Mbunge Godbless Lema akamatwa na polisi

Mbunge Godbless Lema akamatwa na polisi

kwahio unataka kusemaje? Sijakuelewa
Rejea mchango wangu kwamba Mtanzania anajitambua na anajua haki zake na wapi pa kuzipata, Kikatiba, akizikosa. Wewe bado kwa kushabikia wanasiasa wakutumie kufanikisha malengo yao!

Hivi hujatambua tu kuwa viongozi wa CHADEMA, baada ya kushindwa kuwashawishi Watanzania kuwaingiza Ikulu, kwa kauli mbiu ya 'mabadiliko Lowasa - Lowasa nabadiliko', wanahaha sasa kutafuta jinsi ya kuvuruga juhudi za 'mabadiliko' ya kweli ya Rais Magufuli na viongozi wenzake katika Serikali ya awamu ya 5.

Kuna Watanzania wanajifanya kipofu wakati macho yao yaona kinachoendelea. Wapo wengine wanajifanya hawasikii wakati maasikio yao mazima yanasikia. Ila naamini wana matatizo ya kuchambua pumba na mchele, kama ilivyotokea wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu 2015 kuzungusha mikono.
Muda wa siasa za Kampeni umekwisha wasubiri 2020. Kwa sasa, vyama vya upinzani:

1) Vijiimarishe kaa siasa za maendeleo (kutimiza ahadi) kwenye majimbo waliyopewa ridhaa na Watanzania kuongoza. Kama Serikali, kwa njia yoyote itawawekea vikwazo, halali kuhamasisha Wananchi kupinga hilo.

2) Vitumie mafanikio ya maendeleo katika majimbo hayo kujijenga kisiasa.

3) Hata kama Serikali haikosilewi moja kwa moja, kushindwa kwake kutimiza ahadi zake, kutumike kuiondoa madarakani 2020.

SIKIO LA KUFA HALISIKII DAWA KAMWE
 
Hivi hujatambua tu kuwa viongozi wa CHADEMA, baada ya kushindwa kuwashawishi Watanzania kuwaingiza Ikulu, kwa kauli mbiu ya 'mabadiliko Lowasa - Lowasa nabadiliko'
Proof yako kwamba walishindwa iko wapi??
 
Mikakati mipya ni kukamatwa Viongozi wote wa UKUTA kabla ya tar 30.
 
Proof yako kwamba walishindwa iko wapi??
Du, wewe mzito wa kuelewa au king'ang'anizi cha kutokukubali ukweli.

Katika mengi niliyoandika na kushauri, ni hilo la kushindwa kwa UKAWA kushawishi Watanzania na kaulimbiu ya 'mabadiliko Lowasa, Lowasa mabadiliko' pamoja na kuzungusha mikono, hadi unadai ushahidi!

Ushahidi ni asilimia za kura za Rais na Wabunge na Madiwani ilizopata CCM kwa kauli mbiu ya 'hapa kazitu' dhidi ya vyama 4 vinavyounda UKAWA.
 
jeshi la polisi mkoani kigoma limewakamata viongozi waandamizi wanne wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA kwa kile kinachodaiwa ni kujihusisha na vitendo vya uchochezi. source gazeti la mwananchi
 
"Those who would give up essential liberty, to purchase a little temporary safety, deserve neither liberty nor safety" Benjamin Franklin
Misplaced quote. First liberty sio kama ligi ya simba na Yanga. Pili sioni kama nchi ikilipuka kutakuwa na liberty bali anarchy.

Mashabiki wa shari whether wakiwa upande wa Ukuta au serikali ni wapumbavu tu. Hakuna jina jingine la kuwaita.
 
Ni "proof" kulingana na Katiba ya JMT, ambayo inadaiwa kuvunjwa. Kama mna imani nayo!
Hahahaha ndio maana nikasema proof yenu sio genuine, mnayafahamu yote mliyotenda kwenye kipindi kile mkijua fika kuwa baada ya hapo mtasingizia Katiba.
 
Misplaced quote. First liberty sio kama ligi ya simba na Yanga. Pili sioni kama nchi ikilipuka kutakuwa na liberty bali anarchy.

Mashabiki wa shari whether wakiwa upande wa Ukuta au serikali ni wapumbavu tu. Hakuna jina jingine la kuwaita.
umenena la msingi,, mtu mwenye akili atasimamia ukweli hatatetea vyama vya siasa maana hivi vinaangalia maslahi yao sio maslahi ya taifa kwa ujumla,,, tufikilie kabla ya kujaji
 
Back
Top Bottom