Eric Ongara
Senior Member
- Sep 19, 2006
- 165
- 8
Mkandara Heshima na kwako pia,
Kwenye sera ya majimbo kutakuwa na serekali za majimbo na wilaya, sioni ni kwa jinsi gani tutatua miji mingine na kutengeneza mmoja. Kwa sababu ya mgawanyo muafaka wa mapato ya rasiliamli na ushiriki wa wananchi, ambapo watakuwa na nguvu ya kuwajibisha viongozi wanaofanya vibaya miji mingi itasonga zaidi.
Nisichokubaliana na wewe ni kwamba Tz ilikuwa na Ukabila, Tukirejea mfano wako wa Afrika kusuni, weupe waliwabagua weusi. Je hapa Tz, kabla ya Nyerere kubadili jina toka Jimbo mpaka mkoa(maana aleendeleza mfumo ule ule wa wakoloni) nani alikuwa anabagua mwingine? Kabila gani lilikuwa linabaguliwa na jingine?
Je Nyerere angeibuka na sera ya majimbo kubalisha mfumo wa kichifu ukabila ungekuwepo Tanzania?
Mimi siamini wala sishawishiki kwamba Tanzania ilikuwa na ukabila, ila wapo watu wachache wabifsi wenye kupenda ukabila.
Nyerere alitaka Nchi iwe na muelekeo mmoja, mfumo mmoja wa utawala. watu wenye ukabila wasingekubali kirahisi kupoteza mamlaka yao na mamlaka yao kupewa watu wengine! Wangepinga na wafuasi wao wangepinga sana.Tungesikia machifu kazaa wamewekwa kizuizini, kwa maana makabila yaliendelea kuwepo na machifu bado waliendelea kuheshimika sana kwenye jamii zao. Nashindawa kuona ukabila uliokuwepo Tanzania, ambao ilikuja kuondolewa na MaDC na maRC!
Pia zilikuwepo fursa nyingi za ukabila kuchomoza wakati ule, kulikuwa na fursa ya vyama vingi,kabla ya kufutwa, vyama vingapi vilikuwa na mguso wa makabila? Kwanini hawa machifu waliondekeza ukabila wasingejiunga au kuanzisha vyama vya kikabila vikitetea maslahi ya makabila yao? Mbona ilikuwa raisi hivyo kuondoa ukabila?
Mchanganyiko baina ya makabila utakayoletwa na mgawanyo mzuri wa mapato ya rasilimali ndio suluhisho la "hofu" ya "ukabila".
Hulka pia huchangia watu kutengeneza sera na mifumo ya kibaguzi. Makaburu walimuona mtu mweusi ni kiumbe dhaifu na anapaswa kuwatumikia kwa sulubu ndio maana wakabuni mfumo wa kikandamizaji.Mifumo hubuniwa na watu kwa maksudio fulani, kama una hulka ya ubinafsi utajenga mfumo wa kufanikisha lengo.Ndio maana Serekali inakuwa ngumu kubadili katiba kwa maana wanafaidikia na mfumo mbovu wa sasa.
Hoja ya kusema Mzaramo hataweza kuwa Gavana wa kanda ya ziwa haina mantiki, kwani leo hii Mzaramo anaweza kugombea na kushinda u meya au ubunge Bariadi? Je kwanini Halmashauri ya zisitunge sheria ndogo za kibaguzi/kikabila! Mbona kuna mianya mingi tu ya kuweza kuendeleza ukabila katika mfumo wa sasa? Watanzania wangekuwa wakabila wasingeshindwa kutumia mianya hii,ukabila si tatizo la msingi Tanzania na mabo ya msingi yataposhugulikiwa litajimaliza.
Naendelea kusisitiza kuwa umoja wa watanzania upo hatarini kila siku, ubinafisi na ufisadi unalishambilia vibaya taifa kila siku.
Kwenye sera ya majimbo kutakuwa na serekali za majimbo na wilaya, sioni ni kwa jinsi gani tutatua miji mingine na kutengeneza mmoja. Kwa sababu ya mgawanyo muafaka wa mapato ya rasiliamli na ushiriki wa wananchi, ambapo watakuwa na nguvu ya kuwajibisha viongozi wanaofanya vibaya miji mingi itasonga zaidi.
Nisichokubaliana na wewe ni kwamba Tz ilikuwa na Ukabila, Tukirejea mfano wako wa Afrika kusuni, weupe waliwabagua weusi. Je hapa Tz, kabla ya Nyerere kubadili jina toka Jimbo mpaka mkoa(maana aleendeleza mfumo ule ule wa wakoloni) nani alikuwa anabagua mwingine? Kabila gani lilikuwa linabaguliwa na jingine?
Je Nyerere angeibuka na sera ya majimbo kubalisha mfumo wa kichifu ukabila ungekuwepo Tanzania?
Mimi siamini wala sishawishiki kwamba Tanzania ilikuwa na ukabila, ila wapo watu wachache wabifsi wenye kupenda ukabila.
Nyerere alitaka Nchi iwe na muelekeo mmoja, mfumo mmoja wa utawala. watu wenye ukabila wasingekubali kirahisi kupoteza mamlaka yao na mamlaka yao kupewa watu wengine! Wangepinga na wafuasi wao wangepinga sana.Tungesikia machifu kazaa wamewekwa kizuizini, kwa maana makabila yaliendelea kuwepo na machifu bado waliendelea kuheshimika sana kwenye jamii zao. Nashindawa kuona ukabila uliokuwepo Tanzania, ambao ilikuja kuondolewa na MaDC na maRC!
Pia zilikuwepo fursa nyingi za ukabila kuchomoza wakati ule, kulikuwa na fursa ya vyama vingi,kabla ya kufutwa, vyama vingapi vilikuwa na mguso wa makabila? Kwanini hawa machifu waliondekeza ukabila wasingejiunga au kuanzisha vyama vya kikabila vikitetea maslahi ya makabila yao? Mbona ilikuwa raisi hivyo kuondoa ukabila?
Mchanganyiko baina ya makabila utakayoletwa na mgawanyo mzuri wa mapato ya rasilimali ndio suluhisho la "hofu" ya "ukabila".
Hulka pia huchangia watu kutengeneza sera na mifumo ya kibaguzi. Makaburu walimuona mtu mweusi ni kiumbe dhaifu na anapaswa kuwatumikia kwa sulubu ndio maana wakabuni mfumo wa kikandamizaji.Mifumo hubuniwa na watu kwa maksudio fulani, kama una hulka ya ubinafsi utajenga mfumo wa kufanikisha lengo.Ndio maana Serekali inakuwa ngumu kubadili katiba kwa maana wanafaidikia na mfumo mbovu wa sasa.
Hoja ya kusema Mzaramo hataweza kuwa Gavana wa kanda ya ziwa haina mantiki, kwani leo hii Mzaramo anaweza kugombea na kushinda u meya au ubunge Bariadi? Je kwanini Halmashauri ya zisitunge sheria ndogo za kibaguzi/kikabila! Mbona kuna mianya mingi tu ya kuweza kuendeleza ukabila katika mfumo wa sasa? Watanzania wangekuwa wakabila wasingeshindwa kutumia mianya hii,ukabila si tatizo la msingi Tanzania na mabo ya msingi yataposhugulikiwa litajimaliza.
Naendelea kusisitiza kuwa umoja wa watanzania upo hatarini kila siku, ubinafisi na ufisadi unalishambilia vibaya taifa kila siku.