara ya mabilioni hata kabla COVID19 hajazaliwa sasa wanataka kumtumia kama KISINGIZIO cha mradi wa yesu fake kufeli.

Endeleeni kutumia kovidi kama kivuli cha kujificha, muda utaongea tu!

Siku hizi kila kitu kovidi, hata mdeni wangu hanisumbui tena... namwambia tu hali ni mbaya si unaona!!!
 
Naoana post yangu imefutwa, narudia tena hivi unaweza ukafurahi baba yako kufeli, utakua mzima kweli, hizi ndege ni kwa faida ya nani? Ni yetu sote watanzania lilifanyika jambo hili kwa manufaa yetu lakini watu mnakejeli sana uwekezaji huu.
Tukubali au tukatae, uwekezaji huu wa kununua midege kwa Cash ulikuwa wa kiboya sana
 
Back
Top Bottom