Edward Sambai
JF-Expert Member
- Nov 16, 2013
- 2,822
- 3,832
Sielewi kama uko makini na unachokiandika, kwani kura alizopata Magufuli alikuwa anashindana na Lowassa au ulitaka apewe nani ili ujue nyingi zilikuwa za wafuasi wa EL.Ile team yake au alikuwa akiwanunua? Kama team yake kweli ina kisasi na CCM mbona Magufuli ilipata 87.....% ya kura za wana CCM?si wangeonyesha hasira zao pale na wote walikuwepo? Acheni kujidanganya mchukuweni halafu muone kweli anawafuasi? Mnaopiga kampeni Jf muulizeni Saanane kimemkuta nini Rombo?
Lakini ukumbuke kuwa tuko kwenye mapambano na kila mtu ana tafuta ushindi na unapotaka kushinda huwezi ukachagua silaha ya kutumia hata kama ina kinyesi utaitumia bila kujali kuwa itakupaka kinyesi ili mradi tu uwe na uhakika kuwa hiyo silaha unayotaka kuitumia itakufanya umshinde mpinzani wako,kama utatumia rungu kumpiga adui yako kichwani sawa tu,kama utampiga na jiwe kichwani ni wewe tu kwani kinacho tafutwa ni ushindi bila kujali ushindi umepatikana kwa namna gani,kwani hujawahi kusikia kibaka kajinasua chini ya ulinzi wa polisi kwa kujipaka kinyesi au baada ya kumumwagia polisi kinyesi?.
Kama maneno haya ni ya kweli basi Chadema nao wanaenda kusambaratika kama ilivyo CCM, Mbowe kwa kumkaribisha maalun huyu Chadema inagawanyika sasa hivi. Mlisema ananuka rushwa leo mmempaka pafyumu gani hadi anukie vizuri? Eti eti mnamwambia ni chama cha watanzania wote basi wakaribisheni akina Chenge, Prof Muhongo, Karamagi, Ngeleja, Rostam na wengine kwa kuwa Chadema ni chama cha Watanzania wote Mbowe please usituharibie chama.
Wamchukue tu , lakini hii sasa itakuwa vita ya ziwa na kaskazini! Labda awe mwanachama wa kawaida tu! Ina maana UKAWA hawawezi kushinda wenyewe mpaka waazime koti kwa jirani? Hili litakuwa doa na maccm ndo yatakapotupigia!
Labda aje kuwa mwanachama wa kawaida vinginevyo narudisha kadi.atasafishwaje huyu fisadi?hapo Zitto atawapigia bao.
Hahahaha et chadema sasaiv wanaomba ushahid ku prov ufisadi wa lowasa, et leta ushahid kwamba lowasa nifisad mbona PCCB awamkamat, naamini lowasa angepitishwa na ccm chadema mwanzo mwisho wa kampen wangehubiri ufisad wa lowasa, SHKAMOO SIASA:banghead:
lowasa hasafishiki hata kwa Jik....
Tetty
Hiyo list of shame ilisomwa lini na leo ni lini, karibu miaka kumi mtu habadiliki?
Kama unamuona Lowassa ni fisadi kwa kuangalia list ile basi Kikwete atakuwa mwalimu wake kwa vile Kikwete ni wa kwanza kwenye list.
Kila siku mnaambiwa aliye na ushahidi wa ufisadi wake atuletee au aende mahakamani.