Tindo
JF-Expert Member
- Sep 28, 2011
- 58,998
- 103,386
Hata Magufuli mwenyewe haya anayoyafanya Chato,hakuyafanya kipindi kile alichokuwa mbunge wa Chato,amesubiri mpaka amekuwa Rais ndio ameanza kuyafanya kwa kuwa kufanya kile na kile hasa kinachohusu matumizi ya pesa si kazi ya mbunge ni kazi ya serekali kupitia kodi za wananchi, kazi ya mbunge ni kukusanya kero na mahitaji ya wananchi katika jimbo lake na kuipelekea serekali yenye wajibu wa kuwahudumia wananchi wake.
Sasa kama kila mbunge atakuwa anafanya mambo yote kwa kutumia fedha zake, kazi ya serekali itakuwa ni ipi kwa kuwa kazi zote zitakuwa zimefanywa na wabunge wa majimbo kwa kutumia fedha zao?, kama ni hivyo basi hata maana ya kuwa na serekali haitakuwepo.
Ndio maana sisi wengine tunasema huo uwanja wa ndege wa Chato ni matumizi mabovu ya pesa za umma, kwani atakapotoka madarakani ndio itakuwa mwisho wa huo uwanja. Miradi mingi iliyoanzishwa na viongozi kutokana na nafasi zao kimadaraka, mingi ya miradi au biashara hizo za upendeleo, husuasia ama hata huanguka pindi tu viongozi hao wakitoka kwenye nafasi hizo.