MJIMPYA
JF-Expert Member
- Mar 27, 2011
- 506
- 272
HATMA ya kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, itajulikana Jumatatu ya wiki ijayo kwa kuwa mdhamini wake amejisalimisha mahakamani jana.
Mdhamini huyo, Julius Magwe alijisalimisha katika mahakama hiyo saa 5.15 huku akiambatana na wafuasi mbalimbali wa chama hicho na wakili wa upande wa utetezi, Method Kimomogoro.
Wakili Kimomogoro alidai kuwa, mdhamini huyo alikuwa akihudhuria mahakamani siku zote lakini isipokuwa juzi kwa kuwa alikuwa mgonjwa.
Ili kuongeza nguvu katika utetezi wake, Magwe aliwasilisha vielelezo mahakamani hapo ikiwemo cheti cha daktari aliyemruhusu kupumzika.
Wakati mdhamini huyo akijisalimisha mahakamani mkoani Arusha, jijini Dar es Salaam Mbowe aliitisha mkutano na waandishi akidai kuwa alikuwa sahihi kutokwenda mahakamani kama alivyopaswa.
Katika mkutano huo, Mbowe alisema atasimamia haki yake kwa gharama yoyote iwapo Polisi watatekeleza agizo la kumkamata kwa madai ya kudharau Mahakama.
"Ni bora ufe umesimama kuliko kuishi umepiga magoti," alisema Mbowe na kusisitiza "huu ni uonevu wa polisi, tutaupinga kwa nguvu zote," alisema Mbowe wakati akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za Bunge kupinga madai kuwa ameidharau Mahakama.
Juzi Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, Charles Magesa alitoa amri ya kukamatwa kwa Mbowe na mdhamini wake kwa kutofika mahakamani siku hiyo, kitendo kinachotafasiriwa kuwa ni kuidharau Mahakama.
Wakati Mbowe akijitetea kuwa alikuwa sahihi, Mbunge mwenzake Godbless Lema (Arusha) alifika mahakamani na Philemon Ndesamburo (Moshi Mjini) alituma mdhamini jambo lililotafsiriwa kuwa waliheshimu Mahakama.
Wakati huo huo Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani bungeni, Tundu Lissu alisema Mbowe hakuhudhuria mahakamani katika tarehe zote mbili kwa kuwa amekuwa akihudhuria vikao vyote vya kamati mbalimbali za Bunge.
Lissu ambaye pia ni mwanasheria, alisema mila na desturi za kibunge za Jumuia ya Madola zinataka kinga ya wabunge dhidi ya kukamatwa iwe na nguvu wakati wa mkutano wa Bunge pamoja na muda muafaka wa kutosha kabla na baada ya mkutano wa Bunge.
"Hivyo Mbowe akiwa ndani ya gari lake la ofisi, haruhusiwi kukamatwa, akiwa nyumbani kwake, akiwa humu ndani na hata akiwa barabarani ni eneo la Bunge kwani yuko hapa kuhudhuria vikao vya Bunge," alisema Lissu.
Alidai kuwa mila hizo zinataka muda muafaka na wa kutosha kuwa siku arobaini kabla na baada ya mkutano wa Bunge "Kwa mantiki hiyo wakati Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha inatoa amri dhidi yake, Mbowe alikuwa analindwa na kinga ya Bunge."
Source; Habari Leo
Mdhamini huyo, Julius Magwe alijisalimisha katika mahakama hiyo saa 5.15 huku akiambatana na wafuasi mbalimbali wa chama hicho na wakili wa upande wa utetezi, Method Kimomogoro.
Wakili Kimomogoro alidai kuwa, mdhamini huyo alikuwa akihudhuria mahakamani siku zote lakini isipokuwa juzi kwa kuwa alikuwa mgonjwa.
Ili kuongeza nguvu katika utetezi wake, Magwe aliwasilisha vielelezo mahakamani hapo ikiwemo cheti cha daktari aliyemruhusu kupumzika.
Wakati mdhamini huyo akijisalimisha mahakamani mkoani Arusha, jijini Dar es Salaam Mbowe aliitisha mkutano na waandishi akidai kuwa alikuwa sahihi kutokwenda mahakamani kama alivyopaswa.
Katika mkutano huo, Mbowe alisema atasimamia haki yake kwa gharama yoyote iwapo Polisi watatekeleza agizo la kumkamata kwa madai ya kudharau Mahakama.
"Ni bora ufe umesimama kuliko kuishi umepiga magoti," alisema Mbowe na kusisitiza "huu ni uonevu wa polisi, tutaupinga kwa nguvu zote," alisema Mbowe wakati akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za Bunge kupinga madai kuwa ameidharau Mahakama.
Juzi Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, Charles Magesa alitoa amri ya kukamatwa kwa Mbowe na mdhamini wake kwa kutofika mahakamani siku hiyo, kitendo kinachotafasiriwa kuwa ni kuidharau Mahakama.
Wakati Mbowe akijitetea kuwa alikuwa sahihi, Mbunge mwenzake Godbless Lema (Arusha) alifika mahakamani na Philemon Ndesamburo (Moshi Mjini) alituma mdhamini jambo lililotafsiriwa kuwa waliheshimu Mahakama.
Wakati huo huo Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani bungeni, Tundu Lissu alisema Mbowe hakuhudhuria mahakamani katika tarehe zote mbili kwa kuwa amekuwa akihudhuria vikao vyote vya kamati mbalimbali za Bunge.
Lissu ambaye pia ni mwanasheria, alisema mila na desturi za kibunge za Jumuia ya Madola zinataka kinga ya wabunge dhidi ya kukamatwa iwe na nguvu wakati wa mkutano wa Bunge pamoja na muda muafaka wa kutosha kabla na baada ya mkutano wa Bunge.
"Hivyo Mbowe akiwa ndani ya gari lake la ofisi, haruhusiwi kukamatwa, akiwa nyumbani kwake, akiwa humu ndani na hata akiwa barabarani ni eneo la Bunge kwani yuko hapa kuhudhuria vikao vya Bunge," alisema Lissu.
Alidai kuwa mila hizo zinataka muda muafaka na wa kutosha kuwa siku arobaini kabla na baada ya mkutano wa Bunge "Kwa mantiki hiyo wakati Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha inatoa amri dhidi yake, Mbowe alikuwa analindwa na kinga ya Bunge."
Source; Habari Leo