Mbunge Godbless Lema akamatwa na polisi

Mbunge Godbless Lema akamatwa na polisi

Du, wewe mzito wa kuelewa au king'ang'anizi cha kutokukubali ukweli.

Katika mengi niliyoandika na kushauri, ni hilo la kushindwa kwa UKAWA kushawishi Watanzania na kaulimbiu ya 'mabadiliko Lowasa, Lowasa mabadiliko' pamoja na kuzungusha mikono, hadi unadai ushahidi!

Ushahidi ni asilimia za kura za Rais na Wabunge na Madiwani ilizopata CCM kwa kauli mbiu ya 'hapa kazitu' dhidi ya vyama 4 vinavyounda UKAWA.

sawa usemacho, ila ni kwa tume ipi ya uchaguzi?
 
Niliposikia kuwa Lema kakamatwa sijahuzunika wala kushangaa bali nimemwambia rafiki yangu kuwa polisi wameamua tena kumpandisha chart kamanda Lema kwa speed ile ile ya 2011. Kadiri mwanasiasa anayeonekana kutetea umma anavyokamatwa na kunyanyaswa na serikali au polisi awe na kosa au asiwe nalo ndivyo anaendelea kuwa na wafuasi wengi nyuma yake kuliko wapinzani wake. Mwisho wa siku ccm Arusha na wagombea wao wataendelea kuangukia pua daima.
 
Sina uhakika kama hii serikali inajiamini. Na moja ya kanuni za uongozi ni kujiamini. Ila kujiamini ni zao la kujua kwamba upo hapo ulipo kwa haki na stahili. Nahisi kuna kitu kinawasuta kwenye nafsi zao.
 
sawa usemacho, ila ni kwa tume ipi ya uchaguzi?
Kushiriki kwa vyama vyote vya siasa chini ya "hiyo Tume" vilikubali uhalali wake na hivyo basi matokeo iliyoyatangaza. Ni Tume hiyo hiyo iliyotangaza, matokeo ya majimbo vyama vya upinzani yalishinda.
 
Huwezi mnyamazisha mtu kwa kumuweka mahabusu hata siku moja labda awe hajawahi kaa kwa sisi wengine ambao tumeingia huko toka tukiwa darasa la 5 si kwa kushangaa..watafute suluhisho
sasa si uingie uandamane mnatusumbua humu mitandaoni......
 
Polisi wanawapa umaarufu sana wanasiasa wa Chadema, Chadema wanakitangaza kirahisi sana chama chao wakisaidiwa na polisi,kila siku Chadema inasikika kwenye vyombo vya habari wakisaidiwa napolisi.
Polisi imekuwa kama idara ya uenezi ya Chadema.
 
Ni kweli, kumbe mmegundua ee! Sept 1 jitokezeni wengi ili ule msemo "kifo cha wengi ..." utimie, maana mtakavolabuliwa, hadi nawaonea huruma.

Aisee, unadhani polisi wanaoua wao wanakaa angani? ebu jaribu kua na akili kidogo.
 
Atakuwa kahusika. Maana inaonekana chadema wamehusika ktk kutafuta sare ili askari wao fake waue waandamanaji na baadaye wapige picha na kuipelekea ile NGO yao ya haki zabinaadam
Hilo la kuua waandamanaji halihitaji askari feki. Askari halisi wanaliweza vizuri tu, na wameshadhihirisha uwezo, sababu na nia ya kufanya hivyo.
 
Habari zilizotufikia hivi punde ni kuwa Askari Polisi walivamia nyumbani kwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mh Godbless Lema alfajiri ya leo na kumkamata.
Hivi sasa yupo central police ya Arusha.

Sababu za kukamatwa kwake haijajulikana bado....


Tutawajuza kila kitakachokuwa kinajiri
Inawezekana ni huu msako wa majambazi unaoendelea!
 
Mzee hili si swala la kuwauliza hawa wana AR, Lema bado atakuwepo kwa kipindi kirefu hapo. Labda ungetafuta swali lingine la kuuliza. Je umejiuza ni kwanini Korogwe Vijijini walimchagua Profesa Maji Marefu?
Waingezee na Lusinde ambaye ni mpiga debe asiye jua lipi aongee na mahali gani.
 
Back
Top Bottom