PreGE2025 Mbunge Sophia Mwakagenda aitema CHADEMA, Ajiunga rasmi na CCM

PreGE2025 Mbunge Sophia Mwakagenda aitema CHADEMA, Ajiunga rasmi na CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya, Sophia Mwakagenda, ametangaza kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM), akisema uamuzi huo unalenga kuendeleza jitihada zake za kuwatumikia wananchi kwa ufanisi zaidi.

Akizungumza mbele ya mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Bulyaga iliyopo Tukuyu, mkoani Mbeya, ametumia nafasi yake kuwaaga wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), akikipongeza kwa kumlea na kumjenga kisiasa tangu aanze safari yake ya uongozi.

“Ninashukuru CHADEMA kwa malezi na mafunzo ya kisiasa niliyoyapata, kuanzia saa tano asubuhi ya Juni 28, 2025, nitajiunga rasmi na CCM ili kuendelea kuhudumia wananchi,” amesema Sophia.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Hata hivyo, Mwakagenda bado hajafichua kama atawania Ubunge wa Jimbo la Rungwe katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Mwakagenda ni miongoni mwa wabunge 19 wa Viti Maalum waliovuliwa uanachama na CHADEMA. Katika uchaguzi wa mwaka 2020, aliwania Ubunge wa Jimbo la Rungwe kupitia tiketi ya CHADEMA, akichuana na mbunge wa sasa, Antony Mwantona wa Chama cha Mapinduzi (CCM)
Sasa ndiyo nasema Rungwe kuna uwezekano wa kupata mbunge wa kweli katika miaka mingi.
 
Bunge linavunjwa tarehe 27 Juni, kesho yake anajiunga rasmi na CCM. Angeweza tu kusema kuwa hatagombea tena na mara baada ya kuvunjwa Bunge ndio akajiunga na CCM. Anafanya hivi kuwaonyesha CDM kuwa hamna kitu wanachoweza kumfanya. Lakini pengine bila kujua anashusha heshima ya Bunge.

Amandla...
Lazima atimize mapatano na CCM hakuna namna kwani utamfanya nini?
 
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya, Sophia Mwakagenda, ametangaza kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM), akisema uamuzi huo unalenga kuendeleza jitihada zake za kuwatumikia wananchi kwa ufanisi zaidi.

Akizungumza mbele ya mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Bulyaga iliyopo Tukuyu, mkoani Mbeya, ametumia nafasi yake kuwaaga wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), akikipongeza kwa kumlea na kumjenga kisiasa tangu aanze safari yake ya uongozi.

“Ninashukuru CHADEMA kwa malezi na mafunzo ya kisiasa niliyoyapata, kuanzia saa tano asubuhi ya Juni 28, 2025, nitajiunga rasmi na CCM ili kuendelea kuhudumia wananchi,” amesema Sophia.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Hata hivyo, Mwakagenda bado hajafichua kama atawania Ubunge wa Jimbo la Rungwe katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Mwakagenda ni miongoni mwa wabunge 19 wa Viti Maalum waliovuliwa uanachama na CHADEMA. Katika uchaguzi wa mwaka 2020, aliwania Ubunge wa Jimbo la Rungwe kupitia tiketi ya CHADEMA, akichuana na mbunge wa sasa, Antony Mwantona wa Chama cha Mapinduzi (CCM)
Karibu sana ndugu mbunge
 
Bunge linavunjwa tarehe 27 Juni, kesho yake anajiunga rasmi na CCM. Angeweza tu kusema kuwa hatagombea tena na mara baada ya kuvunjwa Bunge ndio akajiunga na CCM. Anafanya hivi kuwaonyesha CDM kuwa hamna kitu wanachoweza kumfanya. Lakini pengine bila kujua anashusha heshima ya Bunge.

Amandla...
Huyu na wenzake walishafukuzwa Chadema ila bado waliendelea kubaki bungeni mpaka sasa.

Kiufupi bila kuwa mwanachama wa chama chochote unaweza kuwa mbunge kama wenye nchi wakitaka.
 
Anajua upande ule una mwanamke papa basi anahisi atabebwa na mwanamke mwenzake....asahau😂, COVID 19 si ndio Hawa....watoto sio ridhiki😋
 
Karibu sana CCM.Lakini kumbuka unatakiwa utulie ujifunze miiko,maadili na mapokeo ya chama kwanza ndipo uanze kufurukuta.
Muulize Upendo Peneza alipo na anafanya Nini.
 
Huyu na wenzake walishafukuzwa Chadema ila bado waliendelea kubaki bungeni mpaka sasa.

Kiufupi bila kuwa mwanachama wa chama chochote unaweza kuwa mbunge kama wenye nchi wakitaka.
Ni kweli.
Amandla...
 
Back
Top Bottom