Mbunge Mussa Khamis Silima afariki Dunia

Mbunge Mussa Khamis Silima afariki Dunia

Spika wa Bunge Mh. Anna Makinda, ametangaza muda huu kuwa Mh. Mbunge Silima aliyepata ajali mbaya ya gari juzi na kumpoteza mkewe. Amefariki muda mfupi pale Muhimbili. Bunge limeahirishwa mpaka kesho kwa maombolezo. Poleni wanafamili wote na Bunge zima kwa ujumla wake.

Mkuu, taarifa hii imeshafika...
Nawatakia pole wafiwa wote.
 
RIP mheshimiwa, nilidhani ni wa huku bara nianze kushangilia jimbo lingine kuwa wazi kwa chadema.

Kwa nini msubiri ajali ili mshangilie? Si CHADEMA ina nguvu ya umma, waueni tu mchukue hayo majimbo yenu.
 
Ajali za barabarani ni janga la kitaifa. Kila siku, kila wiki, kila mwezi na kila mwaka watanzania wanapotea kwa ajali barabarani. Je wangapi wafe au nani afe ili hatua zichukuliwe?
 
RIP mheshimiwa, nilidhani ni wa huku bara nianze kushangilia jimbo lingine kuwa wazi kwa chadema.

Kifo si cha kushangiliwa kwa sababu ya jimbo ndugu yangu!

Mungu awalaze pema peponi waliofariki na awape moyo wa subira ndugu zao waliofariki.
 
Innalillahi wainnailah rajiuna, Mungu aiweke roho ya marehemu panapostahili
 
kwenye mambo ya kibinadamu kuwa makini na uwe na utu.Familia imepoteza wazazi kwa muda mfupi mno.
 
Mungu akukirimie kutokana na matendo yako,Pole familia yake kwa kupoteza baba,Ndugu na jamaa kwa kumpoteza mpendwa wenu,pia watanzania kwa kupoteza mwakilishi wetu mjengoni..Hatunaye tena Ndugu Mussa Khamis Silima.
 
Its a tragedy in less than a week watu 3 wa familia moja wanapoteza maisha! walipata ajali wakitokea kumzika kaka wa mke wa marehemu Mhe. Mussa Khamis Silima. "Mungu azilaze Roho za marehemu wote mahali pema peponi. Amina!"
 
RIP, wife then him, watoto sijui wako katika hali gani. Poleni sana wanandugu kweli duniani tunapita kama ndivyo kwanini kwa msiba huu nyinyi wanasiasa msikumbushwe kwamba hii ni nchi yetu wote, tuijenge pamoja na tuifaidi pamoja na Mungu atuchukuapo basi tuhuzunike pamoja? Poleni sana familia!
 
Innalillahi wainnailah rajiuna, Mungu amsamehe alipokosea na ampe makazi mema .Amin
 
tumia busara na siyo masaburi

Nyie msiotumia Masaburi kwa nini mnasubiri ajali ndio mshangilie vifo vya wabunge wa CCM ili CHADEMA ichukue hayo majimbo badala ya kutumia nguvu yenu ya umma kuwaua hao wabunge ili myachukue hayo majimbo?
 
Back
Top Bottom