zumbemkuu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2010
- 11,339
- 9,819
WanaJF,
Niko uzini leo siku ya Tatu. Naomba niwahakikishie wanachadema na wapenzi wenu kuwa tutafanya mpaka kieleweke. Uzini wananchi ni waelewa sana. Wanapenda hoja na si porojo. Wanaopiga porojo kwenye jamvi hili au hawajui kinachoendelea on the ground au wanasukumwa na ushabiki tu kama walivyozoea. Uzini na Zanzibar iko tayari kwa mabadiliko makubwa. Uzini tofauti na watu wanavyofikiri Chadema ina matawi sasa kila Shehia katika Shehia (sawa na vijiji au mitaa bara). Jana nimezindua ofisi, matawi,maskani 7 katika majimbo mbalimbali nje ya Uzini mathalan Mfenesini,Magogoni, Bububu na kadhalika. Kwa hakika moto utakaowaka kutokea Bambi(Uzini) tunakozindulia Kampeni yetu kwa hakika utaunguza Zanzibar yote. Kwa bahati mbaya ndani ya Uzini hakuna network isipokuwa Zantel na hata hivyo hakuna mtandao (internet hadi uende mjinZanzibar. Ndio maana hakuna taarifa. Tunaomba radhi. Lakini kuanzia leo waandishi wa habari watakuwepo ambapo jioni wanaweza kuleta habari wakirejea mjini.
Narudia tena wananchi ni wakarimu sana. Kwa kuwa hakuna guesti kabisa wananchi wamewapokea timu yetu ya Kampein kwenye nyumba zao. Hii ni dalili njema. Tunawashukuru sana.
thanks Dr. tunawaombea mafanikio huko.
mjihadhari sana na CCM maana wakati huu wanatumia mbinu zote chafu wanazozijua ili tu kukwamisha CDM kukubalika znz, naamini kwa nguvu za mola CDM watalichukua jimbo.