HECHE AUNGURUMA KUKAMATWA KWA MHE MBOWE,BAVICHA WATOA SAA 48 AACHIWE HURU
Mwenyekiti wa baraza la chadema (BAVICHA) John Heche amekemea vikali na kulaani kitendo cha polisi kumkamata Mwenyekiti wa Chadema Mh mbowe kwani ni kinyume cha sheria.
Heche ametoa kauli hiyo wakati akiwa katika chuo cha sauti jijini Mwanza wakati alipokuwa akikabidhi vyeti kwa wahitimu 55 wa chadema chuoni hapa.
Amedai kuwa vitendo hivi vimezidi ambapo ndani ya miezi 3 karibu viongozi wote wa juu wa chadema na baadhi ya wabunge wameshakamatwa na kudhalilishwa,ametoa mfano wa viongozi waliokamatwa ni pamoja na Mbowe,slaa,Lema,Ndesamburo,Tindu Lissu,Esther Matiko na Zito Kabwe,pamoja na wafuasi wao wengi.
Amesema kwa sasa BAVICHA halipo tayari kuona viongozi wao wakidhalilishwa na kunyanyaswa,wametoa saa 48 Mh Mbowe aachiwe huru ambapo kesho BAVICHA watatoa kauli kuhusiana na unyanyasaji huo ambao amedai kuwa umeanza kuwa utamaduni,amesema sasa imetosha.
Ametoa mfano mbunge wa CCM (Busega) Dr Kamani alipotakiwa kuhojiwa na polisi ilibidi polisi waombe kibali kwa katibu wa bunge,amehoji kuna utofauti gani wa kisheria kati ya mbunge wa upinzani na CCM katika kukamatwa au kuhojiwa na polisi?.
Amesema Mh Mbowe licha ya kuwa ni mbunge ni kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni ambapo anasimama kama waziri mkuu kivuli,amewataka vijana wa Chadema kuwa tayari kwa tamko la kesho.