Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
WAITARA NAONYWA KWA UTOVU WA NIDHAMU, ATAKIWA KUJIREKEBISHA
Mbunge wa Tarime Vijijini, Mwita Waitara amepewa onyo baada ya kuonesha vitendo vya utovu wa nidhamu kwa kukiuka Kakuni ya Bunge 83: 1 (c).
Waitara alitoka nje ya Ukumbi wa Bunge akionesha kutoridhishwa na majibu ya Serikali kuhusu Wananchi wanaodai fidia maeneo ya Mgodi wa Barrick North Mara Komarera, Nyamichele na Murwambe.
Naibu Spika, Mussa Azan Zungu amesema “Hii ni mara ya pili kwa Waitara kukiuka kanuni, hivyo si vitendo vya Kibunge, humu Bungeni hata ukihama kwenye kiti chako kwenda kiti kingine ni kosa, inaitwa ‘Kutangatanga ndani ya Bunge’.”