Mbunge Godbless Lema akamatwa na polisi

Mbunge Godbless Lema akamatwa na polisi

Alafu mbona hawa jamaa wanapenda kumvamia kibabe kwani wakimuita huwa aendi mwenyewe?
 
Halafu mnauliza ni kwanini raia wanalichukia jeshi la polisi? Hivi kama polisi walimhitaji Lema walishindwa kumpigia simu aripoti kituoni? Kulikua na haja gani kwenda usiku usiku kana kwamba wanaenda kumkamata bin laden? Wapiga kura wake hapo arusha na wafuasi wake nchi nzima wakiona huo uonevu unategemea watakua na mahaba na polisi?
Wanafanya hivyo kwa kutaka sifa na vyeo pia kumkamata bunge huwa ni Ujiko mkubwa sana .
 
Tunajua hata mbowe watamkamata,wakumbuke ili wanalofanya ndio wanazidi kuwapa umoja chadema.wala wasifikiri itasaidia lolote kwenye swala la ukuta.tena inakuwa jambo jema kwao.
 
nawaambieni viongozi wa chadema mtaendelea kukamatwa woote kabla ya tarehe 1 kama mtakaa kizembe. endeleeni kubweteka kufikia tarehe ya maandamano wote mtajikuta ndani....
Toa ushauri basi nini wafanye! Mimi naona njia ya mazungumzo na msajili wa vyama vya siasa bado ina mwanya wa kumaliza hili tatizo
 
Tatizo viongozi wote wa chadema wameshajua wao kukamatwa ni kawaida, kwa hiyo muda wote wameshajiandaa kisaikolojia kukaa selo, labda itafutwe mbinu nyingine
 
Atakuwa kahusika. Maana inaonekana chadema wamehusika ktk kutafuta sare ili askari wao fake waue waandamanaji na baadaye wapige picha na kuipelekea ile NGO yao ya haki zabinaadam


Hivi zile T-shirt walizoonyesha polisi kuna uthibitisho kuwa zilitengenezwa na Chadema?!
 
Hilo ndilo lengo la Kubadirisha mkuu wa mkoa siku chache kabla ya 1st/9.Mtukufu alihitaji mkuu wa mkoa kama huyo ili akamdhibiti Lema.Naamini jua halitazama watakuwa washamwachia.Tofauti na hapo,vyombo vya usalama vinazidi kujiongezea chuki kwa raia wao.
 
Back
Top Bottom