Mbowe: Sidaiwi hata senti NHC

Mbowe: Sidaiwi hata senti NHC

gasto genaro

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2014
Posts
780
Reaction score
554
Habari zenu wakuu,
Leo Gazeti la Tanzania Daima kuna habari isemayo kuwa, Mbowe aendelea kusisitiza kuwa hadaiwi senti yoyote na NHC.

Habari hiyo imeandikwa kwa maandishi yenye rangi nyekundu kuonesha msisitizo nadhani. Maana habari nyingine zote zimeandikwa kwa rangi nyeusi.
Siyo kitambo sana tangu Mahakama izuie NHC kupiga mnada mali za Mbowe hadi hapo Kesi ya msingi itakapotatuliwa.

Najiuliza tu, ilikuaje NHC ikamwacha Mbowe muda mrefu hivyo bila kulipa kodi?? Kwa mawazo yenu wadau mnaonaje hili suala? Mkipanga logic zenu, kuna angalau Mantiki yoyote inayokuja kwamba Mbowe anadaiwa kweli?

Nawasilisha..
 

Attachments

  • 1473479855020.jpg
    1473479855020.jpg
    73.1 KB · Views: 97
sidaiwi hata senti
mahakama imepiga mnada

wakati huo huo kuna mwanasheria nguli kama Tundu.....

tumechoshwa na manenomaneno wachukue hatua kisheria ili kama kweli hawadaiwi waje walipwe fidia ya usumbufu n.k
 
sidaiwi hata senti
mahakama imepiga mnada

wakati huo huo kuna mwanasheria nguli kama Tundu.....

tumechoshwa na manenomaneno wachukue hatua kisheria ili kama kweli hawadaiwi waje walipwe fidia ya usumbufu n.k
Kweli. Kama anadaiwa kweli, zitakwepo documents na kama alishalipa, documents zitakwepo pia. Kwahiyo hapa nyaraka ndo zinaongea
 
Mbowe atashinda kesi na itakuwa kashfa kubwa sana kwa CCM.
Acha kutumika, kwaiyo CCM ndio walimpangisha? Ayo ni mambo ya mtu binafsi acha apambane nayo mkianza kuingiza vyama iyo kesi akishindwa inamaana kimeshindwa chama.
 
Hapo mbowe atalipwa na matokeo yake mnakuja kutubebesha mzigo ambao busara ingetumika tusingeubeba, time will tell
 
Mchechu ndo itabidi alipe fidia atajua yeye hela atatoa wapi mana mambo mengine ni ya kujitakia
 
Gazeti lake unategemea liandike tofauti?

MBOWE: SIDAIWI NA NHC, NAMILIKI JENGO KWA ASILIMIA 75 KUANZIA MWAKA 1997
Alipoulizwa kwamba kulikuwa na kesi ambayo ameshindwa kama inavyoelezwa na Serikali na Uongozi wa NHC, Mbowe alisema "waulize hiyo kesi namba ngapi na ya lini. Jambo zito kama hilo linawezekanaje kuwa na kesi na wahusika wasifahamu? Tusubiri tuone".
Chanzo: Mwananchi


Na hapo chini mwananchi analimiliki yeye?
 
Mbowe anazingua. Atoe mapene yetu. Aache wizi wizi wake na kutafuta cheap popularity.

Mbowe tunataka pesa zetu. Acha utapeli.
 
Gazeti lake liendelee kuandika porojo tu lakini hela zetu atazilipa au huenda ameanza kulipa kimyakimya. Unazungumzia kwanini NHC walimuacha kwa muda mrefu bila kumdai, je una uhakika hawakum- demand kulipa deni hilo? hata hivyo kwani ukomo wa muda wa kumdai au kumshitaki umefikia mwisho? La hasha tuna haki ya kumdai chetu, na lazima atalipa tu maana mahakama sio kichaka cha kujificha.
 
Hivi unajua kuwa kuna wizara zinadaiwa kodi?
Hapa tunamuongelea mbowe.
Huwezi ukaja public kupayuka kuwa hudaiwi eti tu kunafulani anadaiwa.
Mbowe alipe deni kodi yetu iende ikafanye miradi ya maendeleo.

Aache utapeli. Utapeli umepitwa na wakati.
 
MBOWE: SIDAIWI NA NHC, NAMILIKI JENGO KWA ASILIMIA 75 KUANZIA MWAKA 1997



Alipoulizwa kwamba kulikuwa na kesi ambayo ameshindwa kama inavyoelezwa na Serikali na Uongozi wa NHC, Mbowe alisema "waulize hiyo kesi namba ngapi na ya lini. Jambo zito kama hilo linawezekanaje kuwa na kesi na wahusika wasifahamu? Tusubiri tuone".
Chanzo: Mwananchi








Na hapo chini mwananchi analimiliki yeye?

Kuna haja gani ya kutumia nguvu kubwa kuwa hadaiwi halafu haya mambo ya kuchanganya GAZETI LAKE NA BIASHARA ZAKE. KUJA kumtetea ndo anazidi kujiaribia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom