Pharaoh
JF-Expert Member
- Mar 18, 2011
- 843
- 158
Ninawajua vizuri watu wa Uzini, ndio walioanzisha joto la Mapinduzi, na ndipo maandalizi yalioongozwa na John Okello yalipotimia, ni waafrika wuesi pure na hawababaishwa na mhindi kama Raza wa CCM, watampa yeyote wale, hata awe Chadema ilmradi wajitambulishe vizuri, na wawashika watu wa maana jimboni, mi baadhi ninao, lakini niko mbali, ningeisaidia Chadema.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CDM) kesho kitazindua kwa kishindo kampeni za Uchaguzi mdogo wa Uwakilishi jimbo la Uzini ambapo chama hicho kimejizatiti kuchukua kiti hicho na kuandika historia mpya ya chama hicho huko Zanzibar.
Taarifa ya CDM imesema vinara wakuu wa chama hicho Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa watawaongoza maelfu ya wanachama wake wa Zanzibar hapo kesho katika uzinduzi unaotarajiwa kuwa wa kihistoria.
Taarifa zaidi kutoka Zanzibar zinasema tayari Dr Slaa amewasili tangu jana kupanga mikakati ya mwisho mwisho.Pia kuna taarifa kwamba kuna shamrashamra za hapa na pale za wafuasi wa CDM.
Habari zaidi:Tanzania Daima.