Mbunge Godbless Lema akamatwa na polisi

Mbunge Godbless Lema akamatwa na polisi

Hivi mbunge akiitwa kuripoti Polisi atakimbia?

Halafu bado kuna mtu anadhani watu watakuwa na imani na cops?

Mimi binafsi ningekuwa Polisi ni majambazi tu ndio ningekuwa nayakamata kwa ambush, watu wengine ni wakuandikiwa tu wito wa kuitwa polisi au kiwaita kwa simu na wanajisalimisha wenyewe.

Waziri Mwigulu Nchemba amewataka wauwaji waliouwa Polisi wetu wanne wajisalimishe, sasa napata shida kidogo kwa mbunge kutopewa fursa hiyo ya kujisalimisha.

Polisi maboresho: msitishe raia wema wanaotumia social network bali someni michango ya raia wema humu itawasaidia sana kuwa na jeshi la Polisi la kisasa ambalo litakuwa ni PT Pride.

Kama maguvu yanalipa basi sehemu ya kwanza kufanikiwa ingekuwa ni Israel na Palestine conflict.
Ktk nchi zetu hizi za ulimwengu wa tatu, hakuna kanuni mahsusi ya kumkamata aliye ihalifu sheria, huku ukihakikisha ushahidi wa uhalifu wake ukiwa ktk uasilia wake, zaidi ya kumuingilia "in four"...
....hata wa dunia ya kwanza, wamekubali muondoko huu kivitendo, na wameiga!
Hongera jeshi letu la polisi, kwa kutoangalia "makunyanzi"....
 
Anayetaka mazungumzo ni nani????? Nyie mfanye fujo na wakati huo mtake mazungumzo??????!!!!
Nini maana ya fujo ? Naomba unipe japo kwa kifupi orodha ya fujo zilizofanyika mpaka sasa
 
Badala ya kutuletea Tanzania ya viwanda wanawinda wapinzani kama swala!!
 
Habari zilizotufikia hivi punde ni kuwa Askari Polisi walivamia nyumbani kwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mh Godbless Lema alfajiri ya leo na kumkamata.
Hivi sasa yupo central police ya Arusha.

Sababu za kukamatwa kwake haijajulikana bado....


Tutawajuza kila kitakachokuwa kinajiri
Wanapoteza muda tu
Watamuachia Mchana kweupeee
 
haipiti siku sasa hivi mara huyu kakamatwa mara yule duuh
 
Huwezi mnyamazisha mtu kwa kumuweka mahabusu hata siku moja labda awe hajawahi kaa kwa sisi wengine ambao tumeingia huko toka tukiwa darasa la 5 si kwa kushangaa..watafute suluhisho

Sasa huko ndio ataenda kuongea vizuri. Unavijua vyombo vya dola kamanda?
 
Ktk nchi zetu hizi za ulimwengu wa tatu, hakuna kanuni mahsusi ya kumkamata aliye ihalifu sheria, huku ukihakikisha ushahidi wa uhalifu wake ukiwa ktk uasilia wake, zaidi ya kumuingilia "in four"...
....hata wa dunia ya kwanza, wamekubali muondoko huu kivitendo, na wameiga!
Hongera jeshi letu la polisi, kwa kutoangalia "makunyanzi"....
Kwanza napenda kukupongeza kwa kubahatika kuwa quoted na mtu kama mimi kwa upuuzi huu ulioandika, maana huwa sina muda na watu kama wewe.

Kwa sababu hujui hata PGO ni nini, wacha nikudharau tu na kukuignore for good.
 
1299d829fcb8c424175b70568432d597.jpg
Ngoma imekolea.
Ahahaaaah...
Mkuu...
Hii picha nusu ivunje mbavu zangu..!!!
Sawa...
Nachojaribu kukiona na kufikiria ni kwamba SERIKALI imeamua ianze kuuvunja UKUTA taratibu kabla ya tarehe 1...
Hii inafanyika kwa kukamata viongozi wote na kuwasweka mahabusu...
Baada ya hapo UKUTA utakua ni hopeless..!!!
 
Kumbe hii nchi ina hati miliki??
Sivyo.Lkn kwa sababu nchi hii hakipo chama pinzani makini bado CCM Chakii wataendelea kuongoza tu hadi hapo wapinzani wa kweli watapopatikana.Kinachotufanya(Baadhi yetu)tusiwaamini no huko kushindwa kwenu kusimamia hoja na takarashi zenu!Hilo ni tatizo kubwa.Hamjajipanga kimkakati na ki-sera pia.Itoshe kusema,ninyi bado ni GENGE fulani la watamanio madaraka na si uongozi.JIPANGENI na hasa punguzeni UTOTO.
 
Huwezi mnyamazisha mtu kwa kumuweka mahabusu hata siku moja labda awe hajawahi kaa kwa sisi wengine ambao tumeingia huko toka tukiwa darasa la 5 si kwa kushangaa..watafute suluhisho
Wanadeal na objects badala yakudeal na passion+ spirit
 
Watakamata watanzania wangapi?? Wanazidi kuipa kick UKUTA! Wasingeipa promo namna hii isingekuwa hot! Sasa hata watoto wadogo wanajua nini maana ya UKUTA, serikali ndio imeipandisha chart UKAWA! Hata wakiwakamata hali bado ni tete
 
Badala ya kutuletea Tanzania ya viwanda wanawinda wapinzani kama swala!!
Hakuna muwekezaji ambaye anaweza kuwekeza kwenye nchi ambayo haijulikani kesho kukicha kunazaliwa sheria gani mpya.

Kabla ya watu makini hawajatumbukiza pesa zao sehemu wanaangalia kwanza risk management.

Tanzania tutapata wawekezaji kwenye sekta madini, mafuta na gesi maana huko risk yao ya kupata hasara ni sawa na hakuna.
 
Back
Top Bottom