Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Kama kweli bac CHADEMA ni wahongo haiwezekani kabla ya Lowassa kukatwa walikuwa wanamlalamikia nahinga watu wamshawishi fisadi wa Richmond kwenye majukwaa yote mnamponda leo hii mnamkaribisha na sihatahama Chadema ila sitakuwa mwanachama wa chama chochote kuanzia pale watakapomkubali Lowassa
 
Nyie Chadema vipi? Hakika nawaambia siku mtakayompokea huyo fisadi ndio mtakuwa mmejimaliza kabisa. Nyie si ndio mliojipambanua kuwa wapinga ufisadi? Kulikoni sasa?
 
Chadema wanamtaka lowassa ili awape trick jinsi ccm wanavyoiba kura.... Na pia wanaitaji wanachama watakao wapa nguvu ili waitoe ccm madatakani.... Mjinga atakae kataa hii opportunity atakia tahaira.... Chadema sio wajinga bali wanataka kumtumia lowassa ili washinde uchaguzi
 
Labda aje kuwa mwanachama wa kawaida vinginevyo narudisha kadi.atasafishwaje huyu fisadi?hapo Zitto atawapigia bao.
Unasema Lowassa ni fisadi ila ukifuatilia utagundua ni kashfa za kuchafuana tu.
Fisadi ni aliyepotezea issue ya escrow
 
Last edited by a moderator:
Wanaotishia kuhama wote ni magamba na ni wapinzani wa lowassa.
Enzi ya siasa za kijinga Tanzania zimekwisha.
Kama lowassa ni fisadi mpelekeni mahakamani...mbona kubweka tu lowassa ni fisadi kama kambwa kenye mafua!
The monster has to go hell...that's matter.
Nyie bwekeni tu.

Huo ushauri nenda ukampe Dr Slaa kwanza maana kabla ya Richmond, Slaa alishamtaja Lowasa kuwa fisadi.....sasa kama alishatubu kama bavicha mnavyosema, basi Slaa ale matapishi yake kwa kumsafisha kwanza.
 
Lowassa akija Chadema na akafanikiwa kuwa rais...hata km anataka kuiba hataweza kwa sababu wanaomzunguka hawatakubali.
 
John Pombe Magufuli amewataka mumuondelee mabunzi ili torch yake iwake vizuri.
 
Habarini wanaccm
Nianze kwa kutanguliza samahani kwa nitakaowakwaza kwani ni bora nizungumze kuliko kukaa kimya nitakuwa mjinga wa ajabu na nitakuwa sijaitendea haki democracy,
Nasikitika kuona wanaccm hawapendi kuambiwa ukweli kisa wanalinda maslahi yao na hii in miongoni mwa mambo yanayofanya chama hiki kiende mrama maana ukisema ukweli baadhi yetu kulingana na Uwezo wa kufikiri basi huona wewe ni mpinzani kwa chama#
Ndg zangu Nchi yangu ni bora kuliko chama hvyo Mara nyingi naweka mbele maslahi ya Taifa kuliko chama,Leo hii tunapoona watu wanakihama chama chetu sio wajinga na sio suala la kuwabeza bali twatakiwa tujiulize kwann watu wanakihama,
Kumetokea mambo mengi sana ndani ya chama ambayo kimsingi yanasababisha wananchi wakichukie chama cha mapinduzi#
Maneno ya wananchi wanasema tatizo sio magufuli bali tatizo ni mfumo wa kulindana,kubebana na kushughulikiana ndani ya ccm ni miongoni mwa sababu zinazowakera wapiga kura.
Tujipange ila kiukweli mtaani hali ni mbaya.
Leo hii atatambulishwa rasmi James lembeli kwa wanakahama lakini pia kunatukio la madiwani wa Simiyu Na madiwani Na wachama wa ccm monduli kukihama chama cha mapinduzi,Huu sio mtikisiko mdogo in mkubwa sana hebu fikiria Hawa watu wanawatu wangapi nyuma na watakieneza nini kwa watu wao lakini pia baada ya kukaa tukatafakari kwa makini tukiohili sisi tumekalia kujipa ushindi wa whatsap na pale mtu anapoamua kufunguka kwa kusema kweli basi atachukuliwa kama unakipinga chama ila tuamini kuwa wananchi wa leo sio wale wa Mwl Nyerere ,Tanzania ya leo sio ile ya Mwl hii ya leo iko tofauti kabisa,Watanzania wanahitaji mabadiliko hivyo wasipoyapata ndani watayatafuta nje,
Watanzania wamechoshwa na umaskini uliokithiri,Wamechoshwa kuona keki ya Taifa wanafaidika nayo wachache,Wamechoshwa na kuhudumiwa chini ya miti,Wamechoshwa kuona rushwa imekithiri,Wamechoshwa na mishahara duni,mikopo hakuna vyuo vikuu,Elimu isiyoendana na hitaji la MTU, Tunahitaji Tanzania mpya yenye fursa sawa kwa wananchi wake .
Niwasihi vijana wezangu tusiwe daraja la wanasiasa tufanye maamuzi sahihi kwa kiongozi sahihi bila woga,Kura moja inathamani kubwa saana kwako mtanzania .
Tukiona nyeusi tuseme nyeusi na tukiona nyeupe tuseme nyeupe bila woga kwa miaka mitano au kumi ni mingi kwa kweli hivyo binafsi sitokuwa tayari kusema nyeusi kwenye nyeupe.
Tuweke maslahi ya taifa mbele.
Ahsanteni.
 
Unasema Lowassa ni fisadi ila ukifuatilia utagundua ni kashfa za kuchafuana tu.
Fisadi ni aliyepotezea issue ya escrow
Kwahiyo unamaanisha Dr Slaa alitumiwa kumchafua Lowassa which means CHADEMA walitumiwa kumchafua,think before you speak.
 
* Mbona watu wanashangaa vitu vya kawaida kwenye siasa....

* Wanachama wa CCM na mashabiki wa Lowassa wanapokelewa CDM kila siku na kupewa kadi za uanachama sembuse Lowassa mwenyewe kuwa mwanachama wa CDM....kugombea kupitia UKAWA ndiyo itakuwa haikubaliki...

* Kama CDM wanamchukua Lowassa waelewe kuwa wananchi wanahitaji maelezo ya kuridhisha...na waandae majibu ya maswali ya CCM kwenye kampeni....
 
Huu uongo haukubaliki. Nimefuatilia magazeti Star TV na ITV, hamna Habari ya Mbowe kumkaribisha Lowassa. Basi si ungetaja gazeti husika? Huu ni umbea wa asubuhi na mapema

DSC09866.jpg
 
Lowassa si mjinga. Anajua wazi kwamba akitoka CCM na kujiunga na upinzani tu basi atawafuata Yona na Mramba Gerezani.
 
Kuwa mwanachama wa chadema siyo shida, shida itakuja kama atapewa kugombea Urais kitu ambacho hakipo. Kuiondoa ccm inahitajika ccm yenyewe ibomoke na hii ndo kawaida katika nchi zote ni lazima chama kikongwe kipasuke ndipo upinzani utapata nafasi. Hamna namna ya kukwepa hili kama tunataka kuiondoa ccm ni lazima tuibomoe kwanza.
 
Back
Top Bottom