Mbunge wangu Mwigulu umeshindwa kabisa!

Hata Magufuli mwenyewe haya anayoyafanya Chato,hakuyafanya kipindi kile alichokuwa mbunge wa Chato,amesubiri mpaka amekuwa Rais ndio ameanza kuyafanya kwa kuwa kufanya kile na kile hasa kinachohusu matumizi ya pesa si kazi ya mbunge ni kazi ya serekali kupitia kodi za wananchi, kazi ya mbunge ni kukusanya kero na mahitaji ya wananchi katika jimbo lake na kuipelekea serekali yenye wajibu wa kuwahudumia wananchi wake.

Sasa kama kila mbunge atakuwa anafanya mambo yote kwa kutumia fedha zake, kazi ya serekali itakuwa ni ipi kwa kuwa kazi zote zitakuwa zimefanywa na wabunge wa majimbo kwa kutumia fedha zao?, kama ni hivyo basi hata maana ya kuwa na serekali haitakuwepo.

Ndio maana sisi wengine tunasema huo uwanja wa ndege wa Chato ni matumizi mabovu ya pesa za umma, kwani atakapotoka madarakani ndio itakuwa mwisho wa huo uwanja. Miradi mingi iliyoanzishwa na viongozi kutokana na nafasi zao kimadaraka, mingi ya miradi au biashara hizo za upendeleo, husuasia ama hata huanguka pindi tu viongozi hao wakitoka kwenye nafasi hizo.
 
Pascal Mayalla, Tatizo Mwigulu akiwekewa mizengwe CCM anaweza kukimbilia wapi wakati hakuna ruhusa ya mgombea binafsi?

Shida ya Mwigulu wakati wa madaraka vyama vingine alivifanya adui na kuviona takataka nani anaweza kumpa nafasi hata kama anao wapiga kura wa kutosha?

Sent using Jamii Forums mobile app
Aliwahi kuchana bajeti mbadala ya wapinzani bungeni maccm wenzake wakamshangilia sana akajiona boonge moja la genius kumbe ugoro mtupu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
in contrary wapinzani kibao wanapita ubunge bila magufuli...

Magu ana bahati kuwa na big name

Sent using Jamii Forums mobile app

Nitajie mpinzani yoyote aliyepata ubunge ama udiwani kwenye chaguzi yoyote iliyofanyika toka Magufuli amekuwa rais. Chini yake ndio tumeona kwa macho yetu mabox ya kura yakitolewa vituoni mbele ya polisi na wasimamizi wa uchaguzi kwenda kujazwa kura za ccm, kisha msimamizi wa uchaguzi kutangaza mshindi aliyepatikana katika mazingira hayo! Chini ya utawala wake ndio tumeshuhudia ofisi zikifungwa ili wapinzani wasirejeshe fomu ofisini ili ccm wapite bila kupingwa. Chini ya utawala wake, ndio tumeona uchaguzi wa nchi nzima viongozi wakipatikana bila kupigiwa kura, na yote ni maagizo yenye baraka zake. Kibaya zaidi ushindi huo wa mezani, umeshangiliwa kuliko hata chaguzi ambazo ccm walikuwa wakishinda kwa kura kabla yake.
 
Kama unataka kugombea Iramba, gombea tuu kwa kusema utafanya nini, hakuna jimbo lolote ni mali ya mtu, huna haja ya kutumia jina la Magufuli kumtishia Mwigulu, Mbunge aliyepo ni Mwigulu na ni Mbunge wa jimbo la Iramba na amechaguliwa na wana Iramba na sio Mbunge wa jimbo la Magufuli, hivyo hivyo vitisho vya kuwa Magufuli atamkata, usitishe watu, wanaochagua ni wana Iramba, wakijiona kama bado wanamuhitaji Mwigulu wao na Magufuli kweli akamkata, its up to Wanairamba kumkubali huyo atakayepitishwa au kumchukua Mwigulu wao na kumrudisha kupitia chama kingine, hivyo ndivyo wapinzani wengi waliingia bungeni toka Dr. Slaa hadi Mwambe.

P
Ni mbumbumbu tu huyu hana lolote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wangalau ushauri huu una maana. Tatizo linakuja, je ni mtu competent kuweza kupata nafasi kwenye mashirika ya kimataifa? Kumbuka hapa nchini aliweza kupata nafasi za juu kama fadhila kwa mchango wake kwenye uga wa kisiasa, je akienda sehemu wanakohitaji uwezo anaweza kutoboa?
Education wise he is brilliant, ana 1st class ya Economics from UDSM na aliajiriwa BOT.

P
 
Ni mbumbumbu tu huyu hana lolote

Sent using Jamii Forums mobile app
No Mwigulu sio mbumbumbu ni kichwa sana
P
 
Mkuu Mnambua, kwanza mimi sio mtabiri, mimi ni just a commentator,

Kazi ya kuwataja wagombea wa uchaguzi wa 2015 tuliianza toka 2011 kama ambavyo kazi ya kuwataja wagombea wa 2025 turaianza 2021.

kwenye wagombea wote zaidi ya 40 wa CCM, niliwagawa katika mafungu 10 na kutoa list yangu ya 10 bora katika kila fungu

Wengi Magufuli walimjua 2015 baada ya kuteuliwa, angalia akina sisi tulimtaja lini


Huu sio utabiri ni trends readings, usomaji mielekeo. Mfano mzuri ni mwaka huu, huu ni mwaka wa uchaguzi na Tanzania tuna vyama vingi, mwelekeo unaelekeza upinzani unakwenda kuwa dumped totally, Bunge lijalo ni Bunge la CCM predominantly. Hili likitokea utasema ni utabiri?. No sio utabiri ni mielekeo.
P

Paskali hapa ni kama unacheza tu na maneno, sio mara moja au 2 umekuwa ukileta hizo trend readings zako kama utabiri. Hilo la kwamba uchaguzi wa mwaka huu wapinzani wanaenda kuwa dumped umelichomeka ili kuupa utetezi wako nguvu.
 
Wewe ni Mchumi na siku zote wachumi huelezea uhalisia wa mambo kwa namba. Wataalamu wanadai "namba haziongopi".

Mheshimiwa umekosa ujasiri wa kusema mambo ambayo umeifanyia Iramba kwa sababu hamna ulichofanya ambacho unaweza kujivunia.

Au unataka kuongelea kwa mfano shule yako ya Kata yaani Kyengege kutoka nafasi ya 15 kimkoa Mwaka juzi na kufikia nafasi ya 8 kwa Mwaka jana hayo ni mafanikio?

Viko wapi visima vya maji ulivyoahidi katika vijiji mbalimbali vya Iramba, umeshinikiza vipi Mradi wa umeme wa REA kukamilishwa pale ulipokomea?

Ukiacha Kituo cha Afya cha Kinampanda wapi kwingine unapojivunia uliacha?

Ukweli ulikazania siasa za Kitaifa za kutaka uwe Rais - wapi sasa maendeleo uyaonayo yameletwa na siasa zako za Kitaifa zaidi ya kuzidi kunyongonyezwa tu wewe na Nape na Januari?

Na inadaiwa umewekewa TISS wa kumwaga tu hadi chumbani kwako!

Kikubwa tumia akili achia ngazi mapema, tafuta kitu bora zaidi cha kufanya ili kuepukana na Rais Magufuli kwenye siasa kwa kuwa kwa vyovyote anavyokuchulia wewe ni threat kwake atahakikisha anakukata juu kwa juu na Ubunge hutopata!
Achana nae alikuwa na jeuri sana alipokuwa anavaa mabendera anakula alichopanda
 
Education wise he is brilliant, ana 1st class ya Economics from UDSM na aliajiriwa BOT.

P

Paskali nimetumia neno competent sio kwa bahati mbaya, najua kuna tofauti ya kupata first class ya hapo UDSM tena wakati ukiwa waziri, na first class ukiwa huna madaraka. Aliajiriwa BoT kweli, lakini hakuwa gavana bali alikuwa staff wa kawaida. Na isitoshe katika mazingira ya hizi taasisi zetu ambazo watu wanapata kazi kwa mbeleko huwezi kupima uwezo wa mtu kwa uhalisia. Nimesema competent kwenye taasisi za kimataifa, nikijua fika huko uwezo ndio nguzo halisi kuliko hizi blabla za hapa nyumbani. Huyo Mwigulu ana uwezo huo au ana vyeti tu?
 
Sawa Mkuu Paskali. Ingawa unakataa unachoandika sio utabiri lkn kwa uelewa wangu naona ni utabiri.
Mtabiri ni sheikh Yahaya, watabiri wanatumia nyota, au ramli etc, mimi ni msoma trends, kusoma trends ni kuangalia tuu mielekeo, mfano leo ni January uchaguzi ni October, nikikuambia kuna uwezekano hakuna hata Mbunge mmoja wa Chedema atakayerudi Bungeni, ikitokea utasema ni utabiri?. No sio utabiri ni trends tuu.

P
 
Nadhana mtoa mada jibu analo.
Mkuu wa Inchi hawako vizuri na Mbunge wetu.
Mkuu wa Inchi ndiye mwenye mamlaka ya mwisho ya Kiserikali kuhusu kuendeleza miradi ya maendeleo.
Mbunge Mwigulu ana conflict of interest na Mkuu wa Inchi kwa sababu Mwigulu bado anautaka Urais kama sio 2020 basi 2025.
Bado kuna maandishi yaliyoandikwa juu ya majabali mengi kando kando ya bara bara za Singida Arusha na Singida Dar kuwa Mwigulu ni Rais 2015. Mwandiko unafanana kwenye majabali yote na hadi leo takriban miaka 4 hayajafutwa.
Kwenye BASI la Timu ya Singida United kwa nyuma kuna picha kubwa ya Mwigulu ambayo inamtangaza Inchi nzima bila kuwekwa wazi kuwa yeye ni mfadhili au mlezi.
Wengi wanatafasiri kuwa hizi nazo ni Kampeini za kuutafuta Urais 2025.
Katika haya yote tumwombee afanikishe ndoto yake ya kuupata Urais ili mradi havunji kanuni na Sheria za Inchi.
Itakuwa ni Heshima kubwa kwa Wana Singida kama Rais atakuwa Mwigulu kwa mwaka 2025.
Kwa mwaka 2020 aungane na Rais wetu wa sasa katika kumfanyia kampeini ili ashinde kwa kishindo katika nafasi yake ya kikatiba ya kugombea Urais kwa awamu ya pili.
 
Ndio maana sisi wengine tunasema huo uwanja wa ndege wa Chato ni matumizi mabovu ya pesa za umma, kwani atakapotoka madarakani ndio itakuwa mwisho wa huo uwanja. Miradi mingi iliyoanzishwa na viongozi kutokana na nafasi zao kimadaraka, mingi ya miradi au biashara hizo za upendeleo, husuasia ama hata huanguka pindi tu viongozi hao wakitoka kwenye nafasi hizo.
Kuhusu uwanja wa Chato, I'd like to disagree, kinachofanyika sasa baada ya uwanja ni kuweka sustainability strategies ili kuwa sustainable, utalii ni moja ya mipango hiyo.

Mimi naunga mkono uwanja huu.
P
 
No Mwigulu sio mbumbumbu ni kichwa sana
P

Paskali bana huwa unanichekesha sana, kichwa wa nini, alikuwa mfadhili sijui mdhamini wa Singida United, wakati akiwa waziri hiyo timu ilikuwa vizuri, kapoteza uwaziri timu iko hoi! Yeye kama mchumi anashindajwe kuifanya timu isimame kama timu kwa kutumia elimu yake ya uchumi, bali timu inafanya vizuri anapokuwa tu na madaraka!? Hapa ndio hoja yangu ya kuwa competent inaposimama. Hiyo elimu yake ni kwa faida yake na mkewe. Mimi nimeishia darasa la saba la ukweli, lakini nipe milioni 200, kisha mpe Mwigulu 2b, kisha njoo baada ya miaka miwili uchukue mrejesho. Ili mradi wote tuwe kwenye uwanja sawa wa biashara.
 
Watu wanampigia kelele Zitto Kabwe haonekani jimboni kwake, wanawasahau wabunge wa CCM 90% walijazana Dodoma na Dar es Salaam na kwenye majimbo yao hawaonekani kabisa kusaidia changamoto na kero za wananchi wao.

Hasa waliopata "VYEO" kwenye serikali hii. Ila muda ndio ushafika wa "MAPAMBANO".
Kwa hiyo Zitto amewaiga hao 90% ya wabunge wa CCM wasioonekana majimboni kwao?

Vichwa vya hawa vijana wa ufipa nadhani ubongo wao umechanywa na maji ya ndimu. Huwezi kuhalalisha uhalifu wako eti kwa sababu tu na mwenzio anafanya aina hiyo hiyo ya uhalifu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuhusu uwanja wa Chato, I'd like to disagree, kinachofanyika sasa baada ya uwanja ni kuweka sustainability strategies ili kuwa sustainable, utalii ni moja ya mipango hiyo.

Mimi naunga mkono uwanja huu.
P

Paskali inaonekana unazungumza jambo usilolijua au unazungumza kwa matamanio. Jaribu kufanya utafiti wa mapato wa hivyo vivutio vyetu vya utalii kisha utakuja na jibu sahihi badala ya matamanio. Kuwa na vivutio vya utalii ni jambo moja, kuwa na watalii ni jambo jingine. Kama kuwa na vivutio vya utalii ni hoja, Kenya au Rwanda wasingetusogelea kwenye mapato ya utalii. Kama mbuga ya utalii ndio inachangia kuwa na uwanja wa ndege wa 39b, basi huko Selous kulitakiwa kuwa na uwanja wa ndege wa 300b. Paskali tuombe uzima 2030 tuwe hai, miaka mitano baada ya Magufuli kutoka madarakani, iwapo atachaguliwa tena mitano hii, kisha unipe mrejesho wa kitakachokuwa kinaendelea huko Chato.
 
Wewe ni Mchumi na siku zote wachumi huelezea uhalisia wa mambo kwa namba. Wataalamu wanadai "namba haziongopi".

Mheshimiwa umekosa ujasiri wa kusema mambo ambayo umeifanyia Iramba kwa sababu hamna ulichofanya ambacho unaweza kujivunia.

Au unataka kuongelea kwa mfano shule yako ya Kata yaani Kyengege kutoka nafasi ya 15 kimkoa Mwaka juzi na kufikia nafasi ya 8 kwa Mwaka jana hayo ni mafanikio?

Viko wapi visima vya maji ulivyoahidi katika vijiji mbalimbali vya Iramba, umeshinikiza vipi Mradi wa umeme wa REA kukamilishwa pale ulipokomea?

Ukiacha Kituo cha Afya cha Kinampanda wapi kwingine unapojivunia uliacha?

Ukweli ulikazania siasa za Kitaifa za kutaka uwe Rais - wapi sasa maendeleo uyaonayo yameletwa na siasa zako za Kitaifa zaidi ya kuzidi kunyongonyezwa tu wewe na Nape na Januari?

Na inadaiwa umewekewa TISS wa kumwaga tu hadi chumbani kwako!

Kikubwa tumia akili achia ngazi mapema, tafuta kitu bora zaidi cha kufanya ili kuepukana na Rais Magufuli kwenye siasa kwa kuwa kwa vyovyote anavyokuchulia wewe ni threat kwake atahakikisha anakukata juu kwa juu na Ubunge hutopata!
Wamekazania kuyanyima miradi ya maendeleo majimbo ya upinzani.

Hahahaa karma ni hap hapa.

Akina mwigulu hawana uwezo wowote wa kiuongozi wanabebana tu ndani ya chama.
 
Kwenye hili la karma, naomba kumtetea Mwigulu.

Kuna viongozi wengi wametumbuliwa katika hao wanaotumbuliwa kuna baadhi kweli ni majipu na sababu za kutumbuliwa huwa zinawekwa. Lakini wengine wanatumbuliwa tuu kwa sababu nyingine na sio majipu, hawa wanaotumbuliwa ambao sio majipu, sababu za kutumbuliwa kwao huwa hazitolewi, Mwingulu Mchemba ni mmoja wa watu hawa, sasa kwa mujibu wa taarifa za koridoni zilizopelekea Mwigulu kutumbuliwa, naomba uniamini mimi, karma haitamhusu!.

Ukipitia bandiko hili, kuna kitu nilikisema kumhusu Mwigulu kabla hajatumbuliwa kilichopelekea akatumbuliwa ila huyu sio jipu!.

P
Kwahiyo Pasco unataka kusemaje hapa??
 
Chakaza,


Mkuu wala usiseme hivyo, kama cdm walimpokea Lowassa usishangae Mwigulu akiwa mgombea wa cdm. Hivyi vyama vyetu vya upinzani navyo havina msimamo ambao unaweza kuwaamini. Lakini piga ua, Mwigulu yuko radhi adhalilike akiwa ccm, maana anajua fika hana uwezo wa siasa za ushindani nje ya mbeleko ya vyombo vya dola. Na yeye ndio amekuwa akishiriki na kupanga chaguzi za dhuluma, hivyo anajua fika akitoka ccm dhuluma alizokuwa anashiriki zitamfika hata yeye. Atakachofanya ni kuweka sura ya huruma ili apewe hata ukuu wa mkoa. Mwigulu ni baadhi ya viongozi wa ccm walioendesha siasa za chafu sana ndani ya nchi hii.
tindo
Upumbavu uliojitokeza wakati ule kuanzia Lowassa na wafuasi wake na maumivu yake sidhani kama kuna mtu ndani ya Chadema anaweza kuurudia na hata kuuzungumzia tena.
Lakini yote in yote, hakuna kuzungumzia sijui uchaguzi utakuaje au nini, habari iwe tume huru ya uchaguzi tuu. Viongozi wasipotumia nguvu zao kwa hiyo agenda nasi kuwaunga mkono basi nchi imekwisha!
 
Back
Top Bottom