Mbunge Mussa Khamis Silima afariki Dunia

Mbunge Mussa Khamis Silima afariki Dunia

inasikitisha lakini hakuna la kufanya,Binadamu hapa duniani sio kwetu,sote tutaondoka kwa zamu,kila nafsi iliyo zaliwa itaonja mauti,sawasawa na kuku duniani si nyingi, bwana alitoa na bwana ametwaa jina la bwana libarikiwe poleni sana wana familia kwa ujumla.
 
RIP Silima

Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi (CCM), Maalim Mussa Silima, amepata ajali na mkewe, Mwanaheri Alli, amefariki dunia baada ya gari walilokuwa wamepanda kugongana na gari ya mizigo eneo la Nzuguni mkoani Dodoma.

Mbunge wa Jimbo la Uzini, Muhammed Seif Khatib, alisema ajali hiyo ilitokea juzi saa 11:00 jioni na marehemu alifariki dunia muda mfupi baada ya kufikishwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.

Alisema Mbunge huyo ambaye pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Uzini, alikuwa akitokea jijini Dar es Salaam akiwa amefuatana na mkewe akiwahi kikao cha Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilichokuwa kifanyike jana pamoja na kikao cha Bunge la Jamhuri ya Muungano.

"Marehemu anatarajiwa kuzikwa katika kijiji cha Kiboje Mkoa wa Kusini Unguja," alisema Khatib na kuongeza kuwa Mwakilishi huyo alisafirishwa kwa ndege kwa matibabu zaidi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) Kitengo cha Mifupa (MOI).

Alisema baada ya kutibiwa katika Hospitali ya Dodoma, madaktari walishauri ahamishiwe MNH kutokana na maumivu aliyoyapata sehemu ya uti wa mgongo na paja.

Alisema gari ya mbunge huyo ilikuwa ikiendeshwa na dereva wake, Chizani Sembonga, alipokuwa akijaribu kuikwepa gari iliyokuwa mbele yake alikutana na gari lingine na kugongana nalo.

"Ujumbe wa wabunge tisa umeteuliwa kuwakilisha Bunge katika mazishi wakiongozwa na aliyekuwa Mbunge wa Dole, Juma Nhunga," alisema Khatib. Mwakilishi huyo alichaguliwa katika Uchaguzi Mkuu uliopita kwa mara ya kwanza baada ya kumuangusha katika kura za maoni aliyekuwa Naibu Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi, Tafana Kassim Mzee.
Nawapa pole wana ccm wote, ndugu pamoja na wote waliouguswa na msiba huo. Ushauri wangu kwa madereva ni kuwa waangalifu wanapokuwa wanaendesha magari ili kuzuia hasara kama hizi ambazo sio kwa familia tu bali kwa taifa kwa ujumla.
Aidha waheshimiwa wetu hawa wajitahidi kuajiri madereva wenye sifa na uzoefu wa kutosha, pamoja na kuwalipa vizuri ili wafanye kazi zao kwa umakini. Madereva pia wa viongozi waelewe kuwa wamepewa dhamana kubwa wanapowaendesha viongozi hivyo umakini wa hali ya juu unahitajika ili kuzuia mambo kama haya, hili pia linahitajika kuzingatiwa na madereva wote.
Mungu alaze roho za marehemu pema peponi
 
RIP, God take care of their DAUGHTERS and SONS. Give them strength to outstand the pains.
 
RIP mheshimiwa, nilidhani ni wa huku bara nianze kushangilia jimbo lingine kuwa wazi kwa chadema.
<br />
<br />
acha hzo wewe,una fikra potofu kufurahia kifo cha mwenzako hakina justification panzi wewe
 
Kwa kweli hili ni pigo kwa wanafamilia, watu wawili kufa katika kipindi kifupi. Poleni sana wafiwa na mungu awarehemu waja wake.

Nadhani huyu Mh Silima ni ndugu wa Naibu Waziri wa Fedha, Pereira Silima. very sad.

Very sad.
Si wawili pekee, naamini huyo mbunge na mkewe walikuwa wanatoka kwenye mazishi ya kaka yake mbunge. That being said, hiyo familia imepoteza memba wake 3 within a week.
Pole sana wana ndugu, wabunge pamoja na wakazi wa Uzini.
 
Kuna aliyemtaja kibonde Nasikia kUTAPIKA, Kibonde always hana analofikiri la maendeleo kwa nchi hii?????????
 
Poleni sana watz,kilichonisikitisha zaidi ni aina ya gari aliyokuwa anatembelea,ni kama corola ltd.Mi nadhani ingekuwa prado/vx au station wagon yoyote, angeweza kunusurika..anyway ni mtazamo tu.
 
Poleni wazanzibar kwa kufiwa na mwakilishi pamoja na mkewe, Mungu awarehemu marehemu wote
 
Back
Top Bottom