Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

mbowe usituharibie chama.

We badala yakufurahi mwenye dhambi mmoja akitubu mbinguni ni sherehe kuu..alafu ebu jihoji ni lini chadema kimeyumbishwa na mkazi?ama mpitaji?ebu muulize zito,shibuda na wanzake watakwambia Chadema tulivyo Imara...yaani ni jiwe lililo kataliwa..naam sasa limekuwa jiwe Kuu la KARIBU..
 
aje tu awe mwanachama wa kawaida tupigwe mabomu wote tubambikiwe kesi za ugaidi wote sio kuja kupanda ngazi kwa damu za watu zilizopotea kwa ajili ya chadema mwenyekiti umechemka
 
Mkuu sikusikia/kusoma habari magazetini. Amemtaja kabisa 'Edward Lowassa' au kwa kusema ni chama vha watanzania wote, ndiyo mgu una feel kuwa invited?
Unawasiwasi gani kamtaja Lowassa soma Tanzania Daima au Raia Tanzania au sikiliza kipindi cha Kupaka rangi Magic FM kinaendelea.
 
Nakaribisha ujio wa Lowassa ukawa/chadema Lakini asiwe mgombea urais. Lowassa akipitishwa kugombea urais ukawa nitapiga Kura yangu ya kumchagua Rais CCM.

Mnyika atapata Kura yangu kwa utendaji wake na si tena kwa mapenzi ya chama

Naamini hawezi kugombea urais...lakin pia kakaribishwa tu hatujui kama atakubali na kuhamia...
 
Kama ni hivyo acha ccm waendelee kutawala mpaka utakapo zaliwa upinzani wa ukweli.

Kama maneno haya ni ya kweli basi Chadema nao wanaenda kusambaratika kama ilivyo CCM, Mbowe kwa kumkaribisha maalun huyu Chadema inagawanyika sasa hivi. Mlisema ananuka rushwa leo mmempaka pafyumu gani hadi anukie vizuri? Eti eti mnamwambia ni chama cha watanzania wote basi wakaribisheni akina Chenge, Prof Muhongo, Karamagi, Ngeleja, Rostam na wengine kwa kuwa Chadema ni chama cha Watanzania wote Mbowe please usituharibie chama.
 
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mh. Aikael Mbowe amemkaribisha rasmi Edward Lowassa kwenye chama hicho.

Amesema CHADEMA ni chama cha watanzania wote, ameongeza kusema kuwa mgombea yeyote atakayewakilisha UKAWA ndiye atakayekuwa rais.

Chanzo: Habari Magazetini.

Kata mti panda mti, kata ZZK panda EL. Chezea M4C weye?!
 
Wanaotishia kuhama wote ni magamba na ni wapinzani wa lowassa.
Enzi ya siasa za kijinga Tanzania zimekwisha.
Kama lowassa ni fisadi mpelekeni mahakamani...mbona kubweka tu lowassa ni fisadi kama kambwa kenye mafua!
The monster has to go hell...that's matter.
Nyie bwekeni tu.
 
Unawasiwasi-gani kamtaja Lowassa soma Tanzania Daima au Raia Tanzania au sikikiza kipindi cha Kupaka rangi Magic FM kinaendelea.

Wakat mwingine magazet ya bongo ni mpaka ulisome...unaweza kuta content ni tofaut kabisa...
 
Tuweke ushabiki na unazi pembeni. Kama Lowassa atapokelewa CHADEMA, story ya ''CCM ni chama cha mafisadi'' itazikwa rasmi na kimsingi CCM itarudisha hilo dongo kwa CHADEMA wakati wa uchaguzi na kushinda kiulaini.
 
Back
Top Bottom